Uthibitisho kuwa Mungu yupo ni kitendo cha wewe kuwepo hapa duniani Leo hii Mungu ndio aliyekuleta
Sasa kama wewe haujaletwa na Mungu hapa duniani basi yupo aliyekuleta tutajie ni nani pia weka ushahi au kama umejileta mwenyewe pia weka ushahidi ili tujuwe kuwa hakuna Mungu
Walionileta hapa ni baba na mama yangu.
Sasa baba na mama yangu ni Mungu?
Na hata ukitaka kwenda mbali zaidi, unajuaje suala ni la "nani" na si nini?
Umekuta jani la muembe mlangoni mwako, hujui limefikaje, badala ya kuuliza jani limefikaje hapo, unauliza nani kaweka jani hapo.
Kama limewekwa na upepo huoni swali lako la nani litakuwa la makosa?
Wewe unaelewa kwamba dhana nzima ya "hiki kimeanzishwa na kile" ukiifuqtilia sana kwenye fizikia inavunjika?
Unaelewa kwamba kwenye level ya quantum mechanics, chqnzo kinaweza kutokea baada ya matokeo na matokeo yakatokea kabla ya chanzo katika mduara usiomalizika?
Unaelewa kwamba muda wenyewe, unaotupa dhana nzima ya kipi kinaanza na kipi kinafuatia, ukiufuatilia sana unavunjika?
Unaelewa "logical non sequitur" ni nini?
Wewe kusema kwamba mimi kuwapo kwangu ni uthibitisho kwamba Mungu yupo, hakuthibitishi uwepo wa Mungu.
Umeandika tu hilo, hujathibitisha ni vipi Mungu kasababisha mimi kuwapo.
Umeeleza jambo la imani.
Imani si uthibitisho.
Mimi naweza kukuambia naamini mimi ndiye Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Imani hiyo hainifanyi niwe Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Thibitisha Mungu yupo, usitoe kauli za imani tu zilizojaa logical non sequitur.