Waliofeli Form Four kurudia mitihani bure mwaka huu?

Waliofeli Form Four kurudia mitihani bure mwaka huu?

hilo wazo la naibu waziri halitatoa ufumbuzi wa tatizo la elimu tanzania,kufeli kwa hao wanafunzi hakuku sababishwa na mitihani migumu sababu kubwa ni uwezo wa wanafunzi wenyewe, kuna shule moja jirani ya kata ambayo imetoa div 3 wawili 4 kumi na mbili wengine 80 hivi zero.ukifuatilia sana wengi wao hawakustahili wafike kidato cha nne kabisaa kwani shule hiyo hiyo kwenye qt ya form two zaidi ya wanafunzi 80 wame fail kuingia kid cha 3 ni 20 tu walifaulu.hii inaonyesha kiwango cha elimu kimeshuka sana tz.kuna kijana wetu alifeli form 4 tukaingia gharama nyingi kurudia form four tena bwenini yalipotoka matokeo yalikuwa mabaya kuliko yale ya kwanza. Tunahitaji mabadiliko makubwa kwenye mfumo wa elimu tanzania.
 
Ndo wapo kwny mikaki hyo kwa xaxa na amesema wanaangalia jins ya kuwalipia ada.
 
Hata wakirudia tatizo sio kwamba mtihani ulikuwa mgumu. Mfumo wa elimu ni mbovu, wanachukua wanafunzi vilaza toka s/m, walimu hakuna. Miaka minne mwanafunzi ameshindwa kupata hata D moja, kwa mwaka mmoja atawezaje?.
 
Izo gharama cwawalipe watu wa chuo watusaishie mitihani yetu tena kwa kipind hiki make wanachuo wako wengi sana na wanauwezo wa kusaisha mitihan hiyo.
 
Naibu Waziri wa Elimu Philipo Mulugo alipozungumza na gazeti la HabariLeo kuhusiana hatua zitakazochukuliwa na serikali kutokana na idadi kubwa ya watahiniwa wa kidato cha nne kupata sifuri, amedai kuwa serikali inafikiria warudie mtihani mwaka huu.

Amesema serikali inaangalia namna ya kuwalipia ada ya mtihani ambayo mwaka jana walilipa Sh 35,000 kila mwanafunzi. Likipita hilo la kurudia mtihani, serikali italipia ada hiyo na wataufanya kama watahiniwa binafsi.

Ingawa alisema wazo hilo halijapitishwa, lakini hivi sasa linajadiliwa kuona namna ya kuwasaidia watahiniwa zaidi ya 240,000 kurudia mtihani wa Taifa kwa gharama za serikali.

Kuhusu idadi ya watakaoingia kidato cha tano mwaka huu alisema, matokeo hayatarekebishwa kwa namna yoyote, ili kuongeza idadi ya watakaoingia kidato cha tano mwaka huu, bali watahiniwa 23,500 waliopata daraja la kwanza hadi la tatu ndio watakaoendelea. Alisema watakaochukuliwa Ualimu ni wa daraja la nne ya alama 26 na 27 huku wenye alama 28 wakiachwa bila kuchukuliwa mwaka huu.


Source: Habari Leo

N.B: Kwa mahesabu ya haraka haraka kama serikali itaamua kuwalipia wanafunzi zaidi ya 240,000 waliofeli kurudia mitihani itagarimu sio chini ya Sh. 8,400,000,000.

Kwa jinsi ninavyoifahamu serikali yetu ya Kitanzsnia na kwa ambavyo haijui kujali maslahi ya Watanzania, sidhani kama inaweza kufikuria kitu cha namna hii.

Serikali hii inajali sana kumwona best anabaki akivuna,mshikaji anabakia akitesa, mtoto wa dada hapotei kwenye ramani na mengine mengi. Ukiangalia upande wa mambo ambayo ni ya msingi kwa Taifa na faida ya wananchi wote kwa ujumla haina muda wa kuyafuatilia na kwa hakika si kipaumbele cha serikali hii.

Huu wimbo hunekomaa masikioni mwao na hauleti ukakasi wala mshawasho wowote ndani ya vichwa vyao walio na mashangingi. Wanachojali sasa ni maandalizi ya uchaguzi wa 2015 na kuhakikisha mkate wao hauguswi. Kwa nifahamuvyo hakika, Kawambwa asingesalia na hata Ndalichako hapo alipo maana reaction ya wananchi inatosha kutoa dira kuwa nini zuri au baya umefanya kama kiongozi.

