Wanaume nimewavulia kofia

Wanaume nimewavulia kofia

Huyo marehemu lazima takuwa alikuwa mtu wa songea
Yalimpata mdogo wangu juzi juzi, sisi tulijua mdogo wetu ndie mke pekee wa shemeji, duh, bahati mbaya Mungu akamuchukua, mbona siku hiyo tulijionea vituko, tulichofanya tulimbeba ndugu yetu tukarejea home, tukawaachia msiba ndugu zake na hao wake wengine waliojitokeza siku hiyo


Jamaa mmoja ambaye ametangulia mbele za haki, alikuwa na michepuko kadhaa, na baadhi yao kumbe alishazaa nao.

Inaelezwa kuwa jamaa alikuwa jumla na watoto 6 wa nje ya ndoa, kila mmoja akiwa na mama yake.

Wanne kati ya hao walikuwa wakike, na wote aliwaita Doreen. Sawa na binti yake wa kwa mke wa ndoa. Jamaa baada ya kufariki, wazazi wenzie nao wamejumuika msibani, basi vilio ni kwa kwenda mbele, kila mmoja analia "weeeee baba Doreen weeee".

Mke wa ndoa na watu wa karibu wakajua ni Doreen wa mke wa ndoa. Ila sasa, kila watu wa karibu wakipepesa macho, wanashangaa, mbona hawa wala sio wa mtaani kuwa wanamjua baba Doreen? Si wakajitosa kuuliza.

Ndipo yakaja julikana ya kuwa kumbe Doreen anayetajwa sio wa hapo nyumbani msibani, bali ni kina Doreen wengine ambao wako wanne na kila mmoja ana mama yake!! Watu wameshikwa butwaa.

Mama Doreen wa kwenye ndoa, taarifa zilipomkuta naye kazimia. Shughuli za maziko zimesimama kwa muda sasa.

Jamani....... kweli huku michepukoni kunatufunza ujanja mwingi, ijapo mwishowe ndio kuumbuka namna hii.
 
Sasa msimamishe msiba ili mfanyaje? mumuulize maiti?.....busara ni kuzika kwanza mambo mengine baada ya kuzika....hao waliowauliza hao kina mama Doreen yupi nao wambea kupita maelezo.....there is nothing new under the sun.....
interesting, isnt't?
 
Back
Top Bottom