Kuna vituko sana nchi hii
1. Leo Jecha anatoka na vifungu vya sheria, hakuwahi kueleza vifungu vilivyompa haki yeye binafsi au tume ya uchaguzi kufuata uchaguzi
2. Jecha hajatoa kifungu cha katiba kinachoonyesha utaratibu wa uchaguzi wa marudio. Nimeipitia katiba ya ZNZ ya 1984 na marekebisho yote sikuona kitu kinaitwa uchaguzi wa marudio wa nchi nzima isipokuwa wa eneo lenye utata
3. Jecha hajatoa kfungu anachosimama nacho kufuta matokeo.
Alikuja na malalamiko 10 ambayo leo hayaongelei amebaki na la kujitangaza
4. Jecha hajaonyesha kifungu cha kujitangaza kinatoa hukumu gani kwa aliyefanya
5. Jecha anasema majina yatakuwa yale yale bila kutueleza sheria za tume yake na katiba zinasemaje
6. Jecha huyo huyo anayesema wagombea ni wale wale anatoa ulinzi kwa waliokubali kushiriki. Hawa waliokubali kushiriki ni wapi ikiwa majina ni yale yale kama alivyosema hapo juu?
7, Jecha anasema tume itatoa ulinzi. Ulinzi na usalama wa wagombea hautolewi na tume kwasababu si mamlaka yake. Tume inaomba ulinzi kutoka vyombo husika!
8. Jecha aliwahi kukaririwa na gazeti moja akisema amethibitisha vyama kutoshiriki.
Leo hajarudi kufuta kauli ile anapandikiza nyingine. Jecha anajua anachosema?