ILA KWA AKILI YANGU TUMEWACHOKA NA WAMETUCHOSHA SAANA
 
Hakuna haja ya mtihani kurudiwa wakati wanafunzi hawajiwezi
 
Mkuu@Zinedine umenena la maana kwa serikali yetu" tatizo viongozi wetu hawasikilizi maoni ya Wananchi! Kazi kutafuta Cv za akina Mnyika!! Candidate anapata IV27,ana F ya B/mathe na F,Biology ana D ya kiswahili! English nayo ni janga kwenye shule hizi za serkali!! Alafu huyo ndo awe mwalimu wa primary!
 
hizo hela wangepeleka kuboresha maabara na kununua vitabu!

Afterall hizo fedha siyo za Serikali...ni fedha zetu...sisi wananchi...ni kodi zetu...

Ni lini hawa watu wataelewa hivyo?! kwa yeye kusema kwamba wazazi/walezi hawatalipa 35,000 instead serikali italipa anafikiri/wanafikiri wanapunguza hasira za wananchi.


Zaidi ya yote, hata hiyo michango ya 35,000 kama gharama za mitihani hazikupaswa kuwepo in the first place, since we do pay taxes... for christ sake
 
Kwani imetangazwa?

Clouds fm kupitia kipindi cha power breakfast on saturday kimemnukuu waziri wa elimu kuthibitisha kuwa waliopata div 0 serikali itawalipia ada ya mtihan. Mi naona serikal hii imejitoa akili, sasa haioni tena kilichosababisha hii massive failure, maamuzi yao ya kukurupuka ndio yalotufikisha hapa, mf kutoa mitihan ya f2 na drs 4. Pia kutoa adhabu za viboko mashulen, kudharau walimu ni baadhi tu ya visababishi. Wabongo ni wepes sana wa kurubuniwa kwa vitu vidogo, eti serikal itagharimia? Shame on you. Hela yote hiyo mmeitoa wap? Km ilikuwepo, kwa nn hamkuitoa mapema kuboresha mazingira ya kujifunzia? Watoto wanamaliza mwaka mzima bila kuona mwal wa somo hasa ya science! Halafu leo hii hawajui tatzo, kwel? Nakumbuka JK mwaka 2010 akiongea na wazee wa Dar alitoa povu jingi huku akishangiliwa sana akitishia walimu et hawezi ongeza salary kisa gvt haina pesa! Ona sasa aibu uliyoipa nchi ye2! Hata shule yenye jina zuri JKM Kikwete nayo matokeo yake nayo aibu tupu. Cha msingi hapa serikal ituombe radhi watz wote kwa mipango mibovu namna hii, tunajenga taifa gan hili lisilokuwa na afya! Hawa watoto kama si wote, robo 3 yao kilimo tena hawawezi watakuwa wakurubuniwa tu, hapa ndo majambaz, vyangudoa,n.k watapatikana humu. Wazazi,walezi na wadau wengine tuamke kubain hila hz la sivyo vijana wetu wataangamia kwa kuwa watoto wa wakubwa hawa wanauhakika wa milo mitatu na vitu vingine maisha yao yote.
 
Tanzania inaangamia. Tanzania inaangamia ninarudia tena. Miwaziri yenyewe hiyo kazi kuiba tuuuu! Eti waliofeli ndiyo wakafundishe yaani hamuoni hiyo cycle? Jamani angalieni Kenya, Uganda, sisi tunajipaka matope tuu hata raisi mwenyewe hovyooooo! Serikali Hovyoooooo! Elimu Hovyooooo! Mahospitali Hovyoo! Mabarabara hakuna kitu. Ni lini tutajitazama tuone aibu? Raisi ni yeye na pipa na kwenda kuburutwa na farasi Canada. Jamani hivi anaenda amefunga macho au? Acheni ubinafsi fundisheni watoto wote Kiingereza tangu kindergarten. Tunaumia, tunateseka, tunaibiwa, tunanyanyaswa na viongozi tuliowaweka madarakani. Tutafika siku tutawapiga mapanga. Tumechoka kwa kweli!
 
Kweli hii ni serekali legelege


Au wanampango wakuwapa mtihani na majibu yake ili wajisafishe.


Halfu hao mawaziri cjui wana mioyo gani,hawaoni hata aibu,,why wasiwajibike.
 
