Wanaomtetea Prof. Muhongo, jibuni maswali haya

Wanaomtetea Prof. Muhongo, jibuni maswali haya

Kumbe wale wanaodaiwa kuhongwa na Muongo wameshaanza kazi,huwezi kupingana na CAG,PCCB,PAC na Bunge.
Kwani huyu Mheshimiwa si ang'atuke tuu kinachomfanya ang'ang'anie ni nini?Kama yeye ni muadilifu atoke tuu kwani kuna nini anachong'ang'ania.Walikuwepo wangapi bhana na wameng'atuka.Hii ndio shida ya kula hela za watanzania,ameshanogewa sasa anaona mipango yake itaharibika.Nenda tu Mheshimiwa tunajua umefanya mazuri,lakini kwa hili doa huwezi kutakata hata kwa Jiki.Kapumzike.

Kama kweli haya yanatoka moyoni mwako, basi ungemng'ang'ania Chenge ambaye kila "deal" yumo!!!!!!!!!!
 
Nipashe tumekuelewa sasa tutafutie mfanyibiashara aliyekopa bank ya NBC akachoma ushahidi na mabilioni ya hela yakapotea mkimpatahuyo mtu na kumtaja hadharani nami nitachangia kuhusu muhongo
 
Biashara kwa mtu mwenye akili maana yake faida. hakuna faida hiyo siyo biashara niupuuzi.

Business means profit, any loss has no justification to purify the distortion.

Unawezaje kumsifu nakumpigia debe mtu anayetengeneza hasara? Nimpumbavu tu ambaye hafaham maana ya biashara.

-Unapoteza 200, unakopa 400 (-200) (kumbuka mkopo ni deni pia ie (-400)

-next unapoteza 300 unakopa 600 (-300) mkopo ni deni sio zako (-600) from 400 umebakiza ( 100)

1. ulikuwa na 200 ukapoteza zote ukakopa 400 maana yake unadeni -200 -400 = -600 deni

2. Unapoteza 300 kutoka mkopo umebaki na 100 maana yake kutoka hapo juu -600 100 -600 = -1100 Deni

Huu ndiyo ushenzi anaoufanya muhongo kwakukopa mabilion ya shilingi na kutengeneza hasara ya mabilion akiwekeza ndululu. unadeni la 1100 halafu umewekeza 100 tu!!!!!!grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr.

Nimshenzi tu na mpumbavu asiyefahamu maana ya biashara yaani Faida nasio madeni wala hasara na hakunasababu

yoyote ya kusapoti hasara kwenye biashara duniani pote. (ndio maana ya kujioditi mara kwa mara kuzuia hasara

itakayopelekea shirika au kampuni kufilisika
)

Ndugu, mkopo sio deni, ila unaweza ukaufanya uwe deni, but definetly mkopo sio deni hata siku moja
 
Ndugu, mkopo sio deni, ila unaweza ukaufanya uwe deni, but definetly mkopo sio deni hata siku moja

Duh! hii kali professional za watu mnajichezea.

Kwenye vitabu mkopo unakuwa treated as current liability sasa sijui ni deni au nini.
-----------------
Liability
An obligation that legally binds an individual or company to settle a debt.

When one is liable for a debt, they are responsible for paying the debt or settling a wrongful act they may have committed.

cc. adolay
 
Last edited by a moderator:
Ndugu, mkopo sio deni, ila unaweza ukaufanya uwe deni, but definetly mkopo sio deni hata siku moja


mkuu chochote unachopewa au kuomba kwa makubaliano ya kurejesha hilo ni deni

-Mikopo, nimadeni tena yanamasharti mbalimbali

Unaweza kuwa mkopo wa bila riba lakini urudishe kwa kipindi/muda maalum

unaweza kuwa mkopo wenye riba

Simple interest walau kunaunafuu ikiwa factor/rate ni ndogo otherwise majanga

compound interest majanga zaidi

Sielewi unaposema mkopo sio deni unamaagani hebu fafanua nasisi tupate darsa tukakope huko mahera ya bure tufaidike.
 
Shida kwa baadhi ya wanaCCM ni kutetea Serikali (au mwanaccm) hata kama kosa ni la wazi na linaloweza hatarisha maisha ya malaki, wao hawajali, desturi hii ni ya kijuha sana.
 
Hivi jaman naomba kuuliza kosa la Waziri wa nishat na madini Prof Muhongo ni lipi! embu tuweke ushabiki pembeni tuulizane juu ya hili sipo kumtetea nipo ktk kutaka kujua kosa lake kubwa lipi! Na jee km ndio kosa lake hilo ktk hili la Escrow basi ata yule aliyesaini kutoka kwa zile hela pamoja na waziri wa fedha nao wahusike
 
Hivi jaman naomba kuuliza kosa la Waziri wa nishat na madini Prof Muhongo ni lipi! embu tuweke ushabiki pembeni tuulizane juu ya hili sipo kumtetea nipo ktk kutaka kujua kosa lake kubwa lipi! Na jee km ndio kosa lake hilo ktk hili la Escrow basi ata yule aliyesaini kutoka kwa zile hela pamoja na waziri wa fedha nao wahusike

Kufanya udalali/ukuwadi kwenye ofisi ya UMAA!!!!
 
Kosa lake ni kuwanyang'anya madalali vitalu vya madini na gesi
 
Kosa lake ni kuwakabidhi wewe pamoja na jamaa zako Laptop ili kuja kumtetea hapa jukwaani.
 
