Wanachama wa Mwanzo wa TANU walitoka Rufiji

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,922
30,271
WANACHAMA WA MWANZO WA TANU WALITOKA RUFIJI

Shughuli ya usajili wa TANU ilifanywa na watu watatu wenye kadi zinazoongozana: Julius Nyerere kadi no. 1, Ally Sykes kadi no. 2 na Abdul Sykes kadi no. 3.

Walikubaliana Nyerere akasajili chama kwa msajili kisha wote watatu wakutane nyumbani kwa Ally Sykes Kipata Street.

Taarifa alizokujanazo Nyerere ni kuwa msajili amekataa kuisajili TANU na sababu Nyerere alishindwa kuonyesha orodha ya wanachama.

Abdul akasema atafutwe Said Chamwenyewe.

Said Chamwenyewe alipofika kwa Abdul Sykes akapewa rejesta buku na kadi za TANU aende Rufiji akaandikishe wanachama.

Said Chamwenyewe alikwenda Rufiji anaendesha baiskeli akarudi na rejesta buku ina orodha ndefu ya wanachama wapya wa TANU na fedha za manunuzi ya kadi.

Rejesta buku akamkabidhi Abdul Sykes na fedha za kadi akamkabidhi Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa TANU.

Nyerere aliwasilisha orodha ya wanachama kwa msajili na TANU ikasajiliwa.

TANU ilipata usajili mwezi November 1954. Kwa nini ilikuwa kazi rahisi kupata wanachama wa TANU Rufiji?

Rufiji takriban wenyeji wake wote ni Waislam na wafuasi wa Tariqa Qadiriyya. Khalifa wa Qadiriyya, yaani Kiongozi Mkuu alikuwa Sheikh Hassan bin Ameir.

Hawa wafuasi wanafahamika kwa jina la "Murid," na sifa yao kubwa ni utii kwa kiongozi wao.

Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mjumbe wa TAA Political Subcommittee toka 1950 na mwanachama wa TANU mstari wa mbele 1954.

Said Chamwenyewe alikuwa mwenyeji wa Rufiji na Qadiriyya kama walivyokuwa Warufiji wengi. Hii ilifanya kazi yake ya kueneza TANU Rufiji kuwa nyepesi sana.

Picha ya kwanza kushoto ni Said Chamwenyewe na picha ya pili angalia mshale. Picha ya tatu Said Chamwenyewe wa mwisho kulia waliokaa.

1694601804752.png

1694601869161.png

1694601897179.png
 
Lile lizee limeleta tena propaganda zngn kujeni msome
Mpaji Mungu,
Hakika mpaji ni Mungu.

Yeye ndiye huwapa wale awatakao tena akawapa bila hesabu.

Nashagazwa kwa nini umeghadhibika kiasi hiki na kuandika kuwa nimeleta propaganda.

''Lile zee.''

Hakika mimi ni mzee umri wangu ni miaka 71.

Ingetosha kwa wewe kuniwekea staha kwani mimi ni sawa na baba yako.

Badala yake unanitukana bila ya sababu na kunionyesha ufedhuli.

Huku ni kuwafedhehesha wazazi wako kuwa hawakufunza adabu.

Hayo niliyoandika ni kweli tupu labda kwako ni historia mpya ambayo hukupata kufundishwa si shule ya msingi. sekondari au Chuo Kikuu.

Mimi huwasomesha watu historia hii na wengi wao hupigwa na butwaa na wala hawahamaki kama wewe.

Wao huniuliza imekuwaje historia hii haikuhifadhiwa hadi nilipoiandika mimi?

Huniuliza, ''Mohamed hawa watu umejuana nao vipi na ulikuwa karibu yao kwa kiasi gani?''

Jibu langu huwa kuwa wengine ni baba zangu na wengine babu zangu na baadhi nimepata kuwaona na wengine mimi napata akili wao washafariki.

Nakuwekea picha hapo chini unione nilivyokuwa kijana nina miaka 34 na nilikuwa nimeshamaliza kuandika kitabu cha Abdul Sykes.