Kiukweli uwezo mkubwa wa Dr. Shukuru Kawambwa unafahamika wazi kwa mafanukio makubwa aliyoyapata kila wizara aliyoshika, ndipo JK akaona amlete Elimu ili yale makubwa aliyoyafanya huko kwingine, apeleke kwenye Elimu!, Mhe. Mulugo ndiye naibu wake!, unategemea nini?!.Kiukweli kuna baadhi ya mengine yanayotukuta ni ya kujitakia!.P.
 
Nchi moja, Wizara moja sera tofauti- Vyuo vikuu, wanaopata 1st class ndiwo mara nyingi wanaopata nafasi ya kuwa ma-TA, Sekondari wanaofeli ndo wanaenda kuwafundisha wenzao; kwanini wasifeli watakaofundishwa. Ukweli ni kwamba mtoto wa Form Four anaepata Division 4, huyu aidha hajafundishwa au hana uwezo, hivyo hawezi kufundisha watu-Huu ni ujinga toka kwa NW, hwcome aje statement ya ajabu namna hii. Wekeni u, kwa sasa hakuna homa ya. SUALA LA LUGHA YA KUFUNDISHIA PIA TATIZO KUBWA.
 
Kuna habari mtaani kuwa waliofeli wanarudia mtihani, sasa swali wamehakikishiwa kufaulu, na wamerekebisha lini makosa yaliyowafanya wafeli? Kawambwa alisikika akitamba kilichowafelisha vijana ni kuthibiti mitihani isivuje je sasa watavujisha ili wafaulu? Ni lini tutashughulikia miziz ya tatizo la elimu maana tumeshughulikia matawi kwa muda mrefu sasa!
 
kwa akili nangu niliyo pewa na mwenyezi mungu natumaini kama nikweli waziri ametoa statement yaaina hiyo, basi amenifanya niamini kuwa TANZANIA tutaendelea kuwa wajinga namba 1 katika dunia ya sasa.mimi ni mmoja kati ya watumishi kwenye idara hii ya elimu, hivi kweli hao wanafunzi laki 240,000 anaotaka warudie mtihani kwanza nikweli serikali inao uwezo wa kugharamia zoezi hilo la urudiwaji wa mitihani ikiwa kuwalipa tu waalimu walio sahihisha mitihani hiyo ilikuwa ni tabu je sasa hivi wataweza ikiwa wanao tarajiwa kufanya mtihani mwaka huu nizaidi ya waliofanya mwaka jana?pili, tujiulize, je kuna vyumba vya kutosha vya madarasa katika shule zetu kufanikisha zoezi zima la kuufanya mtihani huo ikiwa tu mwaka jana ilibidi baadhi ya wanafunzi wa changanye katika madarsa yao yaani form two una mweaka na form three au form one una wawka na form two nakusababisha uvunjikaji wa vipindi kwa wiki hizo mbili za ufanyaji wa mitihani kwa wanafunzi waliokuwepo shuleni je hawa wanaorudi na wanao kwenda kuufanya huo mtihani utaratibu utakuwaje?tatu, kutokana na wingi wa wanafunzi waliofanya mtihani mwaka jana nguvu kubwa ilitumika kwa waalimu wengi kwenda kusimamia mitihani hiyo, hivyo kufanya ufundishaji wa vipindi katika shule husika kuzorota, sasa ikiwa kuna wanafunzi walioko shuleni hivi sasa walio jihandikisha na wana tarajia kufanya mtihani idadi inaonekana kuzidi ya hawa wa mwaka jana, ukiongeza nahawa anaotaka warudie mitihani anatuhakikishia vipi kuwa ano waalimu wakutosha kusimamia idadi kadiliwa ya 650,000 watakaofanya mtihani nchi nzima? na je kwa kipindi hicho cha mitihani nani ataendelea kufundisha huko mashuleni?nne, hivi kurudia mtihani ndo kutatua tatizo la kufeli kwa wana funzi? lakini pia gharama hizo zinazoenda kugharamia mitihani hiyo zinatoka mfuko upi? alisema kukosekana kwa maabara ndo kumesababisha wanafunzi walio wengi kufeli, sasa wataenda kufanyaje mtihani kwa mara yapili alafu wafaulu sasa hivi ikiwa hizo maabara hazija jengwa? au wata zijenga kwa haraka ili hawa watu wanao rudia na watakao fanya mtihani wafaulu kwa wingi zaidi?ninayo maswali mengi sana ya kumuuliza mh shimiwa wa ziri, ila cha kuku saidia nikuwa Elimu ya tanzania ina poromoka kwa sababu moja kuu TUNACHANGANYA SIASA UCHWARA NA MAMBO YA TAALUMA. wadau wa kuu waelimu ni watu wa nne, kwanza ni mzazi wa mwanafunzi, pili ni mwanafunzi mwenyewe, tatu ni Mwalimu, na nne ni Serikali yenyewe. kwapamoja kila mdau anayo mapungufu yake makubwa sana kama waziri kaaachini ni watu kwenye wizara yako na wadau hao hapo tajwa mja dili kwa kina njia ya kutatua tatizo na si kukurupuka kama watu tusio na version, Tufikiri kabla ya kutoa matamko ya siyo na tija.
 
