Binafsi napata shida sana kuwaelewa wanaume walio wengi.
Unakuta mtu ana mke tena hana kosoro lkn akitokea mwanamke mwingine atatazamwa huyo mpaka utalazimika kusema.
Juzi nilikuwa nakwenda mahali Fulani na mume wangu yeye akiwa anaendesha gari mara tukasimama kwenye zebra kupisha waenda kwa miguu..akapita Dada mmoja mzuri kiasi basi mume wangu alimtazama mpaka alipotokomea.. Haikuishia hapo tulipo fika tulipokuwa tunakwenda muhudumu aliyetuhudumia alikuwa ni mwanamke wakaida tu sana lkn mume wangu ali mtazama mara amkonyeze basi fujo tupu mpaka nikaamua kukatisha kinywaji na kuamua kurudi home.
Nawauliza wanaume kwanini mkiona mwanamke udenda unawatoka? Kwann msilidhike na wapenzi au wake zenu?
Jitathiminini heshima ifuata mkondo.
Nawasirisha.