Wanafunzi 6 wafariki kwa kugongwa na basi Mbeya

Wanafunzi 6 wafariki kwa kugongwa na basi Mbeya

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Wanafunzi 6 wa shule ya Sekondari Chalangwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, waliokuwa wakifanya mazoezi barabara kuu ya Chunya-Mbeya , wamefariki dunia kwa kugongwa na basi la Safina aina ya Yutong lenye namba za usajili T 194 DCE, linalofanya safari zake kutoka Lwalaje wilayani Chunya na Mbeya mjini, huku wengine nane wamejeruhiwa, chanzo cha ajali hiyo kikitanjwa kuwa ni uzembe wa dereva

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Bw.Mbarack Batenga baada ya kutokea ajali hiyo ametoa maagizo kwa wakuu wa shule na Mkurugenzi na kuahidi atakae kaidi agizo hilo kushughulikiwa




Chanzo: ITV DIGITAL
 
Wanafunzi 6 wa shule ya Sekondari Chalangwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, waliokuwa wakifanya mazoezi barabara kuu ya Chunya-Mbeya , wamefariki dunia kwa kugongwa na basi la Safina aina ya Yutong lenye namba za usajili T 194 DCE, linalofanya safari zake kutoka Lwalaje wilayani Chunya na Mbeya mjini, huku wengine nane wamejeruhiwa, chanzo cha ajali hiyo kikitanjwa kuwa ni uzembe wa dereva

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Bw.Mbarack Batenga baada ya kutokea ajali hiyo ametoa maagizo kwa wakuu wa shule na Mkurugenzi na kuahidi atakae kaidi agizo hilo kushughulikiwa




Chanzo: ITV DIGITAL
Pole sana Kwa wafiwa

Lakini pia tuangalie matumizi sahihi ya barabara
 
Pole sana. Mazingira yalikuwa mabaya. Saa kumi na moja asubuhi bado giza, barabara kuu na wanafunzi si rahisi kujipanga kwa utaratibu.
 
Wanafunzi 6 wa shule ya Sekondari Chalangwa iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya mkoa wa Mbeya, waliokuwa wakifanya mazoezi barabara kuu ya Chunya-Mbeya , wamefariki dunia kwa kugongwa na basi la Safina aina ya Yutong lenye namba za usajili T 194 DCE, linalofanya safari zake kutoka Lwalaje wilayani Chunya na Mbeya mjini, huku wengine nane wamejeruhiwa, chanzo cha ajali hiyo kikitanjwa kuwa ni uzembe wa dereva

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Bw.Mbarack Batenga baada ya kutokea ajali hiyo ametoa maagizo kwa wakuu wa shule na Mkurugenzi na kuahidi atakae kaidi agizo hilo kushughulikiwa




Chanzo: ITV DIGITAL
Watanzania tuogope barabara kuliko ukimwi maana barabara zinaua kuliko ukimwi. Kule mwanza watu wa mazoezi walikufa barabarani tena huko mbeya watu wamekufa barabarani kwa kufanya mazoezi. Hivi serikali bado tu hawajashitukia hii trend. Open spaces zinajengwa maghorofa...duh
 
Poleni sana wafiwa. Ila na wakuu wa shule pia mna wajibu wa kuepukana na haya matukio ya vifo vinavyoweza kuepukika.

Sidhani kama kulikuwa na sababu za msingi za wanafunzi kuacha kufanya hayo mazoezi kwenye eneo la shule, na kwenda kufanya kwenye barabara kuu.
 
Back
Top Bottom