Wanandoa: Upangaji wa nguo chumbani

Wanandoa: Upangaji wa nguo chumbani

Ha ha ha nimecheka sana yaani we umeona nguo tu bado viatu na handbags mpaka unatamani saa nyingine ugaweeee vyote wakija ndugu unagawa then week hiyohiyo unanunua handbags nne, viatu pea tano nguo ndio usiseme ngoma inarudi palepale ha ha yaani nimecheka sana aisee
 
Aisee kuna issue ya sox,utatafuta unapata rangi tofauti...kwa hali hii bora nijipangie mwenyewe kuokoa muda wa kudamka usubuhi...

Mkuu issue ya soksi kama una imani za ajabu unaweza ukasingizia mapepo aisee maana zingine zinapotea na hasa ukiwa na pair za kutosha yaani ukitaka kuvaa unakutana na soksi za baba mmoja mama mbalimbali na wakati mwingine hata kama utasema ufanye inventory ya soksi zako unakuta zingine hazionekani, wakati mwingine inabidi muwe wabunifu wakati wa kuzifua na kuzianika yaani zinaanikwa kwa pair na hata zikiwekwa sehemu zinawekwa kwa style ya pair na kwa unyoofu wake na sio kuziweka furushi
 
hakuna hata haja ya chumba, kama kapange inakuaje?? Anunue la milango6 wajinafasi wote

Chumba cha kupanga aweke kabati la milango 6? Wenyewe wanavyojenga vidogo ukiweka kitanda cha 6*6 hata pa kugeukia ni shida.
 
wanawake wanashona nguo na kununua kila kukiwapo na sherehe au kijishughuli pia wengi wao wana tabia kila mwezi wananunua nguo mpya mara mbili au moja ndio mana makabati yana jaa co kama sisi.
 
Heeee makubwa!!! Ukitaka Adha hii uiepuke muachie mkeo akupangie na yeye ndo akutayarishie kila kitu,vitu kama soksi atawajibika mwenyewe,vile atakavyokuwa anahangaika kuvipata akili zitamkaa sawa kupangilia vyema. Pia mnaweza kuweka utaratibu kila mwisho wa mwaka mnagawa nguo,kanisani Mara nyingi huwa wanatangaza wale wenye nguo walete wanazipeleka huko vijijini kuwapa wahitaji.
 
hivi hilo kabati unaloongelea ni la aina gani..kwa mfano kama una kijichumba cha kuweka nguo na kimegawanywa makabati ya ukutani mawili..lake na lako...huo muingilianao unatokea wapi?....kutatua tatizo hili ni kujenga chumba maalumu kwa ajili ya kutunzia nguo.

wenzetu wazungu walishaliona hilo na kutafuta suluhisho la kudumu....tuwaige kwa haya machache mazuri.

Aisee.. yaani mimi nyumba yangu ina plan ya dressing room kabisaa.. kujaza makorokoro chumbani bhaassiii...
 
Yaani bedroom, mke hata awe mstaarab kiasi gani kikawaida huwa anameza nafasi ya uhifadhi wa nguo.

Kama ni kabati atajaza nguo zake mpaka wewe uhamie masandukuni na huko usipokuwa makini utakuta kaanza kuweka nguo zake inabidi uhamie kwenye mabegi.

Pia huko atajaza na kwa sababu wanaume hatutaki usumbufu wa kutafuta na kupekua nguo utampisha utafute namna ya kutundika nako huko atakufata utakosa nafasi ya kutundika.

Wakati huo chumba kitakuwa kama store, nyie wamama nyiee.

Vichwa vyenu made in wapiii?

Rahisi tu ukijenga nyumba master bedroom iwe na dressing room weka makabati ya maana yenye drooo mnagawana pande na drooo but ni very easy kutunza nguo labatini na kuzipanga bila kuvuruga wakati wa kutoa. Tatizo mmeoa wanawake wasiojua utaratibu na ninyi wenyewe ni mabosi hapo lazima chumba kiwe store
 
Yaani bedroom, mke hata awe mstaarab kiasi gani kikawaida huwa anameza nafasi ya uhifadhi wa nguo.

Kama ni kabati atajaza nguo zake mpaka wewe uhamie masandukuni na huko usipokuwa makini utakuta kaanza kuweka nguo zake inabidi uhamie kwenye mabegi.

Pia huko atajaza na kwa sababu wanaume hatutaki usumbufu wa kutafuta na kupekua nguo utampisha utafute namna ya kutundika nako huko atakufata utakosa nafasi ya kutundika.

Wakati huo chumba kitakuwa kama store, nyie wamama nyiee.

Vichwa vyenu made in wapiii?


hahahahahha vichwa vyetu made in tanzania,in an africa culture way..lol,aisee nimecheka sana,ila hata nyie wanaume mnamatatizo kwenye hii sector,mkianza kutafuta nguo zenu lazima mvurugue alafu mnaziangusha chini mnaacha ivyoivyo hapo unakuta jana tuu nimepanga kabati lako,umezivurugua kama vile ulikuwa unaogelea kabatini.
 
Nimesahau kabisa zoezi la kupanga nguo maana sina sehemu maalumu ya kuziweka kila siku nahama kama mkimbizi nimejiamulia kuvuruga tu utaratibu ila tatizo akisafiri natamani kupaa maana bila kumpigia simu anielekeze hakika navaa sox tofauti nimejikuta nimerudi utotoni kwa kutegemea kuambiwa kipi kiko wapi kisa ni yeye kumiliki kila sehemu haa haaa nshawahi kumuuliza "ivi tunawindana?"maana kila nikihamisha nguo zangu ananifata wakati nna vishati na suruali vichache.

Hahaaaa eti hivi tunawindana? Mbona pole
 
Dawa akizidi kukubana ni kuzivaa nguo zake tu ukijidai ulidhani ni zako, hapo atakoma tu!
 
Chumba cha kupanga aweke kabati la milango 6? Wenyewe wanavyojenga vidogo ukiweka kitanda cha 6*6 hata pa kugeukia ni shida.

basi waweke na uvunguni au wapange chumba cha nguo
 
Aisee kuna issue ya sox,utatafuta unapata rangi tofauti...kwa hali hii bora nijipangie mwenyewe kuokoa muda wa kudamka usubuhi...

Pole mkuu.
Kwani wife si ndio anakunja/ ananyoosha nguo baada ya kuanua.
Kawaida anapoanua soksi kabla ya kupeleka kabatini anatakiwa avalishe zakufanana (zinakaa kipea, moja ndani ya nyingine) so wakati wa kuvaa unabeba soksi moja yenzie inakua ndani yake.
 
Back
Top Bottom