wanasarufi hii sentensi ni sahihi au si sahihi?

einstein newton

JF-Expert Member
Oct 18, 2015
1,969
2,672
hivi wanasarufi katika isimu ya lugha ya kiswahili,hii sentensi ni sahihi au si sahihi? "samahani kaka,naweza kukuuliza swali?" NB:katika fikra zangu,nimeona kuwa hii sentensi ina makosa ya "kisemantiki",yaani haijafata mtiririko wa kimawazo au logic,haiwezekani mtenda wa hiyo sentensi aombe kuuliza swali wakati huohuo ameshauliza swali.naweza kuwa sahihi?na kama nipo sahihi na sentensi ikaonekana ina makosa/kosa nililolitaja hapo juu,je muundo sahihi wa hii sentensi ulitakiwa uweje?kazi kwenu wakuu.
 
Hajauliza swali alilokusudia kuuliza ndio,anategemea ridhaa ya yule aseme ULIZA au USIULIZE
 
Hajauliza swali alilokusudia kuuliza ndio,anategemea ridhaa ya yule aseme ULIZA au USIULIZE

mkuu,swala hapa siyo kuuliza swali alilokusudia,kumbuka ombi kuu la mtenda ni kuomba kuuliza swali(hapa haijalishi ni swali gani anataka kuuliza)lakini kabla hajauliza swali ameshauliza swali,mimi naona kuwa hii sentensi ni paradox katika lugha ya kiswahili,haiwezekani mtu aombe kuuliza swali kwa kuuliza swali.sijui tupo pamoja mkuu?
 
mkuu,swala hapa siyo kuuliza swali alilokusudia,kumbuka ombi kuu la mtenda ni kuomba kuuliza swali(hapa haijalishi ni swali gani anataka kuuliza)lakini kabla hajauliza swali ameshauliza swali,mimi naona kuwa hii sentensi ni paradox katika lugha ya kiswahili,haiwezekani mtu aombe kuuliza swali kwa kuuliza swali.sijui tupo pamoja mkuu?

Sawa mdau,
Me naishia hapo
 
Samahani naomba kuuliza swali..?kwani swali ni nini?
Naomba nijibu swali la swali langu kabla hujanipa swali
 
kwa waingereza neno ask lina maana ya kuomba au kuuliza,hapo huyo dada ame omba ridhaa ila bado hajauliza
 
samahani imetumika kama kitangulizi/neno la kumuweka sawa muulizwa swali, kimsingi si swali ila anahitaji ruhusa na usikivu kwa swali atakalouliza
 
kwa waingereza neno ask lina maana ya kuomba au kuuliza,hapo huyo dada ame omba ridhaa ila bado hajauliza

mkuu nimekuelewa,kumbe kuna tofauti ya kuomba ridhaa ya kuuliza swali na kuuliza swali,lakini kuomba ridhaa nini na kuuliza nini?
 
samahani imetumika kama kitangulizi/neno la kumuweka sawa muulizwa swali, kimsingi si swali ila anahitaji ruhusa na usikivu kwa swali atakalouliza

sasa mkuu,sentensi hii ilitakiwa iweje ili huyo dada anayetaka kuuliza swali aulize swali baada ya kupewa ruhusa na mhusika,maana anaposema "...naweza kukuuliza swali?"hapa tayari ameshauliza swali,lakini kivipi aulize swali wakati bado hajapewa ruhusa na mhusika?
 
hivi wanasarufi katika isimu ya lugha ya kiswahili,hii sentensi ni sahihi au si sahihi? "samahani kaka,naweza kukuuliza swali?" NB:katika fikra zangu,nimeona kuwa hii sentensi ina makosa ya "kisemantiki",yaani haijafata mtiririko wa kimawazo au logic,haiwezekani mtenda wa hiyo sentensi aombe kuuliza swali wakati huohuo ameshauliza swali.naweza kuwa sahihi?na kama nipo sahihi na sentensi ikaonekana ina makosa/kosa nililolitaja hapo juu,je muundo sahihi wa hii sentensi ulitakiwa uweje?kazi kwenu wakuu.

Binafsi, ingawa sio mjuzi wa lugha nafikiri hiyo sentensi ilitakiwa kuwa hivi;
Samahani, naomba kukuuliza swali. <kwa maana ya request, hii ni kuepuka kumuuliza mlengwa maswali mawili>

Atakapojibu sawa au hapana, ndipo muuliza swali ataendelea kulingana na mrejesho wa mlengwa!

Ni mtazamo wangu tu wanajamii!
 
Nilidhani ungesema una mashaka na maneno 'swali' na 'kuuliza' kutumika kwa pamoja maana ukishasema kuuliza haina haja ya kutaja tena swali
 
Binafsi, ingawa sio mjuzi wa lugha nafikiri hiyo sentensi ilitakiwa kuwa hivi;
Samahani, naomba kukuuliza swali. <kwa maana ya request, hii ni kuepuka kumuuliza mlengwa maswali mawili>

Atakapojibu sawa au hapana, ndipo muuliza swali ataendelea kulingana na mrejesho wa mlengwa!

Ni mtazamo wangu tu wanajamii!

inawezekana,lakini unaposema "samahani naomba kukuuliza swali".na mwisho ukaweka nukta badala ya alama ya kuuliza(?),kutakuwa hakuna haja ya kusubiri mrejesho kutoka kwa mlengwa wakati hakuna swali ulilouliza.mimi nafikiri unaposema "samahani naomba kukuuliza swali."unatakiwa kumuuliza hilo swali ulilokusudia bila kusubiri mrejesho!
 
Nilidhani ungesema una mashaka na maneno 'swali' na 'kuuliza' kutumika kwa pamoja maana ukishasema kuuliza haina haja ya kutaja tena swali

mkuu hata tukiondoa neno 'swali' katika hiyo sentensi na sentensi ikawa hivi;"samahani kaka,naomba kukuuliza?" still kutakuwa na utata kwanini uombe kuuliza wakati automatically umeshamuuliza?
 
Back
Top Bottom