Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,194
- 4,116
Serikali imesema wataalamu wa afya, wanamalizia kufanya mchakato wa namna bora na sahihi ya jinsi ya kutengeneza barakoa, zinazofaa kuvaliwa kwa wananchi kama njia mojawapo ya kujikinga na virusi vya corona.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile anasema wataalamu watakapokamilisha mchakato huo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu atatoa maelekezo kwa wananchi ya jinsi ya kuzitengeneza.
Dk Ndugulile amebainisha hayo kwenye kipindi cha Hamza Kasongo, kinachorushwa hewani na kituo cha Televisheni cha TV E jijini Dar es Salam.
Alisema barakoa zinazotengenezwa kwa vitambaa vya nguo, ndizo zitatolewa maelekezo ya namna ya kuzitengeneza, ili wananchi waweze kuzitumia kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya corona na kufuata maelekezo mengine ya jinsi ya kujikinga.
“Wataalamu wetu wanamalizia mchakato wa kuandaa maelekezo ya jinsi ya kuzitengeneza, Waziri wa Afya atatoa maelekezo ya hili, ili jamii waelewe na kuchukua hatua ya kuzitengeneza kwa kufuata njia sahihi ili ziwe na sifa, maana lazima ziwe na ‘leya’ angalau tatu ya kusaidia kuzuia kwa kiasi uwezekano wa kuambukiza na kuambukizwa,”amesema Dk Ndugulile.
Alisema hiyo itasaidia mtu akipiga chafya, kama amevaa barakoa, majimaji yatabaki ndani yake; au akikohoa virusi havitaweza kuruka na kumpata mtu mwingine, hivyo kusaidia kasi ya maambukizi kupungua.
Nchini China wao walifanikiwa kupunguza maambukizi ya virusi vya corona, baada ya raia wake kuanza kuvaa barakoa sambamba na kuchukua hatua nyingine zinazohimizwa, ikiwemo kunawa mikono na sabuni , dawa na maji yanayotitirika, kutumia vitakasa mikono na kuepuka kushika shika vitu na viungo vya mwili, hususan vya maeneo ya usoni.
Dk Ndugulile alisema hivi sasa nchini, kumekuwa na taharuki kubwa kuhusu matumizi ya barakoa. Alisema jambo hilo linapaswa kutolewa ufafanuzi, ili litumike vizuri na kwa usahihi, pamoja na njia nyingine za kuzuia maambuziki ya virusi vya corona.
“Barakoa ziko za aina nyingi, kumekuwa na hataruki kubwa kuhusu matumizi yake. Sasa wataalamu wa afya wanamalizia kuweka sawa habari za barakoa na jinsi zinavyotakiwa, kisha waziri wa afya atatoa maelekezo kwa jamii namna bora ya kuzitengeneza,”alisema.
Akifafanua kuhusu aina za barakoa na kama kuna haja ya Watanzania wote kuanza kuzitumia, Dk Ndugulile alisema kuwa barakoa zipo za aina nyingi. Kwa mfano, alisema kuna N95, ambazo huzuia maambukizi kwa ya virusi vya asilimia 95.
Sifa nyingine za barakoa hiyo ni kwamba huzuia pia bakteria kwa asilimia 100 , vumbi jingine kwa asilimia 100 na vumbi ya mimea inaposhavushwa kwa asilimia 100.
Akizungumzia aina hiyo ya barakoa, Dk Ndugulile alisema N95 kwa wakati huu zinapaswa zitumiwe zaidi na watoa huduma za afya, ambao wanahudumia wagonjwa wa virusi vya corona moja kwa moja, kwa sababu kidunia uzalishaji wake umepungua.
Alisema sio busara kwa makundi mengine kuzivaa, isipokuwa tu kwenye kundi hilo lililo hatarini. Alitaja aina nyingine ya barakoa kuwa ni zile zinazotumika kwenye vyumba vya upasuaji katika hospitali mbalimbali.
Alisema barakoa hizo zinaweza kutumiwa na watoa huduma katika hospitali mbalimbali na hata vituo vya afya, ambao hawawahudumii moja kwa moja wagonjwa wa covid-19.
Sifa za barakoa hizo za kitabibu, kwa mujibu wa wataalamu wa afya, ni kwamba zina uwezo wa kuzuia maambukizi ya virusi kwa asilimia 95, maambukizi ya bakteria kwa asilimia 80, vumbi ya kawaida kwa silimia 80 na vumbi ya mimea itokanayo na uchavushwaji kwa asilimia 80.
Aidha zipo barakoa aina ya FFP1 ambazo zinaweza kutumiwa na watu wanaofanya kazi mwenye maeneo hatarishi kama mipakani, viwanja vya ndege na hospitalini. Kwamba aina hiyo zina uwezo sawa na barakoa za zile zinazotumika kwenye vyumba vya upasuaji.