1694602590736.png

Ally Sykes na Mwandishi Muthaiga Club Nairobi 1989​
 
Kama kawaida yako kuleta historia za kumdogosha JKN. Jihad propagandist. Historia ya nchi iliishaandikwa na iko wazi.
 
Dar mpka Rufiji kwa Baiskeli?

Hakika ilikuwa safari haswa! Umalize mkuranga uipate kibiti ambayo ndio rufiji ya miaka hiyo ni shughuli pevu

Labdq rufiji ilijumuisha na maeneo ya huku juu mkuranga, kisiju lakini bado watu walipambana hakika

Haikuwa rahisi
 
Kama kawaida yako kuleta historia za kumdogosha JKN. Jihad propagandist. Historia ya nchi iliishaandikwa na iko wazi.
Jiwe...
Historia ya kweli ya Nyerere haikupata kuandikwa na ndiyo maana nilipoandika kitabu cha Abdul Sykes na ndani yake nikaeleza historia ya kweli ya Nyerere kitabu changu kiliwashtua walimu na wanafunzi wengi wa African History kiasi kilifanyiwa review na mabingwa wa African Historit: John Iliffe, Jonathon Glassman na James Brennan.

Review zao ziko katika Cambridge Journal of African History.

Historia ya Nyerere ilikuwa haifahamiki vyema wakati kitabu cha Abdul Sykes kinachapwa na Minerva Press, London 1998.

Sijapata kuandika au kutoa mhadhara kote nilikoalikwa nikamdogosha Mwalimu Nyerere.
Ikiwa una ushahidi wa hilo leta ushahidi hapa jamvini.

Sikiliza video hiyo hapo chini:

 
Dar mpka Rufiji kwa Baiskeli?

Hakika ilikuwa safari haswa! Umalize mkuranga uipate kibiti ambayo ndio rufiji ya miaka hiyo ni shughuli pevu

Labdq rufiji ilijumuisha na maeneo ya huku juu mkuranga, kisiju lakini bado watu walipambana hakika

Haikuwa rahisi
Chillah,
Mimi nimeipita Kilwa Raod nikienda Rufiji kwa nia ya kutazama na kujaribu kufikiri mwaka wa 1954 Kilwa Road na vijiji vyake kuelekea Rufiji wakati ule ilikuwaje.

Nilisimama katika vijiji vya njiani na kuangalia hali ya sasa nikijaribu kuwaza hali ilikuwa miaka ile.
Hakika kazi ilikuwa ngumu sana.
 
Huna adabu we kijana, ndo maana mtaangaika sana na haya maisha.
Covax,
Usimlaumu huyu kijana.

Watu wengi wanaposikia historia ya Mwalimu Nyerere nikiieleza kupitia Nyaraka za Sykes hupandwa na hasira.

Watu ambao hawaghadhibiki ni wasomi nje ya mipaka yetu hawa huniuliza maswali mengi kutafuta uhakika wa niliyoandika.

Hapa nyumbani wengi aanashtuliwa na huu ukweli kuwa harakati hizi zilianza na miaka mingi sana nyuma na Kleist Sykes ndiye aliyewasha moto wa harakati hizi.

Kinawachoma sana ni kuona mchango wa Waislam.
Hawapendi kusikia hilo.
 
Mpaji Mungu,
Hakika mpaji ni Mungu.

Yeye ndiye huwapa wale awatakao tena akawapa bila hesabu.

Nashagazwa kwa nini umeghadhibika kiasi hiki na kuandika kuwa nimeleta propaganda.

''Lile zee.''

Hakika mimi ni mzee umri wangu ni miaka 71.

Ingetosha kwa wewe kuniwekea staha kwani mimi ni sawa na baba yako.

Badala yake unanitukana bila ya sababu na kunionyesha ufedhuli.

Huku ni kuwafedhehesha wazazi wako kuwa hawakufunza adabu.

Hayo niliyoandika ni kweli tupu labda kwako ni historia mpya ambayo hukupata kufundishwa si shule ya msingi. sekondari au Chuo Kikuu.

