Lula wa Ndali Mwananzela
WANANCHI wa Zanzibar wanadhulumiwa na wanadhulimiwa kweli kweli. Wanalazimishwa kuchagua kati ya vitu viwili na ni vitu viwili peke yake. Matokeo yake wananchi wa Zanzibar hawana uchaguzi wa kweli na hata kunyimwa uchaguzi bora. Katika elimu ya mantiki (logic) kuna kitu kinaitwa ulaghai wa hoja (fallacies). Ulaghai wa hoja ni namna ya kauli au hoja ambayo inajengwa kwa makosa na wakati mwingine kwa makusudi ili kumlaghai msikilizaji. Ulaghai huo hufanywa kwa kutegemea kwamba wasikilizaji hawawezi kugundua kuwa wanalaghaiwa.
Njia mojawapo ya kufanya ulaghai wa hoja ni kuwashambulia watu badala ya hoja. Kwa mfano, mtu anakuja nyumbani kwako na kukuambia kuwa nyumba yako ina ufa mkubwa wewe badala ya kuangalia kama kweli kuna ufa (kuiangalia hoja yake) unaanza kumshambulia. Wewe ni mshamba mkubwa nyumba yangu iwe na ufa mimi? Wewe una kichaa nini? ni namna mojawapo ya mashambulizi ambayo kitaalamu yanaitwa ad hominem (kumshambulia mtu). Sasa mtu asiyejua kufikiri vizuri anaweza kurukia tu juu juu kweli mshamba huyo, kwanza katumwa na wote wawili wanaweza kudhania wanaishughulikia hoja ya nyufa. Hoja ya nyufa inaweza tu kupanguliwa kwa kuangalia pale ambapo yule mtu alionesha na kudai kuwa pana nyufa. Kama kweli pana nyufa hata yule mtu angekuwa kichaa, mshamba, mwizi, au mhuni mmoja ukweli utabakia kuwa nyumba ina nyufa!
Njia nyingine ya kuwalaghai watu kwa hoja ni ile ya kuwapa kile kinachoitwa ulaghai wa njia mbili pekee. Kwa kitaalamu hii inaitwa the fallacy of false dilemma yaani mtu anaambiwa kuwa vitu vya kuchagua ni vitu viwili tu. Mfano mzuri uko kwenye lugha yetu ya Kiswahili ambapo mtu anaweza kumwambia mwingine bwana uchaguzi unao kusuka au kunyoa. Sasa kwa haraka haraka mtu asiyefikiri anaweza kuamini kuwa anao uchaguzi wa ama kusuka au kunyoa. Mtoto anaweza kufikiria hivyo lakini mtu mzima anaweza akasema mbona kuna kuchana?, mbona kuna kupunguza kidogo tu?. Kumbe uamuzi wa kusuka au kunyoa ni njia panda ya uongo kwamba mtu anazo njia mbili tu za kuchagua.
Sasa mtu au kundi la watu linaweza kutumia nguvu kubwa sana kuwashawishi watu kuwa zipo njia mbili tu za kwenda na njia nyingine yoyote ya tatu haipo au haiwezekani. Na kama imani hii inajengwa kwa muda mrefu sana wapo watu wanaamini pasipo shaka kweli wanazo njia mbili tu. Ni sawa sawa na mahali kwenye kijiji kimoja kulikuwa na mto na watu walikuwa wanatumia mahali fulani kuvuka kwa kutumia daraja walilojijengea. Kwa muda mrefu uchaguzi ulikuwa wa aina mbili tu kwamba kuvuka kwenda upande wa pili ilikuwa ni ama kutumia mtumbwi au kuogelea.
