Wanasheria Mnatungusha Watanzania

Wanasheria Mnatungusha Watanzania

Najua nitarushiwa mawe! Nimejiandaa kwa hilo. Nimeamka na hang over nikitafakari nchi yangu niipendayo inaelekea wapi. Nimegundua wanasheria they have real fuc..k..ed our country. Ukianzia na Chenge Andrew yule ni mwanasheria, Hosea wa PCB amesomea sheria, Mzee Msekwa amesomea sheria, Mzee Sitta aliyeingia kwa mbwembwe kwenye usipika kumbe naye ni msanii ni mwanasheria, wale jamaa walikuwa wana sign mikataba hewa ya deep green ni wanasheria tena wazawa wa nchi hii hii....
Lawrence Masha naye alikuja na issue yake ya kimitego na vitambulisho lohh the list goes on

whats wrong na wanasheria hivi hawana uchungu na nchi yetu?

Ni wanataaluma wa fani ipi ndio unafikiri ni wazuri? Leta data kutoka kwenye Baraza la Mawaziri! Nionavyo suala sio UANASHERIA, bali ni la mtu binafsi! Ndio maana tuna mifano mizuri ya Wanasheria makini kama akina Dk Slaa, Mwakyembe, Halima Mdee na Tundu Lissu! Tukivuka mipaka tunaye Rais Obama ambaye ni mwanasheria mahiri na mtu maarufu sana! Au ulikuwa unamaanisha wanasheria wa Tanzania ndio tatizo?
 
Hawa watu ni blabla tu ya siasa za majukwaani,wametuangusha tangu mkoloni atupe uhuru bandia.Umefika wakati watu wa sayansi tuchukue nchi sasa tuisogeze mbele.
Mazee wote wa 'mchepuo' twendeni tukachukue fomu!
 
Jamani mke wangu ni mwanasheria, ila kila siku namuambia hii fani yenu inaiangamiza nchi kwani mmekuwa wanasheria msio na maadili wala upeo, kama kweli wangekuwa maadili basi nchi hii isingeingia kwenye mikataba mibovu ya madini na wawekezaji feki, hii inamaanisha kuwa pale ambapo waziri ana percent fulani nao hupata ila wanauwezo wa kukataa kusaini kila jambo linalopindisha sheria na kanuni za mikataba au malipo, ila wanasheria wetu huwa hawajiamini na wanashirikiana na mafisadi matokeo yake wanaingizia nchi kwenye matatizo makubwa.

Unamuonea sana mkeo, yeye ni muadilifu, kwa nini umgenerelize na wengine? Mikataba mibovu inatokana na negotiation mbovu, mkataba ni makubaliano ya pande mbili hivyo mkikubaliana hovyo na mkataba utakuwa hovyo tu kinachoandikwa ni kile kilichojadiliwa, mara nyingi wakati wa negotiations wanasheria wanaachwa naomba muelewe hilo. Ni upuuzi wa viongozi wetu kutoona umuhimu wa lawyers wakati wa negotiations.

Ushauri wa kitaalamu kwetu hapa ni kama kelele za mlango,( haumnyimi usingizi mwenye nyumba) mkuu wa nyumba aliambiwa na daktari wake apumzike, akamuangalia, akamcheka na kwenda kuhutubia Kirumba, ghafla kaanguka kisa hakufuata ushauri wa daktari. Kesho yake daktari wake badala ya kusema anajiuzulu kwa ushauri wake kupuuzwa anaita press conference na kutuambia Rais hakunisikiliza lakini ana afya njema.

kama umeajiriwa kusikilizwa halafu husikilizwi acha hiyo kazi fanya kazi na watu wanaokusikiliza, na hii ifanyike hata kwa wanasheria ambao serikali haitaki kuwasikiliza. Mambo yakiwa mabaya lawama kwao, wakati actually hawakusikilizwa.

