Waliosimamishwa UONGOZI na MBOWE, wahamia CCM

Waliosimamishwa UONGOZI na MBOWE, wahamia CCM

ambao waliamua kuhamia CCM wakifuatwa na wafuasi wao kutoka katika chama hicho.
kiswahili kumbe kigumu sana, aise, kweli hili ni gazet mfu lol,
 
Source...Uhuru...The Toilet Paper
Ukiisha kula chakula na kushiba na kubanwa haja kubwa utakwenda chooni( faragha) ukishajisaidia( waste products) Naomba usikate toilet paper uvae sarawili yako uende kwa marafiki zako uone utakavyo fuatwa na NZI. Katika vitu muhimu katka nyumba huwezi kukidharau choo na viambata vyake(maji, sabuni, tissues(TP). Toilet papers are very vital in every day life.
 
Katika tukio lingine la hivi karibuni lenye kudhihirisha kasi ya CCM kuibomoa CHADEMA, Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Tarime, kimevuna wanachama wapya 800 ambao awali walikuwa ni wanachama na wafuasi wa CHADEMA.

Wanachama hao ambao idadi yao imetimia takriban 800 wamekuwa wakiingia CCM kwa muda wa wiki tatu mfululizo tangu kumalizika kwa ziara ya Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA katika wilaya ya Tarime, ambapo wanachama zaidi ya 600 walijiunga wiki mbili zilizopita na 256 walijiunga na CCM jumanne iliyopita katika mikutano ya hadhara.

Mikutano hiyo ya hadhara ambayo inaendelea wilayani humo, jumanne ya juzi ilifanyika katika uwanja wa kituo cha Sirari, ukihutubiwa na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Rashid Bogomba, ulihudhuriwa na mamia ya wakazi wa eneo hilo na katika mkutano huo ndipo wanachama wengine 256 waliporudisha kadi za chadema na kujiunga na CCM na kutimiza idadi ya wanachama hao wapya kutoka chadema kutimia zaidi ya 800.

Wanachama hao wamedaiwa kuhamia CCM baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa , Freeman Mbowe kuwasimamisha uongozi viongozi wa CHADEMA wa wilaya hiyo ya tarime, ambao waliamua kuhamia CCM wakifuatwa na wafuasi wao kutoka katika chama hicho.

Source: Uhuru_ukurasa wa 8

Ama kweli na wewe ni gwiji la wajinga,kichwa cha habari waliotimliwa chadema wahamia ccm!ni kamati ipi ya chadema ina wajumbe 800?sirali unayosema ilkuwa na mamia ya watu ni ipi?na viongozi hao ni akina nani?kama tarime mjini mlikuwa na watu 80 na watu 50 walikuwa wanachadema je hayo ndio mahudhurio mazuri ya chama kinachotawala?mwenykit wa halmashauri aliulizwa swari na mwananchi ataje kanuni ya 8 kifungu kidogo cha kwanza na cha pili katka kitabu cha kanuni za halmashauri kinahusu nini akashindwa kujibu,nafkiri una ganzi kichwani na wana ccm wenzako,
 
Di lazima chama kuwa na watu wengi wasio na moyo aw kimapinduzi, ni vizuri kuwa na reasonable and committed number of members ili wakati aw uchaguzi wawashawishi watu wengine kupiga kura zilizoanguka maamuzi. Hebu hao waliorudi CCM waende kwani mioyo Yao si ya kimapinduzi kabisa kabisa.
 
Hakuna kitu kama hicho ukweli ni kwamba huyu Mp nyambari magamba yuko most wanted kufika baadhi ya sehemu kubwa ya Tarime manake moja ya ahadi zake alisema ataruhusu watu wachunge ndani ya hifadhi ya serengeti! (kichekesho wakuria wakaamini) ikawa ndivyo sivyo baada ya kupita kwa kuchakachua hajawahi kanyaga tena. Wananchi waliahidi watamkata mapanga huku watu wanachukia magamba mno. Acheni kuaminisha watu uongo
 
Source ni gazeti la uharo? Haliaminiki. Matumizi ya maana ni kupangusa shyt.
 
