Wanaomtetea Prof. Muhongo Sospeter 'Wanaangamia kwa kukosa maarifa'

Wanaomtetea Prof. Muhongo Sospeter 'Wanaangamia kwa kukosa maarifa'

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
12,289
Reaction score
38,942
Mods naomba huu uzi msiuhamishe, msiuchanganye na mwingine. Acha tuujadili ukweli!

Kumekuwa na jitihada za makusudi za kumtetea waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo eti kwa kuwa ni mtendaji bora basi asiwajibishwe kutokana na wizi wa mali ya umma. Huu ni ukosefu wa maarifa na kutokutumia akili kuliko kithiri!

Kwanza kabisa Muhongo Sospeter siyo mtendaji mzuri.

Pili ni mtu wa kujiamulia mambo bila kufuata taratibu na sheria kitu ambacho kimeligharimu taifa kwa kiasi kikubwa!

Je, mnaomtetea Muhongo mna habari kuwa ndiye aliyechangia 13% ya deni la taifa tunaloliona sasa?

Je mnajua kuwa Prof. Muhongo aliwajibishwa na kamati ya maadili ya bunge kwa kuwa aliituhumu POAC iliyokuwa ikiongozwa naZitto Kabwe kabla ya kuvunjwa ambapo alisema kuwa POAC imepewa hongo na Reginald Mengi ili iikwamishe bajeti ya wizara yake kwa mwaka
2014/15?

Baadaye Prof. Muhongo alijieleza mbele ya spika Makinda na kamati ya maadili ya bunge ambapo alikiri mwenyewe kuwa alifanya hivyo ili bajeti ya wizara yake ipite kirahisi eti kwamba hakuitaji usumbufu kutoka kwa aliowaita kuwa wajuaji na hakukuwa na tuhuma zozote za Zitto na kamati yake kupewa rushwa na Reginald Mengi. Makinda akajilaumu sana kwa kuivunja kamati ya Zitto! Muhongo akasamehewa yakafanywa siri, yakapita!

Kama hamjui basi nawaeleza kuwa Prof. Muhongo amekuwa akituhumiwa mara kwa mara ndani ya kikao cha baraza la mawaziri kuwa ni mtu anayelitia hasara taifa kutokana na maamuzi yake ya hovyo na kutokufuata sheria na taratibu za mikataba na manunizi ya umma.


Hafuati sheria za manunuzi ya umma, ni mtu asiyepokea ushauri na amekuwa akilazimisha serikali nzima kusahau mambo mengine kwa ajili ya wizara yake!

Prof. Muhongo amekuwa akitoa takwimu za uongo kwa makusudi mbele ya bunge..Mathalan deni la Tanesco limekuwa likizidi mara mbili kila mwaka na sasa Tanesco
inadaiwa bilioni 100 za Kitanzania ambapo yeye aliingia wizarani Tanesco ikiwa na deni la bilioni 10 pekee hilo analifanya kuwa siri na kutoa takwimu za uongo eti fedha za ESCROW zilibadilishwa kuwa deni la Tanesco kwa IPTL! Utendaji wa huyu mtu uko wapi?

IPTL imekuwa ikizidishiwa malipo kila siku tangu aingie madarakani hilo kaamua kulifumbia macho kwa makusudi kwa kuwa tayari alishakiuka taratibu za mauzo ya IPTL kwa PAP!

Wapo wanaosema kuwa amefanikisha kupeleka umeme vijijini kupitia REA, fine. Je wanajua ni kiasi gani Prof. Muhongo ameidanganya serikali kwa takwimu za uongo na kupikwa ili serikali ihamishie rasilimali zake nyingi REA? REA imepewa kiasi kikubwa sana cha fedha kuliko ambavyo inazalisha! Hilo wanalifahamu?

