Miss Neddy
JF-Expert Member
- Nov 3, 2013
- 14,681
- 8,707
Last edited by a moderator:
Raha huendana na huba,
huba lijazalo kibaba,
cha mengi yenye mahaba,
kwa hiari bila kukaba.
Wewe mama mimi baba,
Tubebe chetu kiroba,
cha mapenzi na mahaba,
Juu ya sita kwa saba.
Wacha weee.....yote hayo naambiwa mimi? Nisiponenepa mwaka huu ndo sinenepi tena mimi maisha yangu yote...
Ondoa yako mashaka,
Pata amani hakika,
Kunyoa au kusuka,
Chagua lililo mwafaka.
Yote haya ni yako,
yaweke moyoni mwako,
kukonda hapana kwako,
Moyo wangu ni wako.
Nakutakia baraka,
Na kila lenye fanaka,
Siku mwezi hata mwaka,
Uishi kwa Uhakika
Amina tena amina,
Amina tena na tena,
Tena na tena Amina.
Nasema tena Amina.
cc Kaizer, kwa kumbukumbu ya chama.
Mweeh thank yu....I luv yu so mach (sina hakika kama chama chenu kinaelewa maana ya hili neno....)
Chama siyo tu kinalielewa hilo neno, bali kinalimiliki.
Ondoa yako mashaka,
Pata amani hakika,
Kunyoa au kusuka,
Chagua lililo mwafaka.
Yote haya ni yako,
yaweke moyoni mwako,
kukonda hapana kwako,
Moyo wangu ni wako.
Nakutakia baraka,
Na kila lenye fanaka,
Siku mwezi hata mwaka,
Uishi kwa Uhakika
Amina tena amina,
Amina tena na tena,
Tena na tena Amina.
Nasema tena Amina.
cc Kaizer, kwa kumbukumbu ya chama.