Wana CCM wamtolea uvivu Dkt. Bashiru

Wana CCM wamtolea uvivu Dkt. Bashiru

Mjumbe wa NEC mkoa wa Pwani, Haji Juma anasema machache juu ya madhaifu ya Dkt. Bashiru akiwa Katibu Mkuu CCM.

CCM ilikuwa kama nyumba ya udongo iliyopigwa ripu na rangi kwa nje lakini ndani ilikuwa bado ya udongo.

Alibadilika alipo pata madaraka na kuacha alichokuamini na kulinda maslahi yake binafsi na aliyemchagua.

Dkt. Bashiru alianza kukidhoofisha chama chetu ndani na kujenga makundi yenye hatari ya ukanda.

Katika uongozi wake vikao vya CCM vilitumika kama rubber stamp tu.

Katika uchaguzi uliopita wagombea wengi walioshinda uchaguzi wa ndani ya CCM walikatwa kwa wingi kuliko wakati wowote tangu CCM ianzishwe.

Robo ya wabunge wote waliopo bungeni hawakushinda chaguzi za ndani ya CCM.

Sasa huo utakatifu wa Dkt. Bashiru unatoka wapi?

Nina mengi sana ya kusema juu ya Dkt. Bashiru.View attachment 1771052
Ni kweli kabisa na ndio maana kuna watu walidiriki kusema Awamu ya Tano ni ya kidikteta.
Maamuzi yalitolewa bila majadiliano.

Ikafika muda Magufuli mwenyewe slilewa madaraka na kutamka wazi kuwa hawezi kuchukua ushauri wala mawazo ya wengine.

Tukubali, Awamu ya Tano CCM ilikuwa disaster kisiasa.
 
Hayo yalifanywa nila mzee meko (apumzike mahali anapostahili) acheni kumsingizia Bashiru.
Wewe na mjunbe wa NEC ndani ya chama nani anajua siri za ndani ya chama?

Alafu soma uzi woote vizuri kwa utuvu naamini utaelewa tu
 
Why Katibu tu not na Mwenyekiti? Maana lao lilikua moja. Amtaje na Mwenyekiti pia kuwa alikua part and parcel ya hayo madudu. Aache unafiki
Kunasehemu amesema kuwa Bashiru alikuwa anayafanya kulinda maslahi ya mteuzi wake.
 
Chadema bana nyie kweli ni super Nyumbu , sasa upinzani wenu ni dhidi ya Hayati, Bashiru au CCM!???

Maana ni kama mnashabikia mabadiliko ndani ya CCM pasipokujijua na kuanzisha nyuzi nyingi kuwaponda kina Bashiru, Hayati, Makonda nk

Ndio maana Lowassa aliwaambia hiki chama kama kina nia ya kushika dola inabidi kibadilike kutoka ktk siasa za uanaharakati
 
Ni kweli kabisa na ndio maana kuna watu walidiriki kusema Awamu ya Tano ni ya kidikteta.
Maamuzi yalitolewa bila majadiliano.

Ikafika muda Magufuli mwenyewe slilewa madaraka na kutamka wazi kuwa hawezi kuchukua ushauri wala mawazo ya wengine.

Thubali, Awamu ya Tano CCM ilikuwa disaster kisiasa.
Walipanda mbegu zenye sumu
 
Mjumbe wa NEC mkoa wa Pwani, Haji Juma anasema machache juu ya madhaifu ya Dkt. Bashiru akiwa Katibu Mkuu CCM.

CCM ilikuwa kama nyumba ya udongo iliyopigwa ripu na rangi kwa nje lakini ndani ilikuwa bado ya udongo.

Alibadilika alipo pata madaraka na kuacha alichokuamini na kulinda maslahi yake binafsi na aliyemchagua.

Dkt. Bashiru alianza kukidhoofisha chama chetu ndani na kujenga makundi yenye hatari ya ukanda.

Katika uongozi wake vikao vya CCM vilitumika kama rubber stamp tu.

Katika uchaguzi uliopita wagombea wengi walioshinda uchaguzi wa ndani ya CCM walikatwa kwa wingi kuliko wakati wowote tangu CCM ianzishwe.

Robo ya wabunge wote waliopo bungeni hawakushinda chaguzi za ndani ya CCM.

Sasa huo utakatifu wa Dkt. Bashiru unatoka wapi?

Nina mengi sana ya kusema juu ya Dkt. Bashiru.View attachment 1771052
Mnafki tu huyu jamaa. Alikuwa wapi kipindi chote kujitokeza hadharani kuongea haya?
 
Jamaa waliamua kuupanda ubaguzi wa kikanda sasa unawatafuna

Mtu huvuna alichopanda:

Akipanda bangi, cha Arusha kitamhusu kwenye mavuno.

Bashiri na pole pole wangefikiria kujiuzulu kama vichwa vyao vingali na chembe chembe za uhai.
 
Mnafki tu huyu jamaa. Alikuwa wapi kipindi chote kujitokeza hadharani kuongea haya?

Palikuwa na mheshimiwa Mungu. Kwani nani aliweza kufurukuta enzi hizo?

Keshakwenda zake sasa wacha "kazi iendelee."

Hapo bado katelefoni, mparamagamba na wenzao kwenye lile genge lao dhwalimu waliloliasisi la wasukuma halisi.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Palikuwa na mheshimiwa Mungu. Kwani nani aliweza kufurukuta enzi hizo?

Keshakwenda zake sasa wacha "kazi iendelee."

Hapo bado katelefoni, mparamagamba na wenzao kwenye lile genge lao dhwalimu waliloliasisi la wasukuma halisi.

Au nasema uongo ndugu zangu?
Ukweli wanaouongea sasa, ungekuwa na impact sana nyakati zile. Kwasasa tunawaona wanafki tu.
 
Hii ngoma yao proper. Sisi nani kuwasemea wao leo?

Yetu mbona leo ni macho tu sana sana na kujisemea kama alivyopenda kusema mwendazake:

Hiiiiiiii!
Wacha wabaguane
 
Huu sasa ni uzuzu. Pwani haina mnec mwenye jina hilo au?
Hao nimakanjanja wa ufipanii. Sisi wanaccm tunatambua kazi nzuri na iliyotukuka aliyoifanya komredi bashiru alli kakurwaa. Kama angefanya hovyo tusingeweza kuwafurumusha wanaufipa huko majimbonii na bungenii. Acheni kutapatapa na bado kazi inaendelea
 
SEMENI TUUU KWAMBA NYIE MAKANJANJA YA HAPO UFIPANI NDO MNAHANGAIKA BILA KULALA MKIDHANI CHAMA DUME CCM KITABABAIKAA. MNATUNGA PROPAGANDA WENYEWEE HALAFU MNAJIPOST WENYEWEE. MTAPATA TAABU SAAANAA.
Kwahiyo we umeamua kumkataa mjumbe wenu wa Nec. Au ndio umetoka usingizini hujui kinachoendelea?
 
Back
Top Bottom