Wanaume mkiondoka nendeni moja kwa moja.

Wanaume mkiondoka nendeni moja kwa moja.

The Donchop

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2014
Posts
294
Reaction score
381
Habari za mida?
Mimi ni mdada niliyewahi kutendwa na nikaumia sana sana sana hata niliwahi kuona maisha yangu hayana thamani yoyote nilishawahi kujaribu kujiua mara kadhaa lakini ilishindikana maisha yakaendelea na nikazoea kidogo kidogo mwenzangu akaenda kwa wanawake wengine kwa sababu tu kuwa amenichoka.

Amebadilisha wanawake kwa karibia miezi saba sasa toka aniache kila wiki ana mpya hata akawa anapitia hadi wauza baa na wamama walioolewa sasa ametendwa na huyo mpenzi wa baa, amepigwa na kuumizwa sana na huyo msichana, amerudi tena kwangu kuwa mimi ndiye mtu wa kweli kwake, hataki niondoke maishani mwake muda huu hata hamu ya mwanaume sina kabisa.

Nikimtazama kama mpenzi napata hasira na sifurahii kuwa naye sasa namtukana lakini bado ameganda tu jamani Wanaume mkitaka kuondoka nendeni kimoja, hata tukiwapenda vipi kuna muda mioyo yetu inabadilika khaaaaaaaaa....
 
Wakiondoka na wewe utapotea kama kaburi la zamani kwani wakiondoka ule ubavu ulioumbiwa wewe utarudishwa kwa mwanaume utapotea huyo aliekutenda kachukua ubavu wake pambana tu na hali yako kumpata mrithi wa aliekutenda
 
Pole sana The Donchop
Nakuomba uendelee na maisha yako. M-block na hata kama akitumia namba mpya usije jaribu kupokea calls au kumjibu sms zake maisha ni matamu sana.
 
Hiyo hali ya wewe kumtukana inadhihirisha kwamba bado hujamove on! Una hasira naye na usimcheke kwakuwa hata wewe hiyo hali itaendelea kukuandama tu hadi pale utakapokuwa tayari kusamehe kutoka moyoni kisha aidha myasuruhishe mmalizane au kila mmoja ashike za kwake.

Ogopa sana mtu ambaye umemtenda ukahangaika weeee na vidampa huko kisha baadaye unakuja kurudi kwake hakutukani wala nini , hakutolei shombo, ila anakuhurumia kwa kukupa maneno ya kukutia nguvu na kukutaka usikate tamaa maisha ndivyo yalivyo na mwishoni anakwambia yeye ameshapiga hatua haupo tena moyoni mwake - weeeeeeeee utajuta nakwambia.

Nakuahauri kama utaamua kumsamehe hakikisha hamgusani hadi mpime afya zenu kwa utaratibu unaotakiwa ili kuilinda afya yako maana huwezi kujua huko alikopita kapewa mangapi
 
Ukikubali kuwa nae tena basi hakukuumiza huyo,lakini Kama kweli alikutenda basi kuwa na msimamo thabiti tafuta mwingine lasivyo atarudia yaleyale akipata mwingine tena
 
Hebu subiri kwanza, ulitaka kujiua kwasababu ya mwanaume kabisa maisha yalivyo matamu ukataka kujiua ungekufa tu kwani uwepo wako hauna faida na huyo jamaa atakutia na kukubwaga mpaka ukome

Pole lakini
 
Hadi anarudi kwako inaonekana haujamsahau na una mazoea nae sana. Huyo anakuchukulia msukule wake usio na nguvu ya kumpinga.

Mtu akikuumiza kihivyo mfungie vioo kila kona sio anatuma sms moja unajibu mara nne,anapiga unapokea haraka na kuongea kwa furaha kama vile umeambiwa ulitumbuliwa kwa bahati mbaya hivyo urudi kazini na mishahara yote utalipwa.
 
Hapo wewe ndio mwenye maamuzi yaliyo sahihi sababu ndio unayemuona alivyokuwa nyuma na sasa tofauti iko wapi.

Ila pia nikwambie umakini naye unahitajika kwani huenda ikawa ana lake jambo ndio sababu anajifanya kukuganda.
 
Hapo wewe ndio mwenye maamuzi yaliyo sahihi
sababu ndio unayemuona alivyokuwa nyuma na sasa tofauti iko wapi.

Ila pia nikwambie umakini naye unahitajika kwani huenda ikawa ana lake jambo ndio sababu anajifanya kukuganda.
Ndio maana nankiu hakauki kukufuatilia hahahaaaaa big up rafiki
 
Back
Top Bottom