Ukweli ni kuwa Muhongo amekuwa akitoa taarifa za uongo kwa serikali ili kufanikisha mpango wake wa kuchota fedha, ametoa takwimu na taarifa za uongo bungeni toka alipoteuliwa kuwa waziri! Spika wa bunge kila bunge la bajeti linapoisha amekuwa akimpeleka Prof. Muhongo mbele ya kamati ya maadili ya bunge kutokana na taarifa za uongo ila hilo limekuwa likifanywa siri!
 
we hujui kitu kichwa chako kimejaa matope hata tukueleze nini hutaweza kufahamu
 
wanao mtetea muhongo ni wahuni na wezi wenzake ccm wanalindana wao kwa wao
 
Majenereta yamedoda na yataozea stooni,wafanyabiashara wamekosa vitalu vya gesi,kampuni ya mkono and advocates imekatiwa mirija,Lowasa ameahidi vyeo kwa wajumbe wa PAC,mahela ya mengi kumbuka kumzomea tu prof 3mil,ukichangia na kushinikiza atoke mil 20,mkono kuwakodishia ndege Zitto na wenzake kwenda kwenye harus ya kafulila,Zitto kupewa bil 1.5 na kupewa jukumu la kutafuta wabunge wenye ushawishi kushinikiza prof na katibu wake waondoke,
 
.... Wanaomtetea Muhongo Labda Na Wao Walipata Kamgawo Au Ni Ndugu Na Jamaa Zake, Hakuna Mtanzania Mwenye Ubongo Timamu Anaemtetea Huyu Jambazi Mkubwa
 
we hujui kitu kichwa chako kimejaa matope hata tukueleze nini hutaweza kufahamu

Wewe kichwa chako ni nazi koroma iliyokwishakwanguliwa akili,imebakiza ashk majnoon hata itokee nini utaendeleza mahaba na profesa wako wa kufa na kuzikana.
Hapa nilipo nimeacha kazi yangu kwa fundi kkoo ina siku tatu haifanyiki sababu umeme unazingua.kila ninapopiga simu,kkoo,ubungo,kimara,mwenge,mji mzima hamna umeme na profesa wenu alisema mgao wa umeme utakuwa historia,halafu unatetea ujinga hapa.
Kuanzia ikulu hadi wizara ya nishati kumejaa mafisadi wa nishati ndio maana nasema tanzania haitakuwa na nafuu ya matatizo ya nishati hadi jk na mafisadi wenzie wa umeme akina muongo waondoke madarakani na wasipewe nafasi kupandikiza mtu wao 2015 ili maumivu haya yasiendelee.
 
Bado sijakuona sababu za msingi za kumuwajibisha Professor Muhongo.
 
Huyu Muhongo mbona ana wafuasi wengi hivi?kwa nini? Au ndio watu wa wizarani?
Hii wizara ina mamluki kweli. Mnakumbuka walivyosukuma gari ya katibu wao yule mwizi na wakamfanyia sherehe?dadeki
 
Majenereta yamedoda na yataozea stooni,wafanyabiashara wamekosa vitalu vya gesi,kampuni ya mkono and advocates imekatiwa mirija,Lowasa ameahidi vyeo kwa wajumbe wa PAC,mahela ya mengi kumbuka kumzomea tu prof 3mil,ukichangia na kushinikiza atoke mil 20,mkono kuwakodishia ndege Zitto na wenzake kwenda kwenye harus ya kafulila,Zitto kupewa bil 1.5 na kupewa jukumu la kutafuta wabunge wenye ushawishi kushinikiza prof na katibu wake waondoke,

leta ushahidi acha porojo una kipaji cha umbea mtafute mzee Yusufu ukaimbe taarabu huenda ukatoka kimaisha huku kutetea wafu wenzako ccm unapoteza muda wako.
 
..Baadaye Prof. Muhongo alijieleza mbele ya spika Makinda na kamati ya maadili ya bunge ambapo alikiri mwenyewe kuwa alifanya hivyo ili bajeti ya wizara yake ipite kirahisi eti kwamba hakuitaji usumbufu kutoka kwa aliowaita kuwa wajuaji....... Makinda akajilaumu sana kwa kuivunja kamati ya Zitto! Muhongo akasamehewa yakafanywa siri, yakapita

Japo simtetei Muhongo hata kidogo, sitaki kuamini kuwa hii kitu ni kweli, au umefabricate tu mkuu!
 
Mods naomba huu uzi msiuhamishe, msiuchanganye na mwingine. Acha tuujadili ukweli!

Kumekuwa na jitihada za makusudi za kumtetea waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo eti kwa kuwa ni mtendaji bora basi asiwajibishwe kutokana na wizi wa mali ya umma. Huu ni ukosefu wa maarifa na kutokutumia akili kuliko kithiri!

Kwanza kabisa Muhongo Sospeter siyo mtendaji mzuri.

Pili ni mtu wa kujiamulia mambo bila kufuata taratibu na sheria kitu ambacho kimeligharimu taifa kwa kiasi kikubwa!