Wanataaluma mbadilike muwe na principle, mkiwa hivyo wananchi watawaelewa
 
I have to say...Sheria ni field muhimu sana! Ila its an area where one can be creative and manipulative! tatizo kubwa la Tz ni ujinga! Na adui wa sheria ni ujinga! Kama wewe ni mjinga, basi siku zote sheria itakukula! Watz wangapi wanaelewa hata basics za sheria...kama Haki zao? Hii ndo sababu moja kuu imenifanya nisomee sheria...kuondoa ujinga! I think you have come across this saying: "ignorance of the law is not a defence!" Sasa kama wewe utakuwa mjinga na kushindwa kudai haki yako....mwanasheria aliye creative na manipulative atakudanganya kwa kusudi la kukuibia. Na hichi ndicho kinachoendelea Tz. So in the end i have come to agree with Nyerere...Adui mkubwa wa Taifa ni Ujinga,... Tukiondoa huo, basi tutaweza kujipanga sawasawa!
Pia ningependa kuwaunga mkono wale waliotaja morals! We (tanzanians) lack a sense of dignity and moral!

Hivi hiyo red ina maana gani;hatuwezi wote tukasomea sheria na ndiyo maana tunawatumia mawakili. sasa inakuaje jamani kila mtu asiyejua sheria aitwe mjinga? Tuna Walimu, Wahandisi,Maafisa Kilimo n.k. Je wote ni Wajinga? Majigambo mengine ni ya kipuuzi mno.
 
Kwa hiyo hapa issue ni mtu na sio profesion tu wapige chini wote hawa ifikapo october.
 
Muulizeni mtu mzima Nirod Mkono, Juzi kasimamia kusaini mkataba mwingine wa gesi na mafuta kwaniaba ya serikali mmeuona au nao ni madudu!

Kunakiongozi alishawahi kusema wanasheria siyo watu wema, ukisoma hata vitabu vya dini haviowangalie kwajichi jema kwani wanauwezo wa kuangamiza taifa.
 
Hivi hiyo red ina maana gani;hatuwezi wote tukasomea sheria na ndiyo maana tunawatumia mawakili. sasa inakuaje jamani kila mtu asiyejua sheria aitwe mjinga? Tuna Walimu, Wahandisi,Maafisa Kilimo n.k. Je wote ni Wajinga? Majigambo mengine ni ya kipuuzi mno.

Kuna a certain level ya kutojua kitu which equates to ujinga. Kitu kama kutojua the works of the system, ni ujinga! Vitu kama kutojua haki za msingi...ni ujinga! Of course no one knows the whole law hata mwanasheria...lakini kuna a certain percentage mwananchi wa kawaida inabidi ajue.

Kuna vitu vingi sana vinaendelea Tz ambavyo vinaonyesha ujinga wa wananchi. Kwa mfano: Wewe kutojua mshahara wa Rais! Ni haki yako kujua hilo. Kuna ile sheria ya viongozi kutaja mali zao...mbona inakuwa siri? Vitu basic kama ivyo vingetakiwa kufundishwa primary school, badala ya kusoma nani ni waziri wa michezo, nk!

Pia kujua vitu kama formalities za bunge, cabinet, uchaguzi nk ni muhimu! i call those general knowledge!
Kwani wewe leo unahitaji afisa kilimo kukwambia muda wa kupanda mazao, nk? He has the extra special knowledge...lakini wewe bado unatakiwa kuwa na basics...kama jinsi ya kupanda, uhitaji wa kunyeshea mazao, nk!
 
Hawa watu ni blabla tu ya siasa za majukwaani,wametuangusha tangu mkoloni atupe uhuru bandia.Umefika wakati watu wa sayansi tuchukue nchi sasa tuisogeze mbele. Mazee wote wa 'mchepuo' twendeni tukachukue fomu!

Hata siasa ni Sayansi, Uchumi ni Sayansi nk. Unamaanisha sayansi ipi au Engineers, MD nk. Lakini wapo pia Mwakyusa, Mwandosya nk. Mimi nashauri apewe Engineer mmoja nchi itakuwa too mechanical lakini ndiyo tutaweza kwenda mbele. Hawa wana sayansi za jamii tunaona wanatuyeyusha tu na kujineemesha.
 
I hate that professional....binti yangu hatosemea hiyo!

Mkuu Masa hapo umekichinja kizungu afadhali tuandikie kiswahili!! You mean 'I hate that profession!! Samahani kama nimekukwaza mkuu.
 
Mkuu Masa hapo umekichinja kizungu afadhali tuandikie kiswahili!! You mean 'I hate that profession!! Samahani kama nimekukwaza mkuu.