kwa akili nangu niliyo pewa na mwenyezi mungu natumaini kama nikweli waziri ametoa statement yaaina hiyo, basi amenifanya niamini kuwa TANZANIA tutaendelea kuwa wajinga namba 1 katika dunia ya sasa.mimi ni mmoja kati ya watumishi kwenye idara hii ya elimu, hivi kweli hao wanafunzi laki 240,000 anaotaka warudie mtihani kwanza nikweli serikali inao uwezo wa kugharamia zoezi hilo la urudiwaji wa mitihani ikiwa kuwalipa tu waalimu walio sahihisha mitihani hiyo ilikuwa ni tabu je sasa hivi wataweza ikiwa wanao tarajiwa kufanya mtihani mwaka huu nizaidi ya waliofanya mwaka jana?pili, tujiulize, je kuna vyumba vya kutosha vya madarasa katika shule zetu kufanikisha zoezi zima la kuufanya mtihani huo ikiwa tu mwaka jana ilibidi baadhi ya wanafunzi wa changanye katika madarsa yao yaani form two una mweaka na form three au form one una wawka na form two nakusababisha uvunjikaji wa vipindi kwa wiki hizo mbili za ufanyaji wa mitihani kwa wanafunzi waliokuwepo shuleni je hawa wanaorudi na wanao kwenda kuufanya huo mtihani utaratibu utakuwaje?tatu, kutokana na wingi wa wanafunzi waliofanya mtihani mwaka jana nguvu kubwa ilitumika kwa waalimu wengi kwenda kusimamia mitihani hiyo, hivyo kufanya ufundishaji wa vipindi katika shule husika kuzorota, sasa ikiwa kuna wanafunzi walioko shuleni hivi sasa walio jihandikisha na wana tarajia kufanya mtihani idadi inaonekana kuzidi ya hawa wa mwaka jana, ukiongeza nahawa anaotaka warudie mitihani anatuhakikishia vipi kuwa ano waalimu wakutosha kusimamia idadi kadiliwa ya 650,000 watakaofanya mtihani nchi nzima? na je kwa kipindi hicho cha mitihani nani ataendelea kufundisha huko mashuleni?nne, hivi kurudia mtihani ndo kutatua tatizo la kufeli kwa wana funzi? lakini pia gharama hizo zinazoenda kugharamia mitihani hiyo zinatoka mfuko upi? alisema kukosekana kwa maabara ndo kumesababisha wanafunzi walio wengi kufeli, sasa wataenda kufanyaje mtihani kwa mara yapili alafu wafaulu sasa hivi ikiwa hizo maabara hazija jengwa? au wata zijenga kwa haraka ili hawa watu wanao rudia na watakao fanya mtihani wafaulu kwa wingi zaidi?ninayo maswali mengi sana ya kumuuliza mh shimiwa wa ziri, ila cha kuku saidia nikuwa Elimu ya tanzania ina poromoka kwa sababu moja kuu TUNACHANGANYA SIASA UCHWARA NA MAMBO YA TAALUMA. wadau wa kuu waelimu ni watu wa nne, kwanza ni mzazi wa mwanafunzi, pili ni mwanafunzi mwenyewe, tatu ni Mwalimu, na nne ni Serikali yenyewe. kwapamoja kila mdau anayo mapungufu yake makubwa sana kama waziri kaaachini ni watu kwenye wizara yako na wadau hao hapo tajwa mja dili kwa kina njia ya kutatua tatizo na si kukurupuka kama watu tusio na version, Tufikiri kabla ya kutoa matamko ya siyo na tija.
 
Back
Top Bottom