Mimi huwasomesha watu historia hii na wengi wao hupigwa na butwaa na wala hawahamaki kama wewe.

Wao huniuliza imekuwaje historia hii haikuhifadhiwa hadi nilipoiandika mimi?

Huniuliza, ''Mohamed hawa watu umejuana nao vipi na ulikuwa karibu yao kwa kiasi gani?''

Jibu langu huwa kuwa wengine ni baba zangu na wengine babu zangu na baadhi nimepata kuwaona na wengine mimi napata akili wao washafariki.

Nakuwekea picha hapo chini unione nilivyokuwa kijana nina miaka 34 na nilikuwa nimeshamaliza kuandika kitabu cha Abdul Sykes.

View attachment 2747882
Ally Sykes na Mwandishi Muthaiga Club Nairobi 1989​
Amazing, hongera sana haijalishi hata kama kuna mahali sikubaliani na skewness yako kuwa bias kwenye dini Yako, hongera sana na uishi miaka mingi zaidi. Encyclopedia ya Tanganyika mojawapo ni wewe, Mohamed Said a.k.a The Encyclopedia of Tanganyika history 🙏🙏🙏
 
Amazing, hongera sana haijalishi hata kama kuna mahali sikubaliani na skewness yako kuwa bias kwenye dini Yako, hongera sana na uishi miaka mingi zaidi. Encyclopedia ya Tanganyika mojawapo ni wewe, Mohamed Said a.k.a The Encyclopedia of Tanganyika history 🙏🙏🙏
Wad....
Ahsante sana.
Maneno hayo yako aliyasema Jonathon Glassman wa Northwestern University, Evanston, Chicago alikonialika kuzungumza.

Katika neno la shukurani alisema kuna mengi hakubaliani na mimi lakini alichojifunza kutoka kwangu ni ukweli kuwa Nyerere alifika pale alipofika katika kupigania uhuru wa Tanganyika kwa msaada mkubwa wa Waislam.
 
WANACHAMA WA MWANZO WA TANU WALITOKA RUFIJI

Shughuli ya usajili wa TANU ilifanywa na watu watatu wenye kadi zinazoongozana: Julius Nyerere kadi no. 1, Ally Sykes kadi no. 2 na Abdul Sykes kadi no. 3.

Walikubaliana Nyerere akasajili chama kwa msajili kisha wote watatu wakutane nyumbani kwa Ally Sykes Kipata Street.

Taarifa alizokujanazo Nyerere ni kuwa msajili amekataa kuisajili TANU na sababu Nyerere alishindwa kuonyesha orodha ya wanachama.

Abdul akasema atafutwe Said Chamwenyewe.

Said Chamwenyewe alipofika kwa Abdul Sykes akapewa rejesta buku na kadi za TANU aende Rufiji akaandikishe wanachama.

Said Chamwenyewe alikwenda Rufiji anaendesha baiskeli akarudi na rejesta buku ina orodha ndefu ya wanachama wapya wa TANU na fedha za manunuzi ya kadi.

Rejesta buku akamkabidhi Abdul Sykes na fedha za kadi akamkabidhi Iddi Faiz Mafungo Mweka Hazina wa TANU.

Nyerere aliwasilisha orodha ya wanachama kwa msajili na TANU ikasajiliwa.

TANU ilipata usajili mwezi November 1954.
Kwa nini ilikuwa kazi rahisi kupata wanachama wa TANU Rufiji?

Rufiji takriban wenyeji wake wote ni Waislam na wafuasi wa Tariqa Qadiriyya.
Khalifa wa Qadiriyya, yaani Kiongozi Mkuu alikuwa Sheikh Hassan bin Ameir.

Hawa wafuasi wanafahamika kwa jina la "Murid," na sifa yao kubwa ni utii kwa kiongozi wao.

Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mjumbe wa TAA Political Subcommittee toka 1950 na mwanachama wa TANU mstari wa mbele 1954.