Ukichaa ni kurudia jambo over and over again ukitegemea matokeo tofauti ambayo hayatokei!!! Punguza uchizi, jitambue kuwa kosa la Muhongo ni Kiburi, Udalali uliosababisha wizi kwenye ESCROW a/c na Uongo uliopitiliza wa kulidanganya Bunge ....


Hivi jaman naomba kuuliza kosa la Waziri wa nishat na madini Prof Muhongo ni lipi! embu tuweke ushabiki pembeni tuulizane juu ya hili sipo kumtetea nipo ktk kutaka kujua kosa lake kubwa lipi! Na jee km ndio kosa lake hilo ktk hili la Escrow basi ata yule aliyesaini kutoka kwa zile hela pamoja na waziri wa fedha nao wahusike
 
Hivi jaman naomba kuuliza kosa la Waziri wa nishat na madini Prof Muhongo ni lipi! embu tuweke ushabiki pembeni tuulizane juu ya hili sipo kumtetea nipo ktk kutaka kujua kosa lake kubwa lipi! Na jee km ndio kosa lake hilo ktk hili la Escrow basi ata yule aliyesaini kutoka kwa zile hela pamoja na waziri wa fedha nao wahusike
Duuh yaani mpaka sas haujajua kosa lake. Basi ngoja nikwambie makosa makubwa ya huyu Prof:
1) Kutompendelea Mengi ili apate vitalu vya gesi
2) Kumuondoa Mkono kwenye uwakili waTanesco ili asiendelee kulitia taifa hasara
3) Kusimamia majukumu ya wizara kwa uhadilifu na kufanikisha utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini
4) Kusema ukweli hata kama unawaumiza watu wengine
Kwa ufupi hayo ndo makosa makubwa kabisa ninayoyafahamu na ambayo hata kamati ya zito iliyaona
 
Hata mimi sioni kosa lake wanahaha sana kumchafua ila hawataweza.
 
Ukichaa ni kurudia jambo over and over again ukitegemea matokeo tofauti ambayo hayatokei!!! Punguza uchizi, jitambue kuwa kosa la Muhongo ni Kiburi, Udalali uliosababisha wizi kwenye ESCROW a/c na Uongo uliopitiliza wa kulidanganya Bunge ....

Hahaha mkuu usitokwe na Povu hili ni swali tu nimeuliza wala haustahili kutoa matusi..hata yesu wakati anapelekwa kwa Pilato,kuna watu waliona Yesu alikuwa na makosa ya kuadhibiwa
 
Mkuu nenda kamwambie mnowe pamoja na pesa zake wengine hawahongeki mwambie tumechoka kuibiwa na mafisadi kama yeye alizoiba inatosha,

Lakini pia mwambie Nipashe pekee haitoshi atumie magazeti yake yote pamoja na tv japo nao zitagota tu.

Thread kama hii ukiona inachangiwa na mtu kam Simiyu Yetu ujue kilichomo ni pumba tupu.
 
Duuh yaani mpaka sas haujajua kosa lake. Basi ngoja nikwambie makosa makubwa ya huyu Prof:
1) Kutompendelea Mengi ili apate vitalu vya gesi
2) Kumuondoa Mkono kwenye uwakili waTanesco ili asiendelee kulitia taifa hasara
3) Kusimamia majukumu ya wizara kwa uhadilifu na kufanikisha utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini
4) Kusema ukweli hata kama unawaumiza watu wengine
Kwa ufupi hayo ndo makosa makubwa kabisa ninayoyafahamu na ambayo hata kamati ya zito iliyaona

Hana makosa kabisa huyu malaika wa mola....
Ana mazuri mengi tu baadhi ya hayo mazuri ni:
1. Kusema fedha za escrow SI ZA UMMA kwani TANESCO wana madeni makubwa wanayodaiwa na IPTL.
2. Kusema ya kuwa Watanzania hawana uwezo wa kuwekeza wakati hata hao wawekezaji wenyewe wanaopewa vitalu wanakopa kwenye Bank zao.
3. Ni profesa mpole sana na mcheshi sana mwenye maneno ya upole sijawahi kuona hasa kwa wana MTWARA
4.Ni Professor wa pekee mwenye uwezo wa kutoa facts and figures ambazo hazikuwa ferified popote zinazopinga report ya CAG.
5.Ni kiongozi ambaye hana Kinyongo, anatafuta suluhu na wadau wake na hana kinyongo na Mengi na Mkono. Ni kiongozi wa mfano wa kuigwa. upendo wake kwa mahasimu wake umezidi kipimo.
6. Hajawahi kusema uongo kabisa. Nawahakikishia alishawahidi waTZ hakutakuwa na Mgao wa Umeme na toka atoe tamko hilo HAKUJAWAHI KUWA NA MGAO WA UMEME. Wote tu mashahidi umeme haukatiki na asilimia 99 ya nchi ina umeme masaa 24 na hasa zile siku za muwasilishwa ripoti ya Esrow aliwapa maagizo mameneja wote wa TANESCO umeme usikatike na HAUKUKATIKA KABISA. Huyu Profesor sio MUONGO KABISA ni MKWELI TUUU.
8. Hajalewa madaraka, hang'ang'anii madaraka na ni mtu wa watu. Ni chaguo la thithiem
9. Ni professor ambaye atachaguliwa kwa kura za kishindo endapo atapitishwa kuwa Mgombea wa Urais na kuna motisha ya Laptops kwa wote!
10.........................................

Viva Le proffeseri.......
 
Back
Top Bottom