Mohamedi Mtoi
R I P
- Dec 11, 2010
- 3,321
- 6,328
Wakuu.
Mtakumbuka kuwa mbunge wa Mtera Mheshimiwa alie kubuhu kwa Matusi Livingstone Lusinde muda mwingi wa kampeni za Arumeru alikuwa akiporomosha mipasho ya matusi badala ya kunadi sera za chama chake dhidi ya viongozi waandamizi wa chadema.
Nimeona nijitoe na kuchukua jukumu la kumshtaki kwa matusi yake aliyo kuwa anatoa, hivyo basi, kwa kutambua kuwa yeye ni mwanasiasa asiye kuwa na staha wala kidhibiti maneno kwenye mdomo wake nimeamua kumfungulia mashtaka kwenye mahakama ya wananchi, mahakama kubwa yenye madhara ya sasa na baadae kwa wanasiasa, mahakama hiyo ni wananchi hasa wa jimbo lake walio mchagua.
Nimeamua kuchoma [ku-burn] cd za matusi yake na kuanzia jumamosi na jumapili ya juma hili [siku za mapumziko baada ya kulitumikia taifa] nitakuwa stendi ya mabasi ya Dodoma nagawa bure cd hizo kwa abiria wanao kwenda Dodoma nikiamini kuwa zita wafikia wale ambao hawana fursa ya ufahamu wa kushusha [kudownload] matusi hayo kutoka kwenye youtube.
Shime wapenda mabadiliko na wote mlio chukizwa na matusi hayo niungeni mkono. Kama una laptop au kompyuta ya kawaida download matusi ya Lusinde, nunua ki kasha cha Cd ambacho ni kiasi cha shilingi elfu 10 au nunua cd za rejareja kwa shilingi 300, zi-burn kisha piga moyo konde nenda pale stendi ya ubungo mwisho wa juma tafuta gari za Dodoma wape bure abiria kiasi unacho weza.
Kwa wale wana JF walioko Dodoma, wafanye hivyo kwa kugawa kwa abiria wanao kwenda moja kwa moja Mtera. Naamini kama wengi wetu hatukupenda matusi yale wapo walio mchagua pia hawata yapenda, watajua namna ya kumuadhibu au kumsamehe.
Naomba kuwasilisha nikiamini kuwa tunaweza kama tukiamua kukomesha viongozi wazalilishaji. Popote ulipo saidia kwenye hili kwa njia yoyote.
Mtakumbuka kuwa mbunge wa Mtera Mheshimiwa alie kubuhu kwa Matusi Livingstone Lusinde muda mwingi wa kampeni za Arumeru alikuwa akiporomosha mipasho ya matusi badala ya kunadi sera za chama chake dhidi ya viongozi waandamizi wa chadema.
Nimeona nijitoe na kuchukua jukumu la kumshtaki kwa matusi yake aliyo kuwa anatoa, hivyo basi, kwa kutambua kuwa yeye ni mwanasiasa asiye kuwa na staha wala kidhibiti maneno kwenye mdomo wake nimeamua kumfungulia mashtaka kwenye mahakama ya wananchi, mahakama kubwa yenye madhara ya sasa na baadae kwa wanasiasa, mahakama hiyo ni wananchi hasa wa jimbo lake walio mchagua.
Nimeamua kuchoma [ku-burn] cd za matusi yake na kuanzia jumamosi na jumapili ya juma hili [siku za mapumziko baada ya kulitumikia taifa] nitakuwa stendi ya mabasi ya Dodoma nagawa bure cd hizo kwa abiria wanao kwenda Dodoma nikiamini kuwa zita wafikia wale ambao hawana fursa ya ufahamu wa kushusha [kudownload] matusi hayo kutoka kwenye youtube.
Shime wapenda mabadiliko na wote mlio chukizwa na matusi hayo niungeni mkono. Kama una laptop au kompyuta ya kawaida download matusi ya Lusinde, nunua ki kasha cha Cd ambacho ni kiasi cha shilingi elfu 10 au nunua cd za rejareja kwa shilingi 300, zi-burn kisha piga moyo konde nenda pale stendi ya ubungo mwisho wa juma tafuta gari za Dodoma wape bure abiria kiasi unacho weza.
Kwa wale wana JF walioko Dodoma, wafanye hivyo kwa kugawa kwa abiria wanao kwenda moja kwa moja Mtera. Naamini kama wengi wetu hatukupenda matusi yale wapo walio mchagua pia hawata yapenda, watajua namna ya kumuadhibu au kumsamehe.
Naomba kuwasilisha nikiamini kuwa tunaweza kama tukiamua kukomesha viongozi wazalilishaji. Popote ulipo saidia kwenye hili kwa njia yoyote.