masdinero masproblemas
JF-Expert Member
- Mar 19, 2022
- 224
- 178
Mtiririko wako una hitilafu kubwa sana. Hitilafu ya lazima chanzo cha kwanza cha ulimwengu kiwe mungu. Kwanini ulazimishe umungu kwenye kila hali? Hakuna hali ya kwamba mungu akakosekana? Anayesema hydrogen atoms mungu wake hizo atoms. Atakayekuja kusema strings utasema mungu wake ni strings? Au weak force? Quantum dynamics? Undefined probabilities?Mungu yupo kwa sababu;
1.Katika maisha yangu nimeshaona wachawi .Wachawi wanafanya uovu hivyo lazima wamtumikie anayewatuma(shetani) hence logically wapo watenda mema wanaomtumikia Mungu.
2.Hakuna asiyeamini Mungu.Wale believers wa big bang theory Mungu wao ni hydrogen atoms zilizofanya collisionna kuunda galaxy.Katika dini Mungu anaweza kuongea n.k.Hivyo chagua Mungu wako ni yupi either hydrogen atoms zilizokuwepo as supernatural or Mungu wa kwenye dini.
NB to atheists:mnasema hakuna Mungu,basi elezea chanzo cha dunia.Kama ni big bang theory,nani aliumba hydrogen atoms.Kama hydrogen atoms hazikuumbwa hence zilikuwepo supernaturally basi hydrogen atoms ndiyo Mungu wenu.
All scientific pioneers who tried to find origin of universe never disbelieved in God.
#Albert Einstein
#Edwin Hubble
#Stephen Hawking n.k
1. Uchawi ni nn? Uchawi unafanyikaje? Unaathiri vipi vitu na watu? Kiimani na kisaikolojia au ina athari za kihalisia? Wewe ndio wale wanaodhani ukiomba kabla ya kuanza safari au mtihani utafika salama au kufaulu? Unadhani mtu akikuendea kwa mganga ufilisike utafilisika kweli bila wewe kusababisha au sababu ingne isiyohusiana na uganga uliofanywa? Nawe ni mmoja wao? Kama ni hivyo pole sana mkuu.
Lakini tuendelee. Ukielewa na kufata taratibu za kitafiti na uchunguzi utagundua hakuna uchawi, wala bahati, wala mkosi, wala miujiza wala viumbe visivyofata sheria asilia. Hakuna anayepaa tu hivihivi. Hakuna anayepona ghafla bila uhalisia wa kibaiolojia. Hakuna anayekufa pasipo sababu za msingi. Hakuna anayedhuriwa kichawi au kwa nguvu zisizopimika. Kila kitu duniani lazima kifate sheria asilia. Hakuna njia ya mkato. Uchawi haupo. Upo kichwani mwako tu. Hakuna haja ya kuongelea sana hili liko wazi sana kwa wenye kufatilia kiundani mambo ya kwenye jamii zetu.
2. Mungu ni nini au nani? Kwa maana za kibinadamu za kawaida hakuna ushahidi wa uwepo wake. Mungu ana ufahamu? Kama ndio basi atoms haziwezi kuwa miungu. Hazina ufahamu wowote. Kama mungu hana ufahamu basi pengine atoms kweli(unajua kuna vipengele ndani vinavyoathiri na vidogo zaidi ya atoms?) ndio miungu yetu. Miungu hii haihitaji imani za kuombwaombwa au kujengewa mahekalu, kutengewa muda na siku fulani na taratibu fulani ili ziridhike kututimizia mambo yetu hapa duniani. Sadaka zetu zitasaidia nn atoms? Ibada zinakuwa hazina maana. Dini zitatakiwa kutoweka kwenyw jamii watakaoelewa miungu hii. Hoja yako ya atoms ni miungu inafaa kupuuzwa mara moja.
Kuna wanasanyansi wana hoja zao kwamba kama uwepo wa kitu mungu unawezekana basi sio mungu aliyehai na kuwepo kila saa na sehemu. Kuna jina wanapenda kulitumia kuongelea hili kundi la imani; Deism. Yaan madai ya hii ni yawezekana alitenga mafiga matatu akainjika chungu akasepa. Kwahiyo mkono wa mungu kwenye dunia hii wala ulimwengu kiujumla. Hayupo tena alishaondoka akatusahau yapata bilioni kadhaa ya miaka. Hapa hakuna mambo ya miujiza, maono, uchawi sijui mapepo, mikosi, bahati, nyota yako sijui na takataka zingine.
Mimi binafsi, kama walivyo wanasayansi na wasio wengi, nasema ulimwengu ulianza bila ya uwepo wa mungu. Kuweka hoja kwamba alianzisha au yupo siyo suluhisho. Bali ni kuongeza tatizo jipya kwenye mtiririko wa suala hili la chanzo cha ulimwengu. Sana sana unaongeza maswali zaidi. Alitoka wap? Ametengenezwaje(hakuna kisichokuwa na mwanzo wa hivihivi tu. Kama ulimwengu lazima uliumbwa basi hata huyo muumbaji wake aliumbwa. Tusizushe umaalumu kama kinga ya hoja)‽ Kwann aanzishe?(Jibu liwe la maana sio ili "aabudiwe" utaanzisha kingine kwann aabudiwe? Bila kuabudiwa hajatimia?) Kwann alilipua muda husika? Alilipuaje? Alikuwa na lengo la kufikia hapa tulipo sasa?
Ukikaa peke yako na imani zako jitathmini sana na mwisho ujikubali kwamba unaamini lakini hujui unachokiamini hata ukisoma likitabu gani la imani haisaidii!
na kuunda galaxy.Katika dini Mungu anaweza kuongea n.k.Hivyo chagua Mungu wako ni yupi either hydrogen atoms zilizokuwepo as supernatural or Mungu wa kwenye dini.