Hahahaha shule za kata babu! usijali
 
Masanilo, usilaumu wanasheria, walaumu wale manaoconcieve hizo plans dhalimu na kuzitekeleza mwanasheria ni mtu wa mwisho na mara nyingi wanakuwa side steped. Kwenye utaratibu wa kawaida kuna procuring process ambayo haiko chini ya mwanasheria, kuna tendering process ambayo wanasheria wanaandika minutes tu hawafanyi recommendations ( eti ni technical), baada ya hapo ndo mkataba unatayarishwa na wanaheria ambao hawakuwepo kwenye negotiations.

Baada ya hapo yanaanza malipo, kuna internal auditors ambao kazi yao pia ni kucheki hivyo vitu kama vimepita process yote ya procurement kama sheria inavyotaka, wao wanapitisha tu.

Sasa hapo mwanasheria ana kosa gani?

Tatizo ni kuwa Watanzania wote hatuna morals, tunataka hela haraka bila kufanya kazi ili wote tuendeshe vogue, tuwe na ghorofa watoto wasome UK, USA, tule movenpick, tushop nje ya nchi , twende vocation South Africa bila kujua kuwa tunafanya hivyo kwa hela ya walipa kodi.


Thanks for that.

Unajua wanasheria tumelalamikiwa sana kutokana na mikataba(contracts) mibovu! The fact is mikataba yote inayolalamikiwa si kwamba imetungwa kinyume cha sheria (they are not ultra vires).

Kinacholalamikiwa ni kwamba what we get from those contracts. In any contract there is what called sufficiency of consideration. Yaani ni lazima upate sawa na unachotoa? Sheria yetu ya Tanzania haisemi ni lazima upate sawa na unachotoa(consideration need not to be adequate), but sufficient as parties may agree. Sasa kama wakuu wanamapendekezo yao, amaboyo unaona si sahihi though they are not illigal, what you can do is to advise them on the effects of the concerned term(s).

Sasa kama wakikataa what do you do? Either you quit the tender or you sign it! Take this point, wewe ni mwanasheria mkuu, kazi yako ni kumshauri raisi, ambaye katiba haimlazimishi kupokea ushauri wowote! Umemshauri, amekataa! what to do? una resign? atakaye kujachukua nafasi yako naye ata resign?

You can see how some times lawyers are place in are hard time. force to do things which, though they are not illigal, are very immoral! Remember Law is not what you feel but what it is exactly in statutes
 
Take this point, wewe ni mwanasheria mkuu, kazi yako ni kumshauri raisi, ambaye katiba haimlazimishi kupokea ushauri wowote! Umemshauri, amekataa! what to do? una resign? atakaye kujachukua nafasi yako naye ata resign? u can see how some times lawyers are place in are hard time. force to do things which, though they are not illigal, are very immoral! Remember Law is not what you feel but what it is exactly in statutes

Any advisor, not only lawyer, worth that title has to do so. You are paid to advise if the bugger who pays you to advise him does not heed to the advise why the hell then do you hang around?
 
Hata siasa ni Sayansi, Uchumi ni Sayansi nk. Unamaanisha sayansi ipi au Engineers, MD nk. Lakini wapo pia Mwakyusa, Mwandosya nk. Mimi nashauri apewe Engineer mmoja nchi itakuwa too mechanical lakini ndiyo tutaweza kwenda mbele. Hawa wana sayansi za jamii tunaona wanatuyeyusha tu na kujineemesha.

Mazee mimi namaanisha sayansi dume kama ulizotaja hapo yani MDs,Engineers..siyo hizo sayansi za jamii za kina Nyerere zilizotulostisha mpaka usawa huu.Hao ndiyo waliojaa CCM,maneno mingi sana,blabla majukwaani,mipango na sera nzuri kwenye makaratasi lakini utekelezaji sifuri.Kwenye top public posts tupate ma realist kama Magufuli.Tupate vichwa kama kina Luhanga,Ngassapa nk
Upo Mukulu??
 
I hate that professional....binti yangu hatosemea hiyo!

Masa umenigusa sana
Binafsi naiona hii profesheni ipo kutuchanganya tuu..mtanisamehe wanasheria kukandia profesheni yenu lakini huo ndiyo ukweli.
I dont believe you in any way. Mifano ni mingi sana tunaishuhudia..Masa ametoa michache ya kwetu bongo
 
Hata siasa ni Sayansi, Uchumi ni Sayansi nk. Unamaanisha sayansi ipi au Engineers, MD nk. Lakini wapo pia Mwakyusa, Mwandosya nk. Mimi nashauri apewe Engineer mmoja nchi itakuwa too mechanical lakini ndiyo tutaweza kwenda mbele. Hawa wana sayansi za jamii tunaona wanatuyeyusha tu na kujineemesha.

anamaanisha degree zinazoanza na BSc. or MSc. na Siyo BA or MA. mkuu mbona unapindisha.
 
