Walipukiwa na mabomu wakitaka kulipua kanisa

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,886
155,869
Washambuliaji wawili wa kujitoa mhanga ambao walikuwa kwenye harakati za kutekeleza shambulizi la bomu katika kanisa moja kaskazini mashariki mwa Nigeria wameripotiwa kufa baada ya bomu waliokuwa nayo kulipuka kimakosa kabla ya kufika kwenye kanisa walililokuwa wakilenga.

Kwa mujibu wa ripoti za polisi, washambuliaji hao walikuwa watatu lakini mmoja akatoroka alipoona wenzake wamelipuliwa. Polisi wamesema kwamba washambuliaji hao walikuwa wakielekea katika kanisa la Seminari kwenye jimbo la Adamawa kutekeleza shambulizi hilo. Polisi wanashuku kwamba kundi la kigaidi la Boko Haram lilihusika kwenye tukio hilo.

Source:- China Xinhua News
 

Haleluya
 
Sasa sijui watapata bikra wote au watapunjwa maana hawajakamilisha mission.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…