Tetesi: Wanasiasa na mipango ovu ya kuiua E-GA

olimpio

JF-Expert Member
Apr 5, 2023
402
834
E-GA ni taasisi inayoratibu serikali mtandao, ni taasisi ambayo inajenga mifumo karibu mingi sana inayotumika na serikali.

Serikali imeokoa pesa nyingi sana kutoka nje ya nchi na imetoa ajira kwa wazawa. Zaidi sana taarifa na usiri ama unyeti wa taarifa za serikali umeongezeka baada ya mifumo ya ndani kuanza kutumia

Nini kinaendelea kwa sasa?
wanasiasa kadhaa ambao sitawataja leo wanaratibu mpango wa kuiua E-GA ili mifumo ya serikali ianze kutengenezwa nje /ku out source kwa jina la kiluguru.

Je hawa wanasiasa wananufaikaje?
wanasiasa hawa wamesha weka hisa zao kwenye kampuni kadhaa ndani na nje ya nchi ambazo wakisha iua EGA , watazipa kandarasi hizo kampuni ambazo nyuma ya pazia ni zao , wanakuja kwa mgongo wa sekta binafsi lakini ukweli sio sekta binafsi , ni matumbo binafsi.

Mpaka sasa wamefanikiwa kuwang'oa E-GA TRA , tayari TRA anakamilisha ununuzi wa mfumo kwa zaidi ya Bilion 12 za kitanzania(TZS).

Mfumo mwingine TANESCO upo njiani.

Hali ni mbaya sana, wanamtafuta Mkurugenzi wa E-GA ikibidi auawe maana anakwamisha madili

************************* UPDATES********************
Taarifa Mpya tulizozipata zinaeleza juu ya uhusika ya Viongozi waandamizi toka taasisi mbalimbali za serikali na wanasiasa kadhaa kusuka mpango huu wa kuifuta E-GA . Script iko kama hapa chini.

1.E-GA iwe moved from ofisi ya rais utumishi kwenda Wizara ya TEHAMA chini ya Waziri Nape Nnauye.
2. Ikishafika wizara ya TEHAMA , haraka haraka mswaada wa kuninafsisha mashirika na taasisi kadhaa za umma utapitishwa , na moja ya taasisi za kubinafsishwa itakua ni E-GA.

3. Wakisha kubaliana bungeni, E-GA itachukuliwa rasmi na kikundi flani ambacho kitakua kimetegesha Kampuni flani kuimeza E-GA.

4. Watumishi waliopo E-GA baadhi watasambazwa kwenye taasisi mbali mbali wengine watabaki kwenye hio kampuni binafsi , kama ilivyo kwa AIRTEL ambapo serikali ina share kadhaa.


Rai yangu: Waziri Nape Nnauye huu ni mtego unategewa , ng'amuka mapema , unaangushiwa jumba bovu .
NOTE: Majina ya wahusika yapo tayari , hayatakua shared hapa kulinda policy za platform hii.
 
Kimsingi kuna taasisi fulani ni consultant wa hiyo mifumo aisee kwa miaka 4-5 existence yao ni kama haipo! Wao ndo walikuwa quad wa epicor kuanzia ver 7.0 hadi 10.2 ambayo ilikuja phase out baada ya MUSE.

Vita kubwa ipo kwenye mfumo wa bill wa serikali wa GePG maana hapo haipotei hata mia...each sent inakuwa countable as long as bill inalipwa thru control number!
MUNGU ATUSAIDIE
 
Kimsingi kuna taasisi fulani ni consultant wa hiyo mifumo aisee kwa miaka 4-5 existence yao ni kama haipo! Wao ndo walikuwa quad wa epicor kuanzia ver 7.0 hadi 10.2 ambayo ilikuja phase out baada ya MUSE.

Vita kubwa ipo kwenye mfumo wa bill wa serikali wa GePG maana hapo haipotei hata mia...each sent inakuwa countable as long as bill inalipwa thru control number!
MUNGU ATUSAIDIE
Magenge ya kihalifu na ufisadi bado yanaharibu serikali
 
Nina kijana wangu ambaye ametoka kwenye kiuno changu aliyebobea kwenye kuunda mifumo ya kielekroniki, ameniambia kuna watu wanategemea kupata 10% ndio hao wanaocheza na mifumo ili ionekane haifai kisha deals wapewe watu wao.
na kuna mbunge juzi anasimama kumtetea kijanammoja eti ana akili sana , moyo uliwaka kwa hasira , kijana anayetetewa ana miliki kampuni ambayo kawekwa na wanasiasa, anapiga pesa anawapa mabwana zake wana siasa ni aibu kubwa sana na wanasiasa wanajua mpaka wamefungua tawi Dubai , ni genge la kihalifu lipo serikalini linaendelea na kazi wengine ni viongozi wakubwa sana
 
E-GA ni taasisi inayoratibu serikali mtandao, ni taasisi ambayo inajenga mifumo karibu mingi sana inayotumika na serikali.

Serikali imeokoa pesa nyingi sana kutoka nje ya nchi na imetoa ajira kwa wazawa. Zaidi sana taarifa na usiri ama unyeti wa taarifa za serikali umeongezeka baada ya mifumo ya ndani kuanza kutumia....
Kwenye hii dili kipara hakosi! Maana Tanesco alishaipereka India
 
Back
Top Bottom