Wanaowasha full light barabarani usiku

Wanaowasha full light barabarani usiku

Kifaranga

Senior Member
Joined
Jan 6, 2011
Posts
144
Reaction score
31
Habari za jioni waheshimiwa, mo naomba bunge lijalo lipitishe sheria kali kwa wale wanaowasha taa full wakati wa usiku kwani huwa zinaumiza sana, kitu ambacho kinaweza kusababisha kutokuona vizuri na wakati mwingine ajali.

Unakuta madereva wengine wanawasha taa kali kama vile wanawinda maporini usiku. Huwa inakera sana wajameni.

Au kama sheria ipo tafadhali nijulishwe hatua za kufuata.

Ni hayo tuu kwa leo, nawasilisha ....
 
Kuwasha taa FULL usiku sio kosa, zimeundwa ili zitumike kuwashwa usiku. Tatizo linakuja pale Dreva anapowasha taa full wakati wa kupishana na gari nyingine ambapo anamfanya Dreva wa gari hiyo nyingine anayopishana nayo asione vizuri. Dreva anayeheshimu uwepo wa wawatumia barabara wengine na kujua kuwa hata hao wengine wana haki ya kutumia barabara kama yeye hawezi kumfanyia mwenzake makusudi hayo ambayo yanahatarisha maisha ya mwenzake. Wajinga na wapumbavu ndio wanaofanya hayo.
 
Nimeielewa hoja yako.

Mimi nashauri wataalam wetu wa semiconductors na electonics kutoka chuo kikuu, Dit pamoja na Veta wa-designe circuit itakayokuwa na uwezo wa ku kutambua mwanga ikimulikwa kisha inabadili automatically kutoka full light kwenda dimm light.

wirring hiyo ya magari ndio itungiwe sheria kushinikiza kila gari lazima lifungiwe kifaa hicho.

TATIZO LITAKUWA LIMEKWISHA.
 
Ni kweli kuna madereva wengi usiku wanakera sana kwa kuwasha gull light muda wote badala ya kuwasha sehemu ambayo anaona yupo peke yake. Ni ngumu kudhibiti ila ni suala la ustaarabu tu ambao kila mwenye chombo cha moto anatakiwa kuzingatia.
 
Nimeielewa hoja yako.

Mimi nashauri wataalam wetu wa semiconductors na electonics kutoka chuo kikuu, Dit pamoja na Veta wa-designe circuit itakayokuwa na uwezo wa ku kutambua mwanga ikimulikwa kisha inabadili automatically kutoka full light kwenda dimm light.

wirring hiyo ya magari ndio itungiwe sheria kushinikiza kila gari lazima lifungiwe kifaa hicho.

TATIZO LITAKUWA LIMEKWISHA.

Duuuuuh!!
 
Hata mm nina mwaka sasa tokea nimepata ajali mbaya sana baada ya kuwashiwa full na hatimaye kukosa mwelekeo na kugongwa nawasihi madereva wenzangu wawe makini kwa hili
 
Baada ya kuchoka kuwaashiria madereva waondoe full light, sasa nawasha full ila naondoa full light linapokaribia gari ninalopishana nalo. Madereva karibu wote nao huondoa full light wakiona nimeondoa.
 
Habari za jioni waheshimiwa, mo naomba bunge lijalo lipitishe sheria kali kwa wale wanaowasha taa full wakati wa usiku kwani huwa zinaumiza sana, kitu ambacho kinaweza kusababisha kutokuona vizuri na wakati mwingine ajali.

Unakuta madereva wengine wanawasha taa kali kama vile wanawinda maporini usiku. Huwa inakera sana wajameni.

Au kama sheria ipo tafadhali nijulishwe hatua za kufuata.

Ni hayo tuu kwa leo, nawasilisha ....

Mkuu sheria ya usalama barabarani inakataza kuwasha full lights, isipokuwa pale palipo na sababu za msingi na ziwashwe kwa tahadhali.
 
Kuwasha taa FULL usiku sio kosa, zimeundwa ili zitumike kuwashwa usiku. Tatizo linakuja pale Dreva anapowasha taa full wakati wa kupishana na gari nyingine ambapo anamfanya Dreva wa gari hiyo nyingine anayopishana nayo asione vizuri. Dreva anayeheshimu uwepo wa wawatumia barabara wengine na kujua kuwa hata hao wengine wana haki ya kutumia barabara kama yeye hawezi kumfanyia mwenzake makusudi hayo ambayo yanahatarisha maisha ya mwenzake. Wajinga na wapumbavu ndio wanaofanya hayo.

Ni kosa soma sheria ya usalama barabarani itakusaidia kulijua hili wakati gani uwashe au usiwashe.
 
no tatizo kujifunzia gari barabarani badala ya vyuoni hivyo kupelekea watu wengi kutojua matumizi sahii ya taa pamoja na road signs ndo maana kila siku watu hupigwa tochi
 
Nimeielewa hoja yako.

Mimi nashauri wataalam wetu wa semiconductors na electonics kutoka chuo kikuu, Dit pamoja na Veta wa-designe circuit itakayokuwa na uwezo wa ku kutambua mwanga ikimulikwa kisha inabadili automatically kutoka full light kwenda dimm light.

wirring hiyo ya magari ndio itungiwe sheria kushinikiza kila gari lazima lifungiwe kifaa hicho.

TATIZO LITAKUWA LIMEKWISHA.

Dah!umetoa kapoint hapa kiongozi,hii idea yako akiipata mchina lazima aifanyie kazi!Nimegundua tatizo madereva wengi wamejifunza magari kinyemela na leseni wameletewa nyumbani!hawajafundishwa matumizi ya full na beam light,jitu linawasha taa tu lakini halijui km ipo full au beam yani unaliflash lkn hata halistuki,afu utakuta hata swich ya kuweka full na beam halijui na halitaki kuuliza!yani mi yananikera,nimeshaiongea hii mada sana kwny facebuk!Asa mm nimeamua kitu kimoja,kabito kangu taa zake sio kali ila sasa nimefunga sports light kali pale juu,ukinipiga full ntakuflash ili upunguze ukikomaa naziwasha zile zangu za juu,huo mwanga wake lzm usimame la sivyo mtaroni utaingia!mana nshachoka sasa hamna jinsi!
 
Madereva wengine hawajui sheria, hawajui matumizi ya full na dim light.
 
Back
Top Bottom