Isalia
JF-Expert Member
- Nov 3, 2011
- 1,211
- 435
Wanahamia kimwili wakishajazwa mapesa,lakini mioyoni bado wako CHADEMA.
endelea kujidanganya uko sasa binaadam kujipa moyo ndio vizuri
Wanahamia kimwili wakishajazwa mapesa,lakini mioyoni bado wako CHADEMA.
Katika tukio lingine la hivi karibuni lenye kudhihirisha kasi ya CCM kuibomoa CHADEMA, Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Tarime, kimevuna wanachama wapya 800 ambao awali walikuwa ni wanachama na wafuasi wa CHADEMA.
Wanachama hao ambao idadi yao imetimia takriban 800 wamekuwa wakiingia CCM kwa muda wa wiki tatu mfululizo tangu kumalizika kwa ziara ya Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA katika wilaya ya Tarime, ambapo wanachama zaidi ya 600 walijiunga wiki mbili zilizopita na 256 walijiunga na CCM jumanne iliyopita katika mikutano ya hadhara.
Mikutano hiyo ya hadhara ambayo inaendelea wilayani humo, jumanne ya juzi ilifanyika katika uwanja wa kituo cha Sirari, ukihutubiwa na Mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo, Rashid Bogomba, ulihudhuriwa na mamia ya wakazi wa eneo hilo na katika mkutano huo ndipo wanachama wengine 256 waliporudisha kadi za chadema na kujiunga na CCM na kutimiza idadi ya wanachama hao wapya kutoka chadema kutimia zaidi ya 800.
Wanachama hao wamedaiwa kuhamia CCM baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa , Freeman Mbowe kuwasimamisha uongozi viongozi wa CHADEMA wa wilaya hiyo ya tarime, ambao waliamua kuhamia CCM wakifuatwa na wafuasi wao kutoka katika chama hicho.
Source: Uhuru_ukurasa wa 8
hawa jamaa wanaohama vyama hawafai kuwa viongozi maana wanatakiwa wapambane na matatizo na sio kuyakimbia hayo matatizo.hawa ndo sometimes wanakimbia familia kwa kwenda kutafuta maisha mteremko
Ndugu yangu naomba unisadie mwenyewe ukianza kwa kuunganisha hapo kwenye RED na BLUE! Hivi hapo WAMEVUNA au WAMEOKOTA?Katika tukio lingine la hivi karibuni lenye kudhihirisha kasi ya CCM kuibomoa CHADEMA, Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Tarime, kimevuna wanachama wapya 800 ambao awali walikuwa ni wanachama na wafuasi wa CHADEMA.
Wanachama hao wamedaiwa kuhamia CCM baada ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa , Freeman Mbowe kuwasimamisha uongozi viongozi wa CHADEMA wa wilaya hiyo ya tarime, ambao waliamua kuhamia CCM wakifuatwa na wafuasi wao kutoka katika chama hicho.
Source: Uhuru_ukurasa wa 8
Virusi vyote vikiondoka ni heri, ili ibaki cream!
Kuna watu hawaamini kitu ambacho hakijaandikwa na Tanzania Daima...
Nimesema kuwa heri waondoke wote tubaki na watu makini wanaomaanisha kuleta ukombozi wa wanyonge!Hawa unawaita virusi ndo waliokua kikijaza mikutano yenu!!
Kama taarifa hii ni ya kweli basi mpaka kufikia 2015 Chadema wanaweza wasiwe na kiti cha Ubunge hata kimoja. Haiwezekani kila kukicha tupate taarifa za watu kukihama chama hiko na kisha tuendelee kujipa imani kuwa kipo salama na kitavuka bahari pamoja na mawimbi haya mazito ambayo chombo chao kimeshaonyesha udhaifu wa kuyakabili.
Kama una mtu anafanya serikalini muulize maana govt ndio reliable market kwa gazeti hilo la chama tawala.Source of information, uhuru news peper;
ipo kazi hapo!!!
Hivi uhuru inatoka siku gani vile kwa wiki, na linauzwa bei gani vile?
Tukio na hatimaye Kifo cha Chacha Wangwe ndi unataka uthibitishio huo?Tunaomba uthibitisho wa uhakika sio unasema tu wanachama 800 onyesha picha, hasa wakati wanarudisha kama ambavyo CHADEMA ilifanya kuleee LOLIONDO