Wanaume huwa mnahitaji nini?

Tofauti na wengi wanavyosema kuwa ukiwa hivyo unaleta upendo lakini kwangu mimi naona inakuwa tofauti. Badala ya upendo, naonekana kama mtu mjinga ambaye nimekufa na nimeoza kwake kiasi kwamba siwezi kujitetea kwa lolote.
Dada kikubwa hapo ni kupiga goti kwa MUNGU ambae anaweza mmbadilisha yeyote ammbadilishe huyo mpenzi wako naamini ni tamaa tuu ila yote yana mwisho ,mshirikishe MUNGU kwanza kabla ya binadamu
 
Pole sana rafiki.

ACHANA NAE, kwa kimombo, LET HIM GO.

Mnatofautiana values na namna mnavyotazama maisha. Kwake kuwa na multiple relationships ni jambo la kawaida sio rahisi sana kumbadilisha hivyo usicheze kamali na moyo wako. Acha aende, jipe muda mtu sahihi atakuja kwa wakati wake.
 

Umeshasamehe vya kutosha au unataka kuletewa UKIMWI? Piga chini huyo mzinzi na usigeuke nyuma. Kumtusi pia umefanya la maana..
 
Katika swali nimewahi jiuliza na sijapata makawabu ni hili. Sijawahi kujua exactly nini wanaume wanataka. Jamani.. utakua mwema sana, mtiifu na mnyenyekevu kwake. Kasheshe atapojua umeoza kwale utakoma. Dharau, harassments, kukupuuzia pasipo kujali hisia zako etc. Kiujumla unabaki kuwa wa mahusiano ya upande mmoja. Yaan utatesekaaa... i just learnt mtu kama hakupendi hatajali hisia zako. anakupuuzia. Kila siku visa na utabadilishiwa kibao wewe ndo mkosefu. Whats wromg with men jamani. Shida ni nn? Hatuko perfect lakini mnataka nini hasa? Malaika? ..


Mkuu... let him go. Let him go kwakweli. Utateseka sana. Hao ndo vijana bwana.
 
Each time you forgive a man and take him back for the same mistake, he loses some level of respect for you.

Sasa jitafakari. Hapo hujaolewa wala hujazaa unadhalilika. Ukija kuolewa ama kupachikwa tu ki zygote kuna rangi utaacha kuona kweli?
Sijui wanakuwa wameshikwa miguuu,uwiii
 

Binadamu hawana jema hata ujitoe kiasi gani
 

Akufukuzae hakuambii toka

Ijue thamani yako pia utambue sio wanaume wote wana hizo tabia za kifedhuli, wapo wanaume waelewa wengi tuu

Mwache aende akapigwe matendo ya uchungu wa shubiri huyo

Na akishatendwa akataka kurudi kwako akute umepata mwenye mapenzi ya dhati wa kuijua thamani yako

Abaki kujuta tuu
 
Una tracko......??? Maana wanaume tunajijua.... Huenda ni hicho tu!!!

Hahahahaaa
 
Nitafute kwa dm haraka sana kabla hayajakupata makubwa ndugu yangu
 
hahahaa, huwa mnayapendea nini lakini?! Whats so special kwa hio kitu wanaume mnaapendaga??
Unafikiri kuna uspesho basi..yani sisi tunapenda tu kuyaangalia na kwenye doggy yanavyokua yanagonga gonga mapajani basi ni burudaniii😂
 
Wewe ni mwanamke muelewa unatakiwa ukutane na mwanaume muelewa sio huyo asiyejitambua. Usibadilike tabia sababu ya kukutana na mpuuzi m'moja. Wanaume wazuri wapo wengi tu.
 
Jamaa anatumia mbinu zitumiazo timu kubwa za mpira wa miguu za kutoa mkataba wa mwaka mmoja kwa wachezaji ambao umri umeenda ama hawana umuhimu sana a.k.a team players. Sina maana ya kukukosea ila nakuambia tu hujajua how expensive you are. Jamaa anakufungia baraka zako na kukufanya pisi ya burudani pale anapotoswa huko. Amka unajizibia njia, fungua njia kwa wenye nia ama achana naye ujipange upya.
 
Mpuuzi huyo piga chini atakuja mwenye kujua thamani yako..namshukuru Mungu ninae ambaye Yuko humble Kama wewe na sithubutu kumzingua cuz Najua thamani ya kuthaminiwa nae
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…