Je, mnaomtetea Muhongo mna habari kuwa ndiye aliyechangia 13% ya deni la taifa tunaloliona sasa?

Je mnajua kuwa Prof. Muhongo aliwajibishwa na kamati ya maadili ya bunge kwa kuwa aliituhumu POAC iliyokuwa ikiongozwa naZitto Kabwe kabla ya kuvunjwa ambapo alisema kuwa POAC imepewa hongo na Reginald Mengi ili iikwamishe bajeti ya wizara yake kwa mwaka
2014/15?

Baadaye Prof. Muhongo alijieleza mbele ya spika Makinda na kamati ya maadili ya bunge ambapo alikiri mwenyewe kuwa alifanya hivyo ili bajeti ya wizara yake ipite kirahisi eti kwamba hakuitaji usumbufu kutoka kwa aliowaita kuwa wajuaji na hakukuwa na tuhuma zozote za Zitto na kamati yake kupewa rushwa na Reginald Mengi. Makinda akajilaumu sana kwa kuivunja kamati ya Zitto! Muhongo akasamehewa yakafanywa siri, yakapita!

Kama hamjui basi nawaeleza kuwa Prof. Muhongo amekuwa akituhumiwa mara kwa mara ndani ya kikao cha baraza la mawaziri kuwa ni mtu anayelitia hasara taifa kutokana na maamuzi yake ya hovyo na kutokifuata sheria na taratibu za mikataba na manunizi ya umma.


Hafuati sheria za manunuzi ya umma, ni mtu asiyepokea ushauri na amekuwa akilazimisha serikali nzima kusahau mambo mengine kwa ajili ya wizara yake!

Prof. Muhongo amekuwa akitoa takwimu za uongo kwa makusudi mbele ya bunge..Marhalan deni la Tanesco limekuwa likizidi mara mbili kila mwaka na sasa Tanesco
inadaiwa bilioni 100 za Kitanzania ambapo yeye aliingia wizarani Tanesco ikiwa na deni la bilioni 10 pekee hilo analifanya kuwa siri na kutoa takwimu za uongo eti fedha za ESCROW zilibadilishwa kuwa deni la Tanesco kwa IPTL! Utendaji wa huyu mtu uko wapi?

IPTL imekuwa ikizidishiwa malipo kila siku tangu aingie madarakani hilo kaamua kulifumbia macho kwa makusudi kwa kuwa tayari alishakiuka taratibu za mauzo ya IPTL kwa PAP!

Wapo wanaosema kuwa amefanikisha kupeleka umeme vijijini kupitia REA, fine. Je wanajua ni kiasi gani Prof. Muhongo ameidanganya serikali kwa takwimu za uongo na kupikwa ili serikali ihamishie rasilimali zake nyingi REA? REA imepewa kiasi kikubwa sana cha fedha kuliko ambavyo inazalisha! Hilo wanalifahamu?

Ukweli ni kuwa Muhongo amekuwa akitoa taarifa za uongo kwa serikali ili kufanikisha mpango wake wa kuchota fedha, ametoa takwimu na taarifa za uongo bungeni toka alipoteuliwa kuwa waziri! Spika wa bunge kila bunge la bajeti linapoisha amekuwa akimpeleka Prof. Muhongo mbele ya kamati ya maadili ya bunge kutokana na taarifa za uongo ila hilo limekuwa likifanywa siri!

Hii nchi imejaa wajinga na prof Muhongo analijua hilo ndio maana anawageuza wadanganyika kama samaki kwenye kikaango.
 
Kwani hata Kagasheki si alikua mtu safi na mtendaji mzuri sana pale wizara ya maliasili na utalii na hakufanya kosa lolote lakini ilibidi a step down kwa makosa ya watendaji wengine. Wala hakushika bunduki wakati wa oparesheni tokomeza lakini kiongozi sifa yake kubwa ni kuhakikisha idara au wizara yake iko vizuri katika kutimiza wajibu wake. Muhongo si mbaya na inawezekana alikua na nina nzuri tu katika hili lakini kwa sababu wananchi wamekosa imani na wizara yake hana budi kuachia ngazi japo ana sifa zote. tusiwe na na double standard kwenye kuwajibishana
 
Japo simtetei Muhongo hata kidogo, sitaki kuamini kuwa hii kitu ni kweli, au umefabricate tu mkuu!

Una myopia kwa Professor wa Uongo. Hivi hujui kama huyu professor alishawatuhumu wabunge wakaundiwa tume kisha ikabainika kuwa alisema uongo?.
 
