GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Kuomba msamaha sio ushamba hata kidogo, Ole Sabaya angeenda Clouds FM kuomba msamaha na kutubu angesamehewa na wananchi kwa uchafu na ujinga alioufanya huku akilindwa na mfalme niliyempigania Katika kitengo cha Propaganda ndani ya chama kwa lazima na sio kwamba nilipenda ilikuwa lazima. Sabaya angeikimbia laana ya wananchi, Angebakiwa na hukumu ya Dunia ambayo kwa sala na maombi ya wananchi waliomsamehe angeishi huko mahabusu kwa neema na mguso wa maombi.
Sabaya kwa kutembea na kivuli cha Marehamu akaenda clouds FM kujinasibu kwa maovu, kuwa ili uchafu na utekaji uendelee basi lazima CCM ishinde Hai, alijisahau kuwa yeye hana hata Biashara ya Bigijii lakini kaharibu biashara za watu za mabilioni ya shilingi.
Katika mfululizo wa watu waliofanya ubaya na uchafuzi wapo wengi sana sana, Sisi wengine tuliomba msamaha hapa na kwa wale wana JF tunaofahamiana na kukutana nina amani tele.
Wafuatao waombe msamaha kuna uchafu mwingi na upuuzi mwingi mmefanya.
Harrison Mwakyembe wakati wa sakata la Roma mkatoliki ulitumika kufanya Roma aogope kuongea yaliyomkuta.
Humprey na Bashiru, Mmeligawa Taifa pande mbili kwa kutumika wakati wa uchaguzi wa mwaka 2020 na ule wa serikali za mitaa. Lengo lenu lilikuwa watanzania wavunje msingi wa Baba wa Taifa waanze kuchukiana na kupigana mitaani, Mlichochea sana ccm wawachukie Wengine, Kama sio Utanzania wetu mambo yangekuwa yameharibika kabisa, Kuna wakati hata wana ccm kama mimi tulihisi wewe Bashiru na Mfalme sio Raia wa Tanzania mnatoka Burundi huko.
Paul Makonda na Mwigulu Nchemba. Mliyoyafanya ni makubwa zaidi, Bora Mwigulu ulikuwa huna la kufanya ukatimuliwa maana kuna maagizo yalizidi uwezo wako na Imani yako ukatimuliwa.
Nashauri iteni Press ongeeni kuwa mnaomba msamaha kwa mabaya mliofanya wakati wa uongozi wenu kwa kujua au kutokujua huo ndio ustaarabu, Karma is a Bitch.
Haya kuna siku watu watawashtaki tu, Hakuna atakayekubali damu za Akwilina, Ben Saanane, Risasi za Lissu na Azory yapite Bure.
Ole Sabaya alijisahau alihisi mfalme bado yupo, Mfalme hayupo. Tuliosoma nyakati tuliomba msamaha hapa kwa kutetea Uchumi unakua na Ajira kedekede huku tukisifia miradi ni pesa za ndani wakati tunajua nchi ipo chali na taabani lakini hatukuwa na jinsi ilitupasa hayo yafanyike.
Kwa sasa tunashindwa hata kutoa analysis za Uchumi kwani sisi wenyewe tulishabikia sheria mbovu za kuficha takwimu na kubana uhuru wa vyombo vya habari.
Labda Mama Samia akirekebisha sheria Itakuwa rahisi kufanya uchambuzi hapa, Sheria bado ni zile zile za Mfalme ambazo tulizifanyia Propaganda kuwa nzuri, Sheria zilibana takwimu na access ya taarifa za Serikali.
Mama Samia ahimize mawaziri kupeleka miswada ya mabadiliko ya sheria Bungeni za Mfalme.
Time will tell
Sabaya kwa kutembea na kivuli cha Marehamu akaenda clouds FM kujinasibu kwa maovu, kuwa ili uchafu na utekaji uendelee basi lazima CCM ishinde Hai, alijisahau kuwa yeye hana hata Biashara ya Bigijii lakini kaharibu biashara za watu za mabilioni ya shilingi.
Katika mfululizo wa watu waliofanya ubaya na uchafuzi wapo wengi sana sana, Sisi wengine tuliomba msamaha hapa na kwa wale wana JF tunaofahamiana na kukutana nina amani tele.
Wafuatao waombe msamaha kuna uchafu mwingi na upuuzi mwingi mmefanya.
Harrison Mwakyembe wakati wa sakata la Roma mkatoliki ulitumika kufanya Roma aogope kuongea yaliyomkuta.
Humprey na Bashiru, Mmeligawa Taifa pande mbili kwa kutumika wakati wa uchaguzi wa mwaka 2020 na ule wa serikali za mitaa. Lengo lenu lilikuwa watanzania wavunje msingi wa Baba wa Taifa waanze kuchukiana na kupigana mitaani, Mlichochea sana ccm wawachukie Wengine, Kama sio Utanzania wetu mambo yangekuwa yameharibika kabisa, Kuna wakati hata wana ccm kama mimi tulihisi wewe Bashiru na Mfalme sio Raia wa Tanzania mnatoka Burundi huko.
Paul Makonda na Mwigulu Nchemba. Mliyoyafanya ni makubwa zaidi, Bora Mwigulu ulikuwa huna la kufanya ukatimuliwa maana kuna maagizo yalizidi uwezo wako na Imani yako ukatimuliwa.
Nashauri iteni Press ongeeni kuwa mnaomba msamaha kwa mabaya mliofanya wakati wa uongozi wenu kwa kujua au kutokujua huo ndio ustaarabu, Karma is a Bitch.
Haya kuna siku watu watawashtaki tu, Hakuna atakayekubali damu za Akwilina, Ben Saanane, Risasi za Lissu na Azory yapite Bure.
Ole Sabaya alijisahau alihisi mfalme bado yupo, Mfalme hayupo. Tuliosoma nyakati tuliomba msamaha hapa kwa kutetea Uchumi unakua na Ajira kedekede huku tukisifia miradi ni pesa za ndani wakati tunajua nchi ipo chali na taabani lakini hatukuwa na jinsi ilitupasa hayo yafanyike.
Kwa sasa tunashindwa hata kutoa analysis za Uchumi kwani sisi wenyewe tulishabikia sheria mbovu za kuficha takwimu na kubana uhuru wa vyombo vya habari.
Labda Mama Samia akirekebisha sheria Itakuwa rahisi kufanya uchambuzi hapa, Sheria bado ni zile zile za Mfalme ambazo tulizifanyia Propaganda kuwa nzuri, Sheria zilibana takwimu na access ya taarifa za Serikali.
Mama Samia ahimize mawaziri kupeleka miswada ya mabadiliko ya sheria Bungeni za Mfalme.
Time will tell