Kama walikua Waislam walishahadia
Ash-hadu an la ilaha illa Allah, Wa ash-hadu anna Muhammadan Rasulu-Allah.”?
Na kama hawakushahadia wanapataje sifa za kua waislamu Sheikh
adriz?
وَإِذۡ قَالَ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ يَٰبَنِيٓ إِسۡرَٰٓءِيلَ إِنِّي رَسُولُ ٱللَّهِ إِلَيۡكُم مُّصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيَّ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَمُبَشِّرَۢا بِرَسُولٖ يَأۡتِي مِنۢ بَعۡدِي ٱسۡمُهُۥٓ أَحۡمَدُۖ فَلَمَّا جَآءَهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ قَالُواْ هَٰذَا
Na Isa bin Mariamu alipo sema: Enyi Wana wa Israili! Hakika mimi ni Mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu, ninaye thibitisha yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati, na mwenye kubashiria kuja Mtume atakaye kuja baada yangu; jina lake ni Ahmad! Lakini alipo waletea hoja zilizo wazi, walisema: Huu ni uchawi ulio dhaahiri! (61 : 6 )
1. Aliposema yeye ni Mtume wa Mungu ; Shahada kuhuhu yeye na Mungu
2. Akataja kuja kwa Mtume na akasema jina lake ni Ahmad (Muhammad) : hapo Yesu mwenyewe (Amani iwe juu yake) kashakubali utume wa Muhammad (Peace and blessings be upon Him) na akiwaambia Wanafunzi wake wakubali .
Uilsamu maana yake ; kujisalimisha kwa Moka mlezi muumba kwa kumpwekesha yeye (kumuabudu peke yake ) , kumtii yeye , kufuata mitume yake na kuachana na washirikina na watu wake.
Mtu awe enzi ya Adam , Nuh , Yusuph , Yakubu nk ni Muislamu ilimradi tu hafanyi ushirikina kwa kuabudu Miungu wengine au kuabudu mwenyewezi Mungu pamoja na Miungu wengine
2. Akawafuata mafundisho wa Mitume katika zama mfano watu wa Yesu wasikilize na kumfuata Yeye au Nuh nk
3. Wakatii maarisho yake mfano kuswali , zaka , kusaidia nk kuacha makatazo mfano zinaa , mauaji nk Kutokana na mafundisho ya MaNabii wao katika wakati husika watahesabika Waislamu.
Ndio maana Wakristo wa Najran Uarabuni kipindi Cha Mtume Muhammad walipokuja na msafara wao kumuona baada kusomewa mafundisho ya Uislamu walikubali na kusema kuwa walikuwa Waislamu toka zamani
ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِهِۦ هُم بِهِۦ يُؤۡمِنُونَ
Wale tulio wapa Kitabu kabla yake (mfano watu wa Yesu injili) wawanakiamini hiki. (Qur'an)
وَإِذَا يُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا بِهِۦٓ إِنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّنَآ إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلِهِۦ مُسۡلِمِينَ
Na wanapo somewa wanasema: Tunaiamini. Hakika hii ni Haki inayo toka kwa Mola wetu Mlezi. Hakika sisi kabla yake tulikuwa ni Waislamu, tulio nyenyekea. (28 : 52 - 53 )
☝️☝️ Hizo Aya zilishuka sababu ya tukio la ujionwa Wakristo wa Najran , walikuwa kama Orthodox sio Wakristo wa utatu mtakatifu baada ya kuona Uislamu na mafundisho yake kuwa hakuna kumshirikisha Mungu unakataza maovu na kuiamrisha mema wakasema misingi hiyo ndio walikuwa wanafuata na kama huo ndio Uislamu basi wao walikuwa Waislamu toka kitambo na wakakubali kumfuata Mtume Muhammad peace and blessings be upon Him