Hadi alipokuja mtu na kuwaambia kwa nini watoto wao waliendelea kufa kwa kuogelea au mitumbwi kusombwa na maji? Kwa nini wasiamue kujenga daraja? Wale wanakijiji walianza kulalamika kuwa gharama za kujenga daraja ni kubwa sana na hawakuwa na wataalamu. Hadi yule mtu akawashawishi na kuwaonesha kuwa wakitafuta mahali ambapo upana wake si mrefu wangeweza kuangusha minazi miwili na kutoka hapo kuweka mbao na kujitengenezea daraja bila kutumia nguvu kubwa. Matokeo yake wakajipatia njia nyingine ya kwenda ngambo.
Wananchi wa Zanzibar wanalazimishwa kuchagua kati ya CCM na CUF kama njia mbili pekee kwa maisha yao ya kisiasa na utawala. Kwa miaka sasa wananchi hao wameambiwa kuwa siasa za Zanzibar zitaamuriwa na vyama hivyo viwili peke yake na kuwa ni CCM na CUF tu ndio wenye mawazo bora kuhusu Zanzibar. Na kwa bahati mbaya sana tangu kurudi kwa mfumo wa vyama vingi siasa za Zanzibar zimetawaliwa na vyama hivyo viwili kana kwamba ndivyo vyenye ubia pekee wa kuitawala Zanzibar na wapo watu Zanzibar ambao hawawezi kufikiri kabisa (hawataki na hawana uwezo) nje ya CCM au CUF. Kwa watu hawa ni ama unaunga mkono CUF au CCM! Na vijana wameuziwa hizi njia mbili pekee!
Kwa mara ya kwanza, hata hivyo, Zanzibar na hususan wananchi wa Jimbo la Uzini wanapewa nafasi ya kumchagua mgombea kutoka CHADEMA ambaye anakubalika na kuwakilisha mawazo tofauti na yale ya wana CCM na wana CUF. Ni chaguo la tatu, chaguo tofauti. Kwamba wananchi wa Uzini wanaitwa kufikiria kubadilisha kabisa siasa za Zanzibar kwa kuleta kwa mara ya kwanza chama tofauti na siasa tofauti na vile vile kutoa sauti tofauti kutoka Zanzibar. CHADEMA wameamua kumpitisha Mwalimu Ali Mbarouk Mshimba kuwa mgombea wa jimbo hilo. Wengine wanasema haiwezekani kwa sababu Zanzibar ni CCM au CUF lakini yumkini Zanzibar ikawa na nafasi kwa chama kingine!
Sasa kwa kuangalia kwa haraka ni wazi kuwa Mshimba anaweza kuonekana hana nafasi kwa sababu eneo hilo ni ngome ya CCM. Lakini wananchi wa Uzini watamchagua yeyote alimradi anatoka CCM? Ni kweli wananchi wa Uzini hawawezi kuangalia njia ya tatu au chaguo la tatu kwa sababu wao na wazee wao waliapa kuchagua CCM bila kujali nani anasimamishwa? Je, wananchi wa Uzini watachagua CCM hata kama sera zake zimepitwa na wakati? Je, Mshimba anakuja na CHADEMA ana anakuja na sera gani kuhusu Zanzibar?
Hatuna budi kuangalia Ilani ya Uchaguzi ya CHADEMA ya mwaka 2010 ambayo inatupa mwanga kidogo wa mawazo ya CHADEMA kuhusu wananchi wa Zanzibar. Ilani ya CHADEMA katika vipengele maalumu inazungumzia Zanzibar. Labda niweke hapa yale ambayo Ilani hiyo inadokeza ili wananchi wa Zanzibar wajue kuwa wakichagua mjumbe wa Baraza la Wawakilishi au mbunge kutoka CHADEMA wanachagua nini na atapigania nini.
Serikali ya CHADEMA ina mpango madhubuti kabisa wa kuimarisha Muungano na kuhakikisha kuwa kero zote za Muungano zinaondolewa katika mwaka wa kwanza na kuachana na utaratibu wa kimazingaombwe unaofanywa na serikali ya CCM na kutishia Muungano wetu. Serikali ya CHADEMA itachukua hatua zifuatazo katika kuiwekea mazingira mazuri kwa maendeleo na katika kuimarisha Muungano:
Suala la mafuta litaachwa mikononi mwa Serikali ya Zanzibar hasa tukizingatia kuwa visiwa hivi vina raslimali ndogo sana za kiuchumi. Masuala ya raslimali nyingine yatajadiliwa ili kuhakikisha kuwa Zanzibar inanufaika na raslimali za Tanzania na vile vile inatoa mchango wake sahihi katika uchumi wa taifa.