Said Chamwenyewe alikuwa mwenyeji wa Rufiji na Qadiriyya kama walivyokuwa Warufiji wengi.
Hii ilifanya kazi yake ya kueneza TANU Rufiji kuwa nyepesi sana.

Picha ya kwanza kushoto ni Said Chamwenyewe na picha ya pili angalia mshale.
Picha ya tatu Said Chamwenyewe wa mwisho kulia waliokaa.

Hizi articles zinakubomoa badala ya kukujenga! Udini mbaya
 
Hizi articles zinakubomoa badala ya kukujenga! Udini mbaya
Kolola,
Sijapatapo kuandika udini.
Ningekuwa naandika udini nisingekuwa ndani ya: Cambridge Journal of African History, Dictionary of African Biography, vitabu vyangu visingechapwa na Oxford University Press, nisingealikwa kuzungumza University of Johannesburg, Ibadan, Iowa, Northwestern, Kenyatta nk.

Sasa wapi nimebomolewa?

Wewe hupendi kalamu yangu kwa kuwa imeandika historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika na kuonyesha mchango wa Waislam.

Nimeibadili historia yote kama ilivyozoeleka.

Hili ndilo linalowachoma wengi na mwisho hutaka kujibanza nyuma ya kichaka cha udini.
 
Huwa ni makusudi au niaje?
Theme moja ila ina maandiko zaidi ya 50+......
Ushaiandikia kitabu, Umeshaiandikia Journals na mabandiko kibao.
Je Tanganyika na Tanzania zilikoma baada ya Hapo.
Kama lengo ni kupeana historia, kuna theme Nyingi za kuzungumza, vitu vingi vya kuzungumza.
Lakini hujataka kufanya hivyo, kwa umri wango ungeweza hata kutusaidia Historia Nyingine, kama Vita ya Kagera, kuingia kwa vyama Vingi, privatization etc.
Ila umekomaa na Theme moja kila siku, haielimishi Tena, its annoying.
 
Kwa nini majina ya Sykes na hao wazee wengine akina Chamwenyewe hayapo tena kwenye siasa na uongozi wa nchi hii.
 
Kolola,
Sijapatapo kuandika udini.
Ningekuwa naandika udini nisingekuwa ndani ya: Cambridge Journal of African History, Dictionary of African Biography, vitabu vyangu visingechapwa na Oxford University Press, nisingealikwa kuzungumza University of Johannesburg, Ibadan, Iowa, Northwestern, Kenyatta nk.

Sasa wapi nimebomolewa?

Wewe hupendi kalamu yangu kwa kuwa imeandika historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika na kuonyesha mchango wa Waislam.

Nimeibadili historia yote kama ilivyozoeleka.

Hili ndilo linalowachoma wengi na mwisho hutaka kujibanza nyuma ya kichaka cha udini.
Napenda unavyofuatilia historia ya Uhuru ila upo biased. Nilikutolea mfano wa upande wa pili, unaufinya makusudi. Ungalikuwa unatenda jambo la maana ungekuwa neutral. Huu udini unazidi
 
Napenda unavyofuatilia historia ya Uhuru ila upo biased. Nilikutolea mfano wa upande wa pili, unaufinya makusudi. Ungalikuwa unatenda jambo la maana ungekuwa neutral. Huu udini unazidi
Kolola,
Hili umelijua lini?
Baada ya mimi kuandika historia ya kweli?
 
Dar mpka Rufiji kwa Baiskeli?

Hakika ilikuwa safari haswa! Umalize mkuranga uipate kibiti ambayo ndio rufiji ya miaka hiyo ni shughuli pevu

Labdq rufiji ilijumuisha na maeneo ya huku juu mkuranga, kisiju lakini bado watu walipambana hakika

Haikuwa rahisi
Wazee wa zamani walikuwa ngangari. Ilikuwa hakuna mambo viepe yai vya rojo rojo.

Hiki kizazi chetu hata kufungua chupa ya maji toto la kiume linaomba msaada.
 
Back
Top Bottom