Mods naomba huu uzi msiuhamishe, msiuchanganye na mwingine. Acha tuujadili ukweli!

Kumekuwa na jitihada za makusudi za kumtetea waziri wa nishati na madini Prof. Sospeter Muhongo eti kwa kuwa ni mtendaji bora basi asiwajibishwe kutokana na wizi wa mali ya umma. Huu ni ukosefu wa maarifa na kutokutumia akili kuliko kithiri!

Kwanza kabisa Muhongo Sospeter siyo mtendaji mzuri.

Pili ni mtu wa kujiamulia mambo bila kufuata taratibu na sheria kitu ambacho kimeligharimu taifa kwa kiasi kikubwa!

Je, mnaomtetea Muhongo mna habari kuwa ndiye aliyechangia 13% ya deni la taifa tunaloliona sasa?

Je mnajua kuwa Prof. Muhongo aliwajibishwa na kamati ya maadili ya bunge kwa kuwa aliituhumu POAC iliyokuwa ikiongozwa naZitto Kabwe kabla ya kuvunjwa ambapo alisema kuwa POAC imepewa hongo na Reginald Mengi ili iikwamishe bajeti ya wizara yake kwa mwaka
2014/15?

Baadaye Prof. Muhongo alijieleza mbele ya spika Makinda na kamati ya maadili ya bunge ambapo alikiri mwenyewe kuwa alifanya hivyo ili bajeti ya wizara yake ipite kirahisi eti kwamba hakuitaji usumbufu kutoka kwa aliowaita kuwa wajuaji na hakukuwa na tuhuma zozote za Zitto na kamati yake kupewa rushwa na Reginald Mengi. Makinda akajilaumu sana kwa kuivunja kamati ya Zitto! Muhongo akasamehewa yakafanywa siri, yakapita!

Kama hamjui basi nawaeleza kuwa Prof. Muhongo amekuwa akituhumiwa mara kwa mara ndani ya kikao cha baraza la mawaziri kuwa ni mtu anayelitia hasara taifa kutokana na maamuzi yake ya hovyo na kutokifuata sheria na taratibu za mikataba na manunizi ya umma.


Hafuati sheria za manunuzi ya umma, ni mtu asiyepokea ushauri na amekuwa akilazimisha serikali nzima kusahau mambo mengine kwa ajili ya wizara yake!

Prof. Muhongo amekuwa akitoa takwimu za uongo kwa makusudi mbele ya bunge..Marhalan deni la Tanesco limekuwa likizidi mara mbili kila mwaka na sasa Tanesco
inadaiwa bilioni 100 za Kitanzania ambapo yeye aliingia wizarani Tanesco ikiwa na deni la bilioni 10 pekee hilo analifanya kuwa siri na kutoa takwimu za uongo eti fedha za ESCROW zilibadilishwa kuwa deni la Tanesco kwa IPTL! Utendaji wa huyu mtu uko wapi?

IPTL imekuwa ikizidishiwa malipo kila siku tangu aingie madarakani hilo kaamua kulifumbia macho kwa makusudi kwa kuwa tayari alishakiuka taratibu za mauzo ya IPTL kwa PAP!

Wapo wanaosema kuwa amefanikisha kupeleka umeme vijijini kupitia REA, fine. Je wanajua ni kiasi gani Prof. Muhongo ameidanganya serikali kwa takwimu za uongo na kupikwa ili serikali ihamishie rasilimali zake nyingi REA? REA imepewa kiasi kikubwa sana cha fedha kuliko ambavyo inazalisha! Hilo wanalifahamu?

Ukweli ni kuwa Muhongo amekuwa akitoa taarifa za uongo kwa serikali ili kufanikisha mpango wake wa kuchota fedha, ametoa takwimu na taarifa za uongo bungeni toka alipoteuliwa kuwa waziri! Spika wa bunge kila bunge la bajeti linapoisha amekuwa akimpeleka Prof. Muhongo mbele ya kamati ya maadili ya bunge kutokana na taarifa za uongo ila hilo limekuwa likifanywa siri!

Mtahangaika sana mwaka huu. Mliuaminisha umma kuwa Prof Muhongo amekwapua fedha za escrow lakini report ya CAG haijaonesha kuwa alilipwa fedha hizo. Watanzania tuweni na tabia ya kusema na kutenda haki.
 
Back
Top Bottom