Serikali ya CHADEMA itaitisha mkutano maalum wa pamoja wa Baraza la Wawakilishi na Bunge la Muungano na wadau wengine ili hatimaye kukaa chini kama ndugu wamoja na kujadili masuala yenye matatizo yanayohusu Muungano. Kutakuwa na kikao cha Pamoja cha Uongozi wa Taifa mara mbili kwa mwaka.
Serikali ya CHADEMA itahakikisha kuwa vikwazo mbalimbali ambavyo vinaonekana kutatiza ufanyaji wa biashara na uwekezaji katika visiwa hivyo vinaondolewa.
11.2 Unguja
Kwa vile Unguja ni eneo la kihistoria na historia yake imefungamana kabisa na historia ya Tanzania bara na pwani ya mwambao juhudi za wazi zitafanyika ili kulinda tunu hiyo ya kihistoria. Hii ni pamoja na:
Kufanya ukarabati wa majengo na maeneo ya kihistoria yaliyoko Unguja ili kuhakikisha yanaingizwa na kutunzwa katika mfumo wa kisasa ili yaendelee kuwa ni urithi kwa vizazi vijavyo.
Kwa kushirikiana na serikali ya Zanzibar, tutatenga eneo jipya kwa ajili ya ujenzi wa Jiji la Kisasa la Zanzibar (Zanzibar City) kwenye eneo ambalo litakubaliwa na Serikali ya Zanzibar ili hatimaye kujenga jiji la kisasa visiwani humo ambalo litakuwa ni kitovu cha utalii wa maeneo ya kisasa na yale ya kihistoria.
11.3 Pemba
Mji wa Pemba ni mji ambao bado haujaingizwa vizuri kabisa katika uchumi wa nchi na umeendelea kubakia mahali penye kuahidi mafanikio bila kuyatoa. Chini ya Serikali ya CHADEMA Pemba itatengwa maalumu kuwa kitovu cha biashara ya mambo ya fedha (Financial Centre) ili kushindana na maeneo kama ya UAE, Saudi Arabia, Qatar n.k Lengo letu ni kuhakikisha kuwa Pemba inakuwa ni makao makuu ya taasisi mbalimbali za kifedha na makampuni mbalimbali. Ili kutimiza adhma hii
Kuanzia Bajeti ya 2011/2012 upembuzi yakinifu utafanywa ili kuona ni jinsi gani mkongo wa mawasiliano ambao unapita katika bahari ya Hindi unaweza kuchepushwa kuelekea Pemba na hivyo kuipatia Pemba njia za fibre optics na kurahisisha mawasiliano.
Kwa kushirikiana na Serikali ya Zanzibar utawekwa mfumo maalum wa kodi mbalimbali kwa ajili ya Pemba kuwa kivutio cha uwekezaji wa taasisi za fedha. Lengo ni kufanya Pemba kuwa ni eneo la unafuu wa kodi (Tax Haven) kwa makampuni ya ndani na ya kimataifa. Ili kuhakikisha hili linafanikiwa tutahakikisha kunakuwepo na umeme wa kudumu, huduma safi ya maji, tiba na udhibiti wa kisasa ili kuhakikisha kuwa Pemba haitotumiwa na wahalifu wa kimataifa katika masuala ya kodi.
Kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Serikali ya Muungano itahakikisha kuwa miji ya Chake Chake na Wete inapatiwa ujenzi wa majengo ya kisasa pamoja na miundo mbinu ya kisasa na huduma za kuaminika za usafiri kati yake ya Tanga.
