Waliosoma Jitegemee Secondary School hebu ingieni hapa Tusalimiane

Hahaa, kwembe mzee wa madumu, alinibebesha dumu 46, kwa mara ya kwanza nikaona huruma ya alieka discpline master kpnd kile jina nimesahau jamaa flan alikua white ana mwili mkubwa kias na kiji mustach na manywele, akaniombea msamaha japo jana yake alituchania modo mpaka kwenye mapaja halaf akatuzungusha kantine mda wa lunch, we bwana weee, yan waliokua wamevaa boksa au pichu tu ni mambo nje nje, watu sio kucheka huko cantine yote hoi, orando nae akaja kunikamata kwenye vibweta mda wa darasan, My class teacher PCB Mgomba akanitetea, ndiamkama akanidaka sina pin tai, nikamuoshea kale ka suzuk kake ikaisha, nikadakwa na simu nikapostiwa getn pale kwa kumalija, kila afande anaekuja ni fimbo ni push up. Ile shule kwa kweli imenishepu sana mpake leo nipo panctual na shapu sana. Wapi p.didy, mkisi, tall, Malegesi, bruno, weng sana sana nimesahau majina.
huyo mwenye mustachi ni sir meja beiya,

;kuna siku kwembe anabebesha watu madum,halafu mkuu mwenyewe mwenye shule zake anakuja meja jenerali rafael muhuga anakuja msafara mkubwa anakuta watoto wanabebeshwa madumu,mkisi baadae akaja kumpa matusi hatare"wewe huna akili kichwa kikubwa km jiwe" unabebesha watt madum,akamtia tusi moja.....
hiyo ndo 7bu iliyomfanya kwembe kuhama jiteute.
 
....nakumbuka ilikuwa taabu kutoroka mchana,alikuwepo mshikaji babayake ni brigedia basi tulikuwa tunampigia simu dereva wa babayake anakuja mapema tunajaa kwenye gari,getini wakiona gari inatoka makao makuu ina nyota,wanafungua geti kiulaiiiniii,watu haoo uswazi....
Hahahah yani kama gazeti la SANI vile
 
Mtanganyika wa kweli, umenikumbusha, jamaa kweli alikua anaitwa beiya, io inshu ya kwembe naikumbuka sana ipo kama ulivyoielezea, umenikumbusha na nziku mzee wa misifa anachapa huku kashka fimbo na mikono miwili kuna siku alidindiwa na dogo wa 4m4 pale karbu na kwa secretary sikuamin Nziku alimhanya dogo wa 4m4.
 
Mtanganyika wa kweli, umenikumbusha, jamaa kweli alikua anaitwa beiya, io inshu ya kwembe naikumbuka sana ipo kama ulivyoielezea, umenikumbusha na nziku mzee wa misifa anachapa huku kashka fimbo na mikono miwili kuna siku alidindiwa na dogo wa 4m4 pale karbu na kwa secretary sikuamin Nziku alimhanya dogo wa 4m4.
yea yule dogo alimkazia na kuna mwamba mmoja wa hkl hv kamaliza duce hapo nziku alimvaa mwamba akamdindia.
sema wakat tulivyokutan chuo nziku wakat yy anafany masterz alikuwa mpole na mwana kinoma huwez jua ndo kam yule aliyekuwa anasumbua makuruta akikuta gari yak iko kweny jua halaf ww uko pemben yak hujaitoa.n.b funguo alikuwa anaicha t kweny gari.
 
Dah...shule nlizosoma mimi zote ungaunga mwana tu...nataman na mimi ningesoma shule za kueleweka kama hzo zenu....ila fresh maisha yanasonga!!
 
Jitegemee (2001 pre form one) 2002-2005. Headmaster F.Masawe, Afande Ismail, Wajadi, Bruno master, Mama Shalua, mzee Bwenge Afande Mkisi hahahahhh. Daaah those days. Kule canten mama Koku
 
Jiteute 2014 balaa kuingia getini na kutoka kwa wale wavaa modo nulikuwa naingia saa 10 alfajiri kabla afande alando wa afande K hawajafika. na ukiruka ukuta faini elf50 mwanangu salmini zedy kashalipishwa sana na mr. omary. mwanangu Samtonga tumeiba sana mabegi ya wanafunz wa form2 na calculator za form6 na kwenda kuziuza keko ila mwalimu wetu wa darasa katubeba sanaaaa madam kilewo pongezi kwake bhn ila mr. ng'wandu balaaaaaaa nilivyokuwa form3 alinyoosha si kitoto BIFU LA 2014 JITE NA AZANIA LILIKUWA GUMZOOO UWANJA WA MAPAMBANO KULE MCHIKICHINI
 
R.I.P mzee Ngamesha.

Kama nawaona vile wazee wa joro.

Mimi sikuwahi kukosa disco ukumbi wa mabatini hata Mara moja.

Watoto wa O'level full kuleta shobo kwa washkaji wa advance, tuliwatafuna sana.

Jite ute ni kama chuo asee, wanafunzi kama elfu tano si mchezo!
 
kwa wale wote tuliosoma jitegemee tukutane hapa tukumbushane enzi zetu za jiteute, bila kusahau lile hall letu kama sikosei liliitwa Sanga hall ambalo tulikutana shule nzima wanafunzi zaidi ya elfu 3, mwisho wa mwaka kwa ajili ya mchujo wa below 40 , nani aendelee nani abaki hapo wanafunzi wote roho zilikuwa juu juu

bila kumsahau mr Bwenge na ukatili wake,
Marehemu Mrimi kipenzi cha wanafunzi na mwandishi mahiri kabisa wa gazeti la shule enzi hizo
Daz Baba enzi hizo na wimbo wao wa kwanza kabisa wa Kamanda ulivyotikisa.

pia nimeukumbuka Mkungu tree na mambo mengine mengi ikiwemo kwatala welcome form one na welcome form 5

sijui kama jitegemee ya sasa hivi inalingana na ile ya Masawe kwaweli

ya kale ni dhahabu jamani japo haiwezi kujirudi tena ila tunaweza kukumbushiana tu
 
Back
Top Bottom