Sasa unaharibu utaribu kiongozi wangu. Jibu maswali niliyo kuuliza kisha uendelee na haya maelezo.Mungu wako, mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, ambaye hapo hapo kaumba dunia ambayo inaruhusu maovu yaweze kutokea, hayupo.
Kwa nini hayupo?
Unakumbuka tumetoka kuongelea habari ya contradiction, kwamba pembetatu yenye nyuzi 180 ambayo pia ni duara lenye nyuzi 360 hapo hapo haiwezi kuwepo?
Kwa sababu ya contradiction?
Mungu wako huyo ni dhana ambayo ipo sawasawa na pembetatu hiyo.
Upande mmoja, anasemwa kwamba ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote. Huu upande ni sawa na pembetatu yenye nyuzi 180.
Upande mwingine, ameumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya yaweze kutokea. Huu upande ni sawa na duara lenye nyuzi 360.
Kama vile ambavyo haiwezekani pembetatu yenye nyuzi 180 ikawa duara lenye nyuzi 360 hapopo, ndivyo Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hatakiwi kimantiki kuumba ulimwengu ambao unaruhusu mabaya.
Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kuumba ulimwengu unaoruhusu mabaya ni contradiction.Kwa nini aumbe ulimwengu unaoruhusu mabaya wakati yeye ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote?
Contradiction hii, inaonesha Mungu huyu hayupo, ni hadithi iliyotungwa na watu tu.
Ingekuwa rahisi sana kukubali uwepo wa Mungu huyu kama ulimwengu ungekuwa hauruhusu mabaya.
Ulimwengu huo ambao hauruhusu mabaya, ungekuwa hauna logical inconsistency na dhana ya kuwepo Mungu, wala usinge contradict uwepo wa Mungu.
Lakini, kwa sababu tunaona ulimwengu ambao unaruhusu mabaya, ulimwengu huu una contradict habari ya kuwepo Mungu na unatuonesha kwamba habari hiyo ni hadithi ya kutungwa na watu tu.
Kama vile contradiction katika habari ya kuwepo kwa pembetatu iliyo duara inavyotuonesha pembetatu duara hiyo haipo, ni tungo ya mtu tu.
Shukrani.