Ni wazi kwamba, kwa vile Serikali hiyo ya CHADEMA haijaundwa basi wale wagombea na wabunge wa CHADEMA wanaendelea kusimamia na kupigania yale. Je, haya ni bora kulinganisha na yale yanayopendekezwa na CCM na CUF? Nina uhakika wapo watu Zanzibar ambao hawakubaliani na siasa za CCM wala zile za CUF na kwa muda mrefu wamekuwa wakisubiri nafasi ya kuchagua kitu kingine.
Lakini, hakuna mtu atakayekuja kutoka akhera kuwaambia nani wamchague; hatakuja mtu kutoka peponi kuwaambia waangalie chaguo jingine. Wao wenyewe kama binadamu wenye uwezo wa kufikiri wanatakiwa kuitikia wito wa kihistoria wa kuangalia kama kuendelea na watu wale wale, wenye sera zile zile na kutoka chama kile kile kumekuwa na manufaa kwao. Wafanye ambacho Watanzania wengine wamekifanya hata sehemu ambazo ziliaminika ni ngome za CCM; waliikataa.
Wananchi wa Uzini wakituma ujumbe huo watakuwa wamewapa wananchi wa Zanzibar kile ambacho Mapinduzi yalipigania yaani uhuru wa kuamua na kuwa na utu bila kulazimishwa kufanya siasa ambazo hazina manufaa. Hili nina uhakika litafanywa na wazee na vijana na kuwa wataamua kuendelea kuambia kuwa njia pekee ni hizo mbili walizozizoea kwa karibu miaka hamsini sasa au kuna njia ya tatu bora. Nani atawaongoza? Je, itakuwa ni sawa na kusaliti? Je, kuchagua chama kingine nje ya CCM na CUF ni kutokuwa mwaminifu kwa Zanzibar? Well, kila kitu kina mwanzo wake, na tusipoangalia tunaweza kuwa mashahidi wa kitu kipya kabisa Zanzibar!
Zanzibar imepewa chaguo la tatu!
SOURCE: Raia Mwema
WANANCHI wa Zanzibar wanadhulumiwa na wanadhulimiwa kweli kweli. Wanalazimishwa kuchagua kati ya vitu viwili na ni vitu viwili peke yake. Matokeo yake wananchi wa Zanzibar hawana uchaguzi wa kweli na hata kunyimwa uchaguzi bora. Katika elimu ya mantiki (logic) kuna kitu kinaitwa ulaghai wa hoja (fallacies). Ulaghai wa hoja ni namna ya kauli au hoja ambayo inajengwa kwa makosa na wakati mwingine kwa makusudi ili kumlaghai msikilizaji. Ulaghai huo hufanywa kwa kutegemea kwamba wasikilizaji hawawezi kugundua kuwa wanalaghaiwa.
Njia mojawapo ya kufanya ulaghai wa hoja ni kuwashambulia watu badala ya hoja. Kwa mfano, mtu anakuja nyumbani kwako na kukuambia kuwa nyumba yako ina ufa mkubwa wewe badala ya kuangalia kama kweli kuna ufa (kuiangalia hoja yake) unaanza kumshambulia. Wewe ni mshamba mkubwa nyumba yangu iwe na ufa mimi? Wewe una kichaa nini? ni namna mojawapo ya mashambulizi ambayo kitaalamu yanaitwa ad hominem (kumshambulia mtu). Sasa mtu asiyejua kufikiri vizuri anaweza kurukia tu juu juu kweli mshamba huyo, kwanza katumwa na wote wawili wanaweza kudhania wanaishughulikia hoja ya nyufa. Hoja ya nyufa inaweza tu kupanguliwa kwa kuangalia pale ambapo yule mtu alionesha na kudai kuwa pana nyufa. Kama kweli pana nyufa hata yule mtu angekuwa kichaa, mshamba, mwizi, au mhuni mmoja ukweli utabakia kuwa nyumba ina nyufa!
