Jamaa mmoja ambaye ametangulia mbele za
haki, alikuwa na michepuko kadhaa, na baadhi
yao kumbe alishazaa nao. Inaelezwa kuwa
jamaa alikuwa jumla na watoto 6 wa nje ya
ndoa, kila mmoja akiwa na mama yake. Wanne
kati ya hao walikuwa wakike, na wote aliwaita
Doreen. Sawa na binti yake wa kwa mke wa
ndoa. Jamaa baada ya kufariki, wazazi wenzie
nao wamejumuika msibani, basi vilio ni kwa
kwenda mbele, kila mmoja analia "weeeee baba
Doreen weeee". Mke wa ndoa na watu wa
karibu wakajua ni Doreen wa mke wa ndoa.
Ila sasa, kila watu wa karibu wakipepesa
macho, wanashangaa, mbona hawa wala sio
wa mtaani kuwa wanamjua baba Doreen? Si
wakajitosa kuuliza!! Ndipo yakaja julikana ya
kuwa kumbe Doreen anayetajwa sio wa hapo
nyumbani msibani, bali ni kina Doreen wengine
ambao wako wanne na kila mmoja ana mama
yake!! Watu wameshikwa butwaa, mama Doreen
wa kwenye ndoa, taarifa zilipomkuta naye
kazimia. Shughuli za maziko zimesimama kwa
muda sasa.
Jamani....... kweli huku michepukoni
kunatufunza ujanja mwingi, ijapo mwishowe
ndio kuumbuka namna hii.