Wanafunzi ni wa kuogopa kama ukoma

Wanafunzi ni wa kuogopa kama ukoma

Good testimony....Hongera sana maana wengi watajifunza nikiwemo mimi maana kuna binti ndo yuko form four halafu simuelewi. Sijui wanapata wapi courage hawa watoto...

Nisichokiamini hapa ni uwepo wako kazini miezi mitano na uwezo wa kuwa na akiba ya milioni nne ulizolipa. Kwa muda huo mfupi hata probation period ulikuwa hujamaliza na kwa vyovyote vile muda uliokimbilia Shinyanga mpaka masuala yasuluhishwe usingerudishwa kazini. Mshahara wako na d moja ya kiswahili ukutoshe kuishi na kumrudisha binti shule huku unalea na mtoto ambae angekuwa kwa bibi mzaa binti ni vigumu kuamini labda ungetuambia wazazi wako na ndugu ndio waliochangia gharama hizo.
 
sheria ziko wazi kabisa kijana kwann ukufikiria hilo
 
Kwahiyo D ya kiswahili ndio inakufanya usijue tofauti ya "jera" na "jela".
Kizazi chenu mlihudhuria shule lakini bure kabisa.
Kila jambo lina matokeo yake aidha yawe chamya au hasi.
Sasa huyo binti inabidi umuoe; umeeleza mengi lakini hujaeleza chochote kuhusu mtoto.
duu nooma
 
Nisichokiamini hapa ni uwepo wako kazini miezi mitano na uwezo wa kuwa na akiba ya milioni nne ulizolipa. Kwa muda huo mfupi hata probation period ulikuwa hujamaliza na kwa vyovyote vile muda uliokimbilia Shinyanga mpaka masuala yasuluhishwe usingerudishwa kazini. Mshahara wako na d moja ya kiswahili ukutoshe kuishi na kumrudisha binti shule huku unalea na mtoto ambae angekuwa kwa bibi mzaa binti ni vigumu kuamini labda ungetuambia wazazi wako na ndugu ndio waliochangia gharama hizo.
Nilikopa mkuu
 
Good testimony....Hongera sana maana wengi watajifunza nikiwemo mimi maana kuna binti ndo yuko form four halafu simuelewi. Sijui wanapata wapi courage hawa watoto...
Hahaha we jamaa kiboko badala useme wewe haujielewi then unasema binti haumuelewi!!kemea pepo
 
Kwahiyo D ya kiswahili ndio inakufanya usijue tofauti ya "jera" na "jela".
Kizazi chenu mlihudhuria shule lakini bure kabisa.
Kila jambo lina matokeo yake aidha yawe chamya au hasi.
Sasa huyo binti inabidi umuoe; umeeleza mengi lakini hujaeleza chochote kuhusu mtoto.
Na wewe hiyo chamya ndio nini..unajifanya kumkosoa mwenzako tu tena bila kufahamu ni athari ya lugha mama kwa makabila yetu.
 
Habari wana MMU,

Mwaka 2011 ni Mwaka ambao ulinifanya mpaka leo wanafunzi ni waogope. Mwaka 2010 mwezi wa 8 niliajiriwa wilayani Bunda kama post yangu ya kwanza nilifika hapo kipindi hicho nilikuwa bado mdogo ki umri pia hata akili yangu ilikuwa bado haijakomaa.

Nilikuwa na miaka 19. Nilikuwa nimepanga balili kwa mzee mmoja anaitwa mzee Masatu, jirani na hapo nilipokuwa nimepanga kulikuwepo na binti mmoja ambaye alikuwa akisoma Secondary kidato cha pili.

Nilianza naye uhusiano kwa bahati mbaya January 2011 aliniambia kuwa hajaziona siku zake ndipo nikanunua kipimo cha mimba nikamuita nilipokuwa nimepanga akaja nikampima mimba na kubaini kuwa ana mimba.

Akili yangu Ilihama ghafla nikaanza kuhisi jela ile naiona ndoto zangu zimeyeyuka!Kwa kweli nilikoswa raha isitoshe toka nianze kazi nilikuwa na miezi mi tano tu.Ilibidi tuanze mchakato wa kuitoa ikashindikana, zaidi ya Mara tatu.

Mwezi wa pili yule binti aliugua sana na hapo wazazi wake walipogundua anamimba isitoshe alikuwa na miaka 15 baada ya kubanwa kwao alinitaja nikatoroka na kukimbilia Shinyanga nilimpigia simu baba mwenye nyumba nikamuomba aka jaribu kuongea na ile familia ili tuone namna ya kulimaliza tatizo.

Familia ile ilikubali kwa kunipatia masharti 3 kumrudishia gharama zake zote za kumsomesha Million 4, alafu na kuendelea kuihudumia mimba na kuhakikisha atakapojifungua namrudisha shule kwa gharama zangu.

Masharti yale niliyakubali maana kupoteza kazi na ukizingatia nina D Moja tu ya kiswahili na kuishia jela niliona pesa makaratasi, mwaka 2012 nilimrudisha shule toka huo mkasa unikute nikiona mwanafunzi hata kama ni mzuri kiasi gani nahisi jela hiyo.

Nawasilisha
UNA BAHATI SANA MKUU!
 
Back
Top Bottom