Njia nyingine ya kuwalaghai watu kwa hoja ni ile ya kuwapa kile kinachoitwa ulaghai wa njia mbili pekee. Kwa kitaalamu hii inaitwa the fallacy of false dilemma yaani mtu anaambiwa kuwa vitu vya kuchagua ni vitu viwili tu. Mfano mzuri uko kwenye lugha yetu ya Kiswahili ambapo mtu anaweza kumwambia mwingine bwana uchaguzi unao kusuka au kunyoa. Sasa kwa haraka haraka mtu asiyefikiri anaweza kuamini kuwa anao uchaguzi wa ama kusuka au kunyoa. Mtoto anaweza kufikiria hivyo lakini mtu mzima anaweza akasema mbona kuna kuchana?, mbona kuna kupunguza kidogo tu?. Kumbe uamuzi wa kusuka au kunyoa ni njia panda ya uongo kwamba mtu anazo njia mbili tu za kuchagua.
Sasa mtu au kundi la watu linaweza kutumia nguvu kubwa sana kuwashawishi watu kuwa zipo njia mbili tu za kwenda na njia nyingine yoyote ya tatu haipo au haiwezekani. Na kama imani hii inajengwa kwa muda mrefu sana wapo watu wanaamini pasipo shaka kweli wanazo njia mbili tu. Ni sawa sawa na mahali kwenye kijiji kimoja kulikuwa na mto na watu walikuwa wanatumia mahali fulani kuvuka kwa kutumia daraja walilojijengea. Kwa muda mrefu uchaguzi ulikuwa wa aina mbili tu kwamba kuvuka kwenda upande wa pili ilikuwa ni ama kutumia mtumbwi au kuogelea.
Hadi alipokuja mtu na kuwaambia kwa nini watoto wao waliendelea kufa kwa kuogelea au mitumbwi kusombwa na maji? Kwa nini wasiamue kujenga daraja? Wale wanakijiji walianza kulalamika kuwa gharama za kujenga daraja ni kubwa sana na hawakuwa na wataalamu. Hadi yule mtu akawashawishi na kuwaonesha kuwa wakitafuta mahali ambapo upana wake si mrefu wangeweza kuangusha minazi miwili na kutoka hapo kuweka mbao na kujitengenezea daraja bila kutumia nguvu kubwa. Matokeo yake wakajipatia njia nyingine ya kwenda ngambo.
Wananchi wa Zanzibar wanalazimishwa kuchagua kati ya CCM na CUF kama njia mbili pekee kwa maisha yao ya kisiasa na utawala. Kwa miaka sasa wananchi hao wameambiwa kuwa siasa za Zanzibar zitaamuriwa na vyama hivyo viwili peke yake na kuwa ni CCM na CUF tu ndio wenye mawazo bora kuhusu Zanzibar. Na kwa bahati mbaya sana tangu kurudi kwa mfumo wa vyama vingi siasa za Zanzibar zimetawaliwa na vyama hivyo viwili kana kwamba ndivyo vyenye ubia pekee wa kuitawala Zanzibar na wapo watu Zanzibar ambao hawawezi kufikiri kabisa (hawataki na hawana uwezo) nje ya CCM au CUF. Kwa watu hawa ni ama unaunga mkono CUF au CCM! Na vijana wameuziwa hizi njia mbili pekee!
Kwa mara ya kwanza, hata hivyo, Zanzibar na hususan wananchi wa Jimbo la Uzini wanapewa nafasi ya kumchagua mgombea kutoka CHADEMA ambaye anakubalika na kuwakilisha mawazo tofauti na yale ya wana CCM na wana CUF. Ni chaguo la tatu, chaguo tofauti. Kwamba wananchi wa Uzini wanaitwa kufikiria kubadilisha kabisa siasa za Zanzibar kwa kuleta kwa mara ya kwanza chama tofauti na siasa tofauti na vile vile kutoa sauti tofauti kutoka Zanzibar. CHADEMA wameamua kumpitisha Mwalimu Ali Mbarouk Mshimba kuwa mgombea wa jimbo hilo. Wengine wanasema haiwezekani kwa sababu Zanzibar ni CCM au CUF lakini yumkini Zanzibar ikawa na nafasi kwa chama kingine!