Hivi hilo gazeti la uhuru huwa linaishia wapi.?

Nina zaidi ya miaka sita sijalisoma hapa Tunduma.!!
 
Kama mnatengeneza video za ugaidi iweje mshindwe kutengeneza kadi za chama fulani?tena source eti UHURU...asante.
 
Kama taarifa hii ni ya kweli basi mpaka kufikia 2015 Chadema wanaweza wasiwe na kiti cha Ubunge hata kimoja. Haiwezekani kila kukicha tupate taarifa za watu kukihama chama hiko na kisha tuendelee kujipa imani kuwa kipo salama na kitavuka bahari pamoja na mawimbi haya mazito ambayo chombo chao kimeshaonyesha udhaifu wa kuyakabili.
Rekebisha - watakuwa hawana mwanachama ! Sijui kama hii propoganda ina maana youote- ofcourse kuna kipindi CHADEMA waliitumia wakionyesha wanachama wa CCM kwa wingi wakiamia kwenye chama hao!
 
Sikuhizi gazeti la uhuru linauziwa chiniya meza nalinapatikana Dar na Dodoma tu,linafichwa kama bangi!
 
katika tukio lingine la hivi karibuni lenye kudhihirisha kasi ya ccm kuibomoa chadema, chama cha mapinduzi (ccm) wilayani tarime, kimevuna wanachama wapya 800 ambao awali walikuwa ni wanachama na wafuasi wa chadema.

Wanachama hao ambao idadi yao imetimia takriban 800 wamekuwa wakiingia ccm kwa muda wa wiki tatu mfululizo tangu kumalizika kwa ziara ya mwenyekiti wa taifa wa chadema katika wilaya ya tarime, ambapo wanachama zaidi ya 600 walijiunga wiki mbili zilizopita na 256 walijiunga na ccm jumanne iliyopita katika mikutano ya hadhara.

Mikutano hiyo ya hadhara ambayo inaendelea wilayani humo, jumanne ya juzi ilifanyika katika uwanja wa kituo cha sirari, ukihutubiwa na mwenyekiti wa ccm wa wilaya hiyo, rashid bogomba, ulihudhuriwa na mamia ya wakazi wa eneo hilo na katika mkutano huo ndipo wanachama wengine 256 waliporudisha kadi za chadema na kujiunga na ccm na kutimiza idadi ya wanachama hao wapya kutoka chadema kutimia zaidi ya 800.

Wanachama hao wamedaiwa kuhamia ccm baada ya mwenyekiti wa chadema taifa , freeman mbowe kuwasimamisha uongozi viongozi wa chadema wa wilaya hiyo ya tarime, ambao waliamua kuhamia ccm wakifuatwa na wafuasi wao kutoka katika chama hicho.

source: Uhuru_ukurasa wa 8


View attachment 89798View attachment 89798

ccm sisi wenyewe kwa wenyewe tunaaibishana mimi mwenyewe nilikuwa mhutubiaji na kwa kweli tumuogope mungu mkutano ule ulitupa shida maana haukuwa na watu hata mia 2 sasa tunaposema watu mia nane walihama tunasababisha hata wale wanaotuamini japo kidogo wanatudharau zaidi mwandishi nyoka usiwe unakurupuka kuandika bila kutuuliza unaaibisha chama na gazeti ;letu unasababisha hata wale wanaotuamini wanatudharau zaidi unaweza kuwadanganya wengine dar na kwingineko lakini kwa wale waliokuwa kwenye mkutano watatuelewaje? Haya mambo ya kutetea hata ujinga yanaangamiza chama kusema uongo sio kusaidia chama jamani
 
Back
Top Bottom