Kichankuli
JF-Expert Member
- Dec 18, 2008
- 887
- 189
Jana mwenyekiti wa UDP Bwan John Momose Cheyo almaaruf Bwana Mapesa alinukuliwa akiwaambia wapiga kura wa Jimbo la Busanda kuwa wasiwazomee Viongozi wa CCM badala yake wawaambie "stop this non-sense". Mimi nilishindwa kumwelewa Bwana Mapesa alimaanisha nini kwa sababu mpaka wananchi wafikie kuzomea inamaana kinachoongewa na viongozi wa CCM kimeonekana kwao kuwa ni upuuzi. kwa hiyo kuzomea ni namna moja wapo ya kufikisha ujumbe kwa wahusika kwani wengi wa wapigakura hao hawafaamu lugha ya kiingereza (achilia mbali kutokuwa na Runinga wala fedha za kununulia magazeti kama alivyowabezxa Bwana Mkuchika) ambacho kingewawezesha kustopisha hizo non sense.Pia wangeweza kupiga makofi yasiyo na kikomo, kupiga kelele ya kumtaka mwogeaji asiendelee kuongea (japo hizi zinaweza kukusababishioa kuwekwa chini ya mikono ya polisi wa CCM wasiojua haki ya raia wa nchi hii)au kuondoka kwenye kikao