Sasa kwa kuangalia kwa haraka ni wazi kuwa Mshimba anaweza kuonekana hana nafasi kwa sababu eneo hilo ni ngome ya CCM. Lakini wananchi wa Uzini watamchagua yeyote alimradi anatoka CCM? Ni kweli wananchi wa Uzini hawawezi kuangalia njia ya tatu au chaguo la tatu kwa sababu wao na wazee wao waliapa kuchagua CCM bila kujali nani anasimamishwa? Je, wananchi wa Uzini watachagua CCM hata kama sera zake zimepitwa na wakati? Je, Mshimba anakuja na CHADEMA ana anakuja na sera gani kuhusu Zanzibar?
Hatuna budi kuangalia Ilani ya Uchaguzi ya CHADEMA ya mwaka 2010 ambayo inatupa mwanga kidogo wa mawazo ya CHADEMA kuhusu wananchi wa Zanzibar. Ilani ya CHADEMA katika vipengele maalumu inazungumzia Zanzibar. Labda niweke hapa yale ambayo Ilani hiyo inadokeza ili wananchi wa Zanzibar wajue kuwa wakichagua mjumbe wa Baraza la Wawakilishi au mbunge kutoka CHADEMA wanachagua nini na atapigania nini.
Serikali ya CHADEMA ina mpango madhubuti kabisa wa kuimarisha Muungano na kuhakikisha kuwa kero zote za Muungano zinaondolewa katika mwaka wa kwanza na kuachana na utaratibu wa kimazingaombwe unaofanywa na serikali ya CCM na kutishia Muungano wetu. Serikali ya CHADEMA itachukua hatua zifuatazo katika kuiwekea mazingira mazuri kwa maendeleo na katika kuimarisha Muungano:
Suala la mafuta litaachwa mikononi mwa Serikali ya Zanzibar hasa tukizingatia kuwa visiwa hivi vina raslimali ndogo sana za kiuchumi. Masuala ya raslimali nyingine yatajadiliwa ili kuhakikisha kuwa Zanzibar inanufaika na raslimali za Tanzania na vile vile inatoa mchango wake sahihi katika uchumi wa taifa.
Serikali ya CHADEMA itaitisha mkutano maalum wa pamoja wa Baraza la Wawakilishi na Bunge la Muungano na wadau wengine ili hatimaye kukaa chini kama ndugu wamoja na kujadili masuala yenye matatizo yanayohusu Muungano. Kutakuwa na kikao cha Pamoja cha Uongozi wa Taifa mara mbili kwa mwaka.
Serikali ya CHADEMA itahakikisha kuwa vikwazo mbalimbali ambavyo vinaonekana kutatiza ufanyaji wa biashara na uwekezaji katika visiwa hivyo vinaondolewa.
11.2 Unguja
Kwa vile Unguja ni eneo la kihistoria na historia yake imefungamana kabisa na historia ya Tanzania bara na pwani ya mwambao juhudi za wazi zitafanyika ili kulinda tunu hiyo ya kihistoria. Hii ni pamoja na:
Kufanya ukarabati wa majengo na maeneo ya kihistoria yaliyoko Unguja ili kuhakikisha yanaingizwa na kutunzwa katika mfumo wa kisasa ili yaendelee kuwa ni urithi kwa vizazi vijavyo.
Kwa kushirikiana na serikali ya Zanzibar, tutatenga eneo jipya kwa ajili ya ujenzi wa Jiji la Kisasa la Zanzibar (Zanzibar City) kwenye eneo ambalo litakubaliwa na Serikali ya Zanzibar ili hatimaye kujenga jiji la kisasa visiwani humo ambalo litakuwa ni kitovu cha utalii wa maeneo ya kisasa na yale ya kihistoria.
