View attachment 3352951
Wanaharakati hao wameamua kufanya hivo kwa kupanda meli iliyoondoka bandari ya Catania kwenye visiwa vya Sicily ambavyo haviko mbali sana na Gaza.
Mwezi uliopita meli kama hiyo zinazoongozwa na taasisi ya Freedom Flotilla ilishambuliwa na Israel na kuwaka moto kulazimika kuokolewa kwa wanaharakati waliokuwemo humo.
Huku akibubujikwa na machozi muda mfupi kabla kupanda meli hiyo yenye misaad Greta alisema ni lazima tuendelee kufanya juhudi za kufikisha misaada Gaza kwani siku tukisitisha kufanya juhudi hizo itakuwa ndio tumesita kuwa watu..Akaongeza kwa kusema juu ya kwamba kufanya hivyo ni hatari lakini uhatari wake haukaribiii hata kidogo ubaya wa ukimya wa dunia nzima kwa madhila yanayowapata wapalestina.