Nyalotsi
JF-Expert Member
- Jul 20, 2011
- 6,989
- 5,066
Nini huwa kinawajia vichwani mwenu pale mtoto wako wa kiume anapokutambulisha mchumba ambaye wewe hujapendelea? Ni kwanini nyie ndio huwa mnakuwa na vikwazo kuliko kina baba? Akiwa ni binti yako ndio anawekewa vikwazo hivyo wewe utajisikiaje?
Nina mdogo wangu kapendana na Dada mmoja wa Arusha na ana mpango wa kumuoa.
Juzi mwezi uliopita katoa utangulizi kwa mzazi atarajie mgeni atakayekuja kutambulishwa.
Swali la kwanza lilikuwa, kabila gani?
Walipoambiwa anatoka Arusha mama akaanza kufoka na kutoa mifano ya watu waliooa huko na maisha yao yalivyo.
Mimi nilichojiuliza, mbona hata mtu mwenyewe hawamfahamu?
Mbona wameanza kumchukia mtu wasiyemuona?
Hivi ni nini huwa mnahofia?
Kwa kizazi cha sasa kumpata mtu unayehisi ni sahihi wa kabila lako ni suala ambalo limekuwa gumu kidogo, kwa nini bado wamama wanalazimisha?
Dogo aliwahi kupendana na binti wa kabila letu lakini alimtenda vibaya mpaka akapoteza mwelekeo. Naombeni mnifungue akili yangu.
Nina mdogo wangu kapendana na Dada mmoja wa Arusha na ana mpango wa kumuoa.
Juzi mwezi uliopita katoa utangulizi kwa mzazi atarajie mgeni atakayekuja kutambulishwa.
Swali la kwanza lilikuwa, kabila gani?
Walipoambiwa anatoka Arusha mama akaanza kufoka na kutoa mifano ya watu waliooa huko na maisha yao yalivyo.
Mimi nilichojiuliza, mbona hata mtu mwenyewe hawamfahamu?
Mbona wameanza kumchukia mtu wasiyemuona?
Hivi ni nini huwa mnahofia?
Kwa kizazi cha sasa kumpata mtu unayehisi ni sahihi wa kabila lako ni suala ambalo limekuwa gumu kidogo, kwa nini bado wamama wanalazimisha?
Dogo aliwahi kupendana na binti wa kabila letu lakini alimtenda vibaya mpaka akapoteza mwelekeo. Naombeni mnifungue akili yangu.