11.3 Pemba
Mji wa Pemba ni mji ambao bado haujaingizwa vizuri kabisa katika uchumi wa nchi na umeendelea kubakia mahali penye kuahidi mafanikio bila kuyatoa. Chini ya Serikali ya CHADEMA Pemba itatengwa maalumu kuwa kitovu cha biashara ya mambo ya fedha (Financial Centre) ili kushindana na maeneo kama ya UAE, Saudi Arabia, Qatar n.k Lengo letu ni kuhakikisha kuwa Pemba inakuwa ni makao makuu ya taasisi mbalimbali za kifedha na makampuni mbalimbali. Ili kutimiza adhma hii
Kuanzia Bajeti ya 2011/2012 upembuzi yakinifu utafanywa ili kuona ni jinsi gani mkongo wa mawasiliano ambao unapita katika bahari ya Hindi unaweza kuchepushwa kuelekea Pemba na hivyo kuipatia Pemba njia za fibre optics na kurahisisha mawasiliano.
Kwa kushirikiana na Serikali ya Zanzibar utawekwa mfumo maalum wa kodi mbalimbali kwa ajili ya Pemba kuwa kivutio cha uwekezaji wa taasisi za fedha. Lengo ni kufanya Pemba kuwa ni eneo la unafuu wa kodi (Tax Haven) kwa makampuni ya ndani na ya kimataifa. Ili kuhakikisha hili linafanikiwa tutahakikisha kunakuwepo na umeme wa kudumu, huduma safi ya maji, tiba na udhibiti wa kisasa ili kuhakikisha kuwa Pemba haitotumiwa na wahalifu wa kimataifa katika masuala ya kodi.
Kwa kushirikiana na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Serikali ya Muungano itahakikisha kuwa miji ya Chake Chake na Wete inapatiwa ujenzi wa majengo ya kisasa pamoja na miundo mbinu ya kisasa na huduma za kuaminika za usafiri kati yake ya Tanga.
Ni wazi kwamba, kwa vile Serikali hiyo ya CHADEMA haijaundwa basi wale wagombea na wabunge wa CHADEMA wanaendelea kusimamia na kupigania yale. Je, haya ni bora kulinganisha na yale yanayopendekezwa na CCM na CUF? Nina uhakika wapo watu Zanzibar ambao hawakubaliani na siasa za CCM wala zile za CUF na kwa muda mrefu wamekuwa wakisubiri nafasi ya kuchagua kitu kingine.
Lakini, hakuna mtu atakayekuja kutoka akhera kuwaambia nani wamchague; hatakuja mtu kutoka peponi kuwaambia waangalie chaguo jingine. Wao wenyewe kama binadamu wenye uwezo wa kufikiri wanatakiwa kuitikia wito wa kihistoria wa kuangalia kama kuendelea na watu wale wale, wenye sera zile zile na kutoka chama kile kile kumekuwa na manufaa kwao. Wafanye ambacho Watanzania wengine wamekifanya hata sehemu ambazo ziliaminika ni ngome za CCM; waliikataa.
Wananchi wa Uzini wakituma ujumbe huo watakuwa wamewapa wananchi wa Zanzibar kile ambacho Mapinduzi yalipigania yaani uhuru wa kuamua na kuwa na utu bila kulazimishwa kufanya siasa ambazo hazina manufaa. Hili nina uhakika litafanywa na wazee na vijana na kuwa wataamua kuendelea kuambia kuwa njia pekee ni hizo mbili walizozizoea kwa karibu miaka hamsini sasa au kuna njia ya tatu bora. Nani atawaongoza? Je, itakuwa ni sawa na kusaliti? Je, kuchagua chama kingine nje ya CCM na CUF ni kutokuwa mwaminifu kwa Zanzibar? Well, kila kitu kina mwanzo wake, na tusipoangalia tunaweza kuwa mashahidi wa kitu kipya kabisa Zanzibar!
Zanzibar imepewa chaguo la tatu!
SOURCE: Raia Mwema