Hata siasa ni Sayansi, Uchumi ni Sayansi nk. Unamaanisha sayansi ipi au Engineers, MD nk. Lakini wapo pia Mwakyusa, Mwandosya nk. Mimi nashauri apewe Engineer mmoja nchi itakuwa too mechanical lakini ndiyo tutaweza kwenda mbele. Hawa wana sayansi za jamii tunaona wanatuyeyusha tu na kujineemesha.

Kuna msomi mmoja wa zamani I mean kazaliwa miaka ya 50s aliwahikuniambia kuwa enzizao watu wote wenye uwezo darasani kwa wakati huo walikua wakienda Science 1 yaani PCM na wanaofuata Sc2 yaani PCB and wakatikati walipelekwa comerce na wale walioonekana kutokua na uwezo wa ku conceptualize ndo walienda arts meaning sheria, political science, international relations etc....

Msinipige mawe jamani...najaribu kuangalia kama kuna ka ukweli wa maneno ya huyo msomi wa kutegemewa.... Labda ndo maana Taifa linashindwa kujikwamua kwani wengi wa hao ndo wenye power ya kudecide on issues hasa kuanzia miaka ya 80s kuja mbele mpaka sasa...So lets hope watakapo phase out things will change...Ni mtazamo tu!
 
Nalisikia siku hizo kwamba faculty of law UDSM kulikuwa hamna disco..maisha yalikuwa shwari..at suprise disco ya kwanza ilikumba mwana wa kigogo fulani!! sijui ni kweli au ni maneno ya mitaani, kwa sababu mimi sijasomea hapo.
 
Tatizo si wanasheria tatizo tumekua nchi ya "kitu kidogo' kuanzia matrafiki wanao kula rushwa ya sh 2000 mpaka wanasheria na wanasiasa wanao jilimbikizia mabilioni. Sasa hivi kila profession ina wezi tofauti ni access kwenye pesa na kiasi gani cha pesa.

Wanasheria kutokana na taaluma yao wengi wana access kwenye pesa nyingi. Kama ulivyo sema mkuu Masa siku hizi vijana tuna taka tugraduate leo kesho tuwe matajiri, we have become victims of our own ambition.

Nchi yetu tunalaumu mafisadi lakini ukiangalia vizuri ni eatu wachache sana kwenye hii nchi hawa fanyi ufisadi tofauti ni kiwango tu.
 
Any advisor, not only lawyer, worth that title has to do so. You are paid to advise if the bugger who pays you to advise him does not heed to the advise why the hell then do you hang around?

And why do you have to hang off? Have u committed any legal wrong? Look, we need to see the substance of the subject matter. I've been employed to advise him, I m doing exactly what am being paid for. Whether or not he take my advice is non of my concern.

If he is doing wrongs for not taking my advice, it is you, the public to judge him, to tell him no for other five years he is asking, and not asking me to resign! should the teacher,after taking all possible and reasonable means to make sure his students understand, resign because they have failed? Or the Doctor should leave the hospital because the patient who for whatever reasons has died?

Its high time to see matters in a wider scope, telescopic view I can call, Its true that lawyers like any other profession abuse their offices, but im not prepared at all, to say that they are source of problems we are having
 
Kuna msomi mmoja wa zamani I mean kazaliwa miaka ya 50s aliwahikuniambia kuwa enzizao watu wote wenye uwezo darasani kwa wakati huo walikua wakienda Science 1 yaani PCM na wanaofuata Sc2 yaani PCB and wakatikati walipelekwa comerce na wale walioonekana kutokua na uwezo wa ku conceptualize ndo walienda arts meaning sheria, political science, international relations etc....

Msinipige mawe jamani...najaribu kuangalia kama kuna ka ukweli wa maneno ya huyo msomi wa kutegemewa.... Labda ndo maana Taifa linashindwa kujikwamua kwani wengi wa hao ndo wenye power ya kudecide on issues hasa kuanzia miaka ya 80s kuja mbele mpaka sasa...So lets hope watakapo phase out things will change...Ni mtazamo tu!

Kuna ukweli kwa sana tu...............
 
Back
Top Bottom