Wanaopiga simu redioni kila siku wanatoa wapi fedha na muda?

Wanaopiga simu redioni kila siku wanatoa wapi fedha na muda?

"Wanapata wapi muda na pesa?" Nijambo ambalo nimekuwa nikijiuliza tokea nikiwa mdogo.

Kuna watu walikuwa vinara wa kupiga simu redioni, leo wengine wamepotea, wengine wamepunguza, watu kama Suzzy Ngodoki, Pagija wa Pagija, Mwili Obale, n.k

Leo wameibuka wengine wanapiga simu kuchangia mada kila redio, utawasikia Clouds kila kipindi, RFA, Redio one, E fm.

Najiuliza hawa watu wanafanya kazi gani? Huu muda wanautoa wapi wakushinda wakitoa maoni redioni? Je, ni ushamba au ni ujanja?

Maoni kutolewa na watu wale wale kila siku, redio hazioni kuna dalili ya kufeli? Wengi wao hutoa maoni mepesi sana, unaweza dhani wanafanya mradi siku isipite bila kuchangia maoni redioni.

Wewe una mtazamo gani? Nani umemzoea kumsikia?
Nihobi tu kama za wana jf, kila dakia lazma upitie humu.
 
"
Leo wameibuka wengine wanapiga simu kuchangia mada kila redio, utawasikia Clouds kila kipindi, RFA, Redio one, E fm.

Najiuliza hawa watu wanafanya kazi gani? Huu muda wanautoa wapi wakushinda wakitoa maoni redioni?

huo muda ni sawasawa kabisa na huo wako unaotumia kuwasikiliza kwenye redio zote hizo mkuu..........
 
Cha kushangaza nikipiga sim nakuta mtandao upo buys, sijui hao wapuuzi huwa wanapigiwa kwa kuwa wanamajina tayari, ukituma ujumbe hausomwi ila wanao sikika kila siku jumbe zao zinasomwa aaaarrg!
 
Cha kushangaza nikipiga sim nakuta mtandao upo buys, sijui hao wapuuzi huwa wanapigiwa kwa kuwa wanamajina tayari, ukituma ujumbe hausomwi ila wanao sikika kila siku jumbe zao zinasomwa aaaarrg!
Wanaita kukamata laini hahaha
 
Titi shara, farida mpimbi,balozi wa kudumu wa e fm sapota ......walikuwepo akina Eido mtoto wa votrotroo in dj fety voice , wale sijui ni wahaa au wasukuma wana kuwa usiku mkali kweny kipindi cha Dj Elly wa clouds fm kuanzia saa saba hadi saa kumi afajir jamaaa wana tuma salamu za kuamshana
 
Back
Top Bottom