Jadda
JF-Expert Member
- May 20, 2019
- 31,548
- 88,539
Mkuu biblia inaelezea watu wawili tu ambao hawakufa walipaa mbinguni kama walivyo nao ni Nabii Henoko na Nabii Elia ukimtoa Yesu maana Yesu siyo mtu ila alikuja tu katika mwili wa mtu na alikufa halafu akafufuka na labda nikwambie tu kuwa binadamu anapokufa roho yake inatoka na hapo itaenda mbinguni au motoni kutokana na imani na matendo yakeWewe ni Mkristo ? Process ya mwili kutoka kwenye kaburi kwenda mbinguni mimi sijui wewe ndiye unayejua na ndio maana ukasema kinachoingia mbinguni ni roho sio mwili
Ndio nikataka kujua kwako Nabii Elijah aliyepaa na Farasi wa moto mbinguni aliingiaje kwa roho au mwili ?
Kwa wale ambao roho zao zitafanikiwa kuingia mbinguni wakifika kule wanapewa miili mipya ambayo haijawahi kutenda dhambi kwa sababu hii miili waliyoiacha duniani imetenda dhambi kwahiyo hapo tunaona kwamba sababu ya mwili kufa na Mungu kuchukua roho ni kwa sababu mwili unakuwa umeshatenda dhambi na mbinguni hakiingii kitu chenye dhambi
Hata kama ulikuwa mzinzi ukaja ukatubu ukasamehewa ule mwili haubadilishi ukweli kwamba ulishawahi kuzini kwahiyo mwili utakuwa ni mchafu japo roho yako inakuwa imesamahewa sasa sababu ya hao watu wawili kuchukuliwa kama walivyo ni kwa sababu miili yao haikuwahi kutenda dhambi na haikuwahi kuwa dhaifu
Ndo maana wanasemaga duniani hakuna binadamu mkamilifu ndo maana wote tunakufa kwahiyo ukisikia watu hawakufa bali walipaa mbinguni ujue hao walikuwa wakamilifu kwenye kila kitu kiasi kwamba Mungu hakuona sababu ya kuwapitisha kwenye kifo kwahiyo tunasema tangu dunia iumbwe hadi leo hii hakujawahi kutokea binadamu mkamilifu zaidi ya hao wawili tu wengine wote walikuwa na mapungufu sasa hizo ni sababu zilizoandikwa kwenye biblia ila Mungu ana siri nyingi sana na ana sababu zake nyingi sana ambazo hawezi kuruhusu binadamu tuzijue