Wanachuo wengi maisha yao yako hivi!

Wanachuo wengi maisha yao yako hivi!

Habarini wanaMMU,

Nimependa kuShare nanyi maisha ya wanachuo walio wengi ambayo ni uzinzi,ulevi bila kusahau Disco usiku kucha.
6228b10b2e01b40c500a883b2b3e519a.jpg


Ni hatari sana maisha hayo.

Kama ulipitia maisha hayo tupe experience yako.

Karibu!!!!!!!
picha ulochora nzuri,ila ishi maisha yako acha unafiki na uandishi pasipo malipo,bwege!
 
sioni hata uzinzi humo! kwani si kila mmoja kalala kitanda chake!
Mbona sie wakati tuko JKT tulikuwa tunakwenda kulala kwenye mahanga ya wanaume kwa kuwa yalikuwa karibu na kombania ili afande akipuliza filimbi ya mchakamchaka tuwahi kufoleni na hatukuwa wazinzi na wala hatukuwa tuna duuu!!!!
 
Wenye tabia ulizozitaja hapo chuoni hawafiki hata 20%. Sa sijui unazungumzia wingi upi.

Unajaribu kukieleza ni propaganda za mtaani.

Nilipokuwa Sekondari nilifikiri Kama wewe lakini Mara nilipoingia chuoni mambo yalikuwa kinyume kwa asilimia kubwa.

Suala kubwa nililoliona ni Uhuru lakini hayo mengine ni Porojo za watu wasiokaa na makundi yote.

Chuoni kuna makundi mengi,
Kuna wenye uwezo ambao kwa vyuo vya serikali Kama Udsm, Sua, Udom, Mzumbe, Muhas n.k kundi hili hawazidi 20% ya wanachuo katika vyuo tajwa hapo juu(serikali).

Wenye Mkopo.
Kundi hili kwa baadhi ya vyuo ni wengi huku vyuo vingine wakiwa ni wachache.

Unachojaribu kuelezea mtoa Uzi ni kuwa Watu waliokaribu yako ndio wenye tabia hizo ulizoziainisha.

Nilitegemea utaje miongoni mwa yafuatayo ambayo wanachuo wengi hupendelea kufanya wakiwa chuoni;
1. Kuvaa Earphones masikioni kila Mara.(68%).
2. Kuvaa mabegi ya migongoni na mikoba kwa wadada.(95%)
3.Kulala Sana mchana hasa siku za wikiend. Kutokana na kukosa kwa kwenda.(70%)
4. Kukaa bila ramani au ratiba yoyote pale wakisubiri vipindi vilivyoacha na masaa yasiopungua mawili.(75%) by
5. Kutokujali mambo yajayo baada ya wao kumaliza chuo.(86%)
6. Kuvaa kufuatana na mitindo husika ya wakati.(70%).
7.kumilikia simu kupangusa-Smartphone(87%).


1. Kwenda disco,Nightclub, n.k (30%).
2. Kusheherekea Sikukuu za kuzaliwa. (10%).
3. Michezo,mitindo, na burudani(25%).
4. kucheki Movies kwenye PC(40%).
5. kutembea mtu na mpenzi wake (10%).
6. Kutembea mwenyewe
Mwaka wa Kwanza 45%
Mwaka wa pili. 10%
Mwaka wa tatu 35%.

7.Kutembea zaidi ya wawili
Mwaka wa Kwanza 55%
Mwaka wa pili 35%.
Mwaka wa tatu.12%.

8.kutembea watu wawili pekee.
Mwaka wa kwanza 30%
Mwaka wa pili 60%
Mwaka wa tatu's 65.
Hongera kwa takwimu nzuri.Japo sample yako ulichukua kwa walimu pekee,sijui kwa wanaisomea udaktari,uNesi,uhandisi n.k hali ikoje?
 
Jihadhari usijemaliza chuo na AIDS badala ya A's...ts okay to have fun but usipitilize,matumizi mabaya ya uhuru wa mwanachuo yanaweza kukuponza...my Uni days nlikua shule shule na mimi ili nipate GPA nzuri,apart frm school nlipenda kushiriki ktk projects za academic groups zile,inakujenga kuwa mtu makini
Ushauri mzuri sana dada
 
Yaani watu wanadinyana chini ye juu amekodolea laptop? Anafanya assignment?[emoji23][emoji23]
 
Mimi nimesoma UDSM hapo miaka kadhaa ya hapo nyuma. Nimekaa na walevi sana sana na sijawahi kuinywa mpaka leo siijui pombe so msifanye Generalization katika maisha ya wanachuo. Ninyi ndio mnachochea Magufuli atumie hoja zenu kunyima wanafunzi mikopo akijua watatanulia maisha na kununulia ma sub woofers (Sabufa) uzi wako wa kichochezi hivii
 
Kimsingi hayo maisha ya chuo/ujana, alimradi husahau kilichokupeleka huko. Wale wanaokomaa na msuli na kusahau kuishi kiasi, ndiyo wanafika miaka 50/60 wanafanya mambo ya ajabu.
 
Back
Top Bottom