Kumekuwa na marumbano ya hoja juu ya Rais wa TLS kutoa tamko la mgomo, kwanza kama yuko serious na huu mgomo angeanzia leo tarehe 28/ 8/2017 siku ya kesi yake Kisutu tungejua kweli anamaanisha lakini yeye siku ya kesi yake kairuka ameweka Jumanne na Jumatano ni sababu gani zilizomfanya airuke hii siku ya Jumatatu ni ujanja wa kuwafanya wenzake mazuzu ilii wasiende mahakani wapoteze wateja
Pili mamlaka ya lisu juu ya wanasheria, inajulika kabisa chini ya section 8 ya
Advocate act kuwa mwenye mamlaka ya kukuapisha na kukupa prectising certificate ni jaji mkuu na ndo mwenye mamlaka na maamuzi sahihi Lissu kwenye chama ni sawa na monitor wa darasa ambae hana mamlaka ya kukuachisha shule ila kukuongoza usipige kelele au kukubebea daftari hivyo mwalimu ndo mwenye mamlaka ya kukufuta shule na ndivyo ilivyo kwa Lissu atakuponza ugome then ukifutiwa uadvocate hatakuwa na msaada wowote juu ya maisha yako.
Tatu katika mgomo huo atasimamishaje mahakama, wanasheria wa serikali, na watu binafsi na vipi hakimu au jaji akitoa judgement in exparte yeye Lissu atakussaidiaje maana katika tamko lake la mgomo hajafafanua juu hili endapo mahakama ikaendelea yeye atachukua hatua zipi ina maana utapoteza kazi au utampoteza mteja mwisho wa siku utarudi kulima kwenu.
Nne mara nyingi wanasheria wamekuwa wakijigamba kuwa ili uonekana guillty lazima mahakama ithibitishe beyond reasonable doubt (pasipo shaka) je vipi yeye amethibitishaje juu ya hili na kwa nini anataka kuulisha uma chuki kwa kuuaminisha kuwa lile bomu ni la serikali wakati hajathibitisha pengine kuna maadui wengine mi naona asitake kuwaforce wenzake wamfuate kwa uongeaji wake usio mimi na mipaka then awaalike kumsaidia wakati hajui wanakulaje, wanaishije na wanamikataba gani na wateje wao, je Lissu atawalipia kodi, kuwalisha hapa mjini.
Kwa ushauri wangu wanasheria msikubali kufuata mkumbo yeye ana kazi nyingi na analipwa sehemu nyingi, ubunge, CHADEMA na sheria ni nyongeza mumwachie mwenyewe apambane na hali yake asialike za wenzake maana hamkumtuma kutoa brake mdomoni kwake akili za kuambiwa ongeza na zako inawezekana kwa ujanja wake kachukua diary yake kaangalia siku ambazo hana kesi ndo kaziweka ziwe za mgomo then wewe ugome ufungiwe yeye aendelee na kazi zake.