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile anasema wataalamu watakapokamilisha mchakato huo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu atatoa maelekezo kwa wananchi ya jinsi ya kuzitengeneza.
Dk Ndugulile amebainisha hayo kwenye kipindi cha Hamza Kasongo, kinachorushwa hewani na kituo cha Televisheni cha TV E jijini Dar es Salam.
Alisema barakoa zinazotengenezwa kwa vitambaa vya nguo, ndizo zitatolewa maelekezo ya namna ya kuzitengeneza, ili wananchi waweze kuzitumia kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya corona na kufuata maelekezo mengine ya jinsi ya kujikinga.
“Wataalamu wetu wanamalizia mchakato wa kuandaa maelekezo ya jinsi ya kuzitengeneza, Waziri wa Afya atatoa maelekezo ya hili, ili jamii waelewe na kuchukua hatua ya kuzitengeneza kwa kufuata njia sahihi ili ziwe na sifa, maana lazima ziwe na ‘leya’ angalau tatu ya kusaidia kuzuia kwa kiasi uwezekano wa kuambukiza na kuambukizwa,”amesema Dk Ndugulile.
Alisema hiyo itasaidia mtu akipiga chafya, kama amevaa barakoa, majimaji yatabaki ndani yake; au akikohoa virusi havitaweza kuruka na kumpata mtu mwingine, hivyo kusaidia kasi ya maambukizi kupungua.
Nchini China wao walifanikiwa kupunguza maambukizi ya virusi vya corona, baada ya raia wake kuanza kuvaa barakoa sambamba na kuchukua hatua nyingine zinazohimizwa, ikiwemo kunawa mikono na sabuni , dawa na maji yanayotitirika, kutumia vitakasa mikono na kuepuka kushika shika vitu na viungo vya mwili, hususan vya maeneo ya usoni.
Dk Ndugulile alisema hivi sasa nchini, kumekuwa na taharuki kubwa kuhusu matumizi ya barakoa. Alisema jambo hilo linapaswa kutolewa ufafanuzi, ili litumike vizuri na kwa usahihi, pamoja na njia nyingine za kuzuia maambuziki ya virusi vya corona.
“Barakoa ziko za aina nyingi, kumekuwa na hataruki kubwa kuhusu matumizi yake. Sasa wataalamu wa afya wanamalizia kuweka sawa habari za barakoa na jinsi zinavyotakiwa, kisha waziri wa afya atatoa maelekezo kwa jamii namna bora ya kuzitengeneza,”alisema.
Akifafanua kuhusu aina za barakoa na kama kuna haja ya Watanzania wote kuanza kuzitumia, Dk Ndugulile alisema kuwa barakoa zipo za aina nyingi. Kwa mfano, alisema kuna N95, ambazo huzuia maambukizi kwa ya virusi vya asilimia 95.
Sifa nyingine za barakoa hiyo ni kwamba huzuia pia bakteria kwa asilimia 100 , vumbi jingine kwa asilimia 100 na vumbi ya mimea inaposhavushwa kwa asilimia 100.
Akizungumzia aina hiyo ya barakoa, Dk Ndugulile alisema N95 kwa wakati huu zinapaswa zitumiwe zaidi na watoa huduma za afya, ambao wanahudumia wagonjwa wa virusi vya corona moja kwa moja, kwa sababu kidunia uzalishaji wake umepungua.
Alisema sio busara kwa makundi mengine kuzivaa, isipokuwa tu kwenye kundi hilo lililo hatarini. Alitaja aina nyingine ya barakoa kuwa ni zile zinazotumika kwenye vyumba vya upasuaji katika hospitali mbalimbali.
Alisema barakoa hizo zinaweza kutumiwa na watoa huduma katika hospitali mbalimbali na hata vituo vya afya, ambao hawawahudumii moja kwa moja wagonjwa wa covid-19.
Sifa za barakoa hizo za kitabibu, kwa mujibu wa wataalamu wa afya, ni kwamba zina uwezo wa kuzuia maambukizi ya virusi kwa asilimia 95, maambukizi ya bakteria kwa asilimia 80, vumbi ya kawaida kwa silimia 80 na vumbi ya mimea itokanayo na uchavushwaji kwa asilimia 80.
Aidha zipo barakoa aina ya FFP1 ambazo zinaweza kutumiwa na watu wanaofanya kazi mwenye maeneo hatarishi kama mipakani, viwanja vya ndege na hospitalini. Kwamba aina hiyo zina uwezo sawa na barakoa za zile zinazotumika kwenye vyumba vya upasuaji.