Waliofeli Form Four kurudia mitihani bure mwaka huu?

Waliofeli Form Four kurudia mitihani bure mwaka huu?

.
Kuna kitu hapa Serikali & Watanzania kwa ujumla hamtaki kukubali ukweli ...

Hao wanafunzi hata wakirudia mitihani yao WATAFELI tena! ...

Asilimia kubwa ni mbumbumbu na hawajaelimika & hata IQ zao zipo chini, hata ufahamu tu wa general knowledge nao upo chini

Tatizo ni kubwa kuliko mnavyofikiria
.

Kitakachofanyika ni kwamba hata wakifeli, bado wanaza kupewa alama za juu ili kujaribu kuepukana na hii kashfa.

Utashangaa na roho yako waliopata sifuri wakatengeneza misonge from no where ndani ya miezi kadhaa.
 
Kwani tatizo ni kufanya mtiahani ama kutokuwa na knowledge inayotakiwa. Tunaomba serikali isipoteze gharama kubwa kutatua matatizo yasiyo ya msingi, matatizo ya masingi yaliyopelekea wanafunzi kufeli mengi yanajulikana. Wajitahidi kuweka motosha wa kutosha na kuwalipa walimu stahiki zao kwa wakati ili wengi wenye uwezo wakatumikie uwalimu. Pia wajitahidi kuboresha vifaa vya kufundishia pamoja na ku-train walimu wazuri wengi wenye sifa zinazohitajika. Nasikitika kuona eti hili ndiyo suluhisho la serikali yetu tukufu.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Kwahiyo sababu ya kufeli ni kwamba watoto wetu hawakujiandaa au hawakuandaliwa? Na sababu ya kurudia mtihani tena ni kutoa fursa kwa watoto wetu kujiandaa, kuandaliwa, au kujaribu tena bahati zao? Nina wasiwasi mkubwa kwamba vyombo husika vinaweza kuligeuza suala hili likae kisiasa zaidi na watoto wetu wakirudia mitihani, wengi watapasishwa hata kama hawana uwezo ili mradi tu takwimu husika ziwe mtaji wa kisiasa/political asset, na kuondokana na hali ya sasa ambapo matokeo husika ni a political liability;

Hivi Tutafika kweli?

Mchambuzi,

Binafsi naamini ni sisi wazazi na uongozi wa kisiasa tunawajibika na kufeli huku kukubwa (massive failure). Kama taifa siamini tumefanya yote kuboresha elimu na kuwapa watoto wetu nafasi ya kufanikiwa. Ni kama tumeamua kuwahukumu kwenye fate ambayo sisi wenyewe tumeitengeneza. Huwezi kuwa na asilimia zaidi ya 90 ya watoto wanafeli.

Lakini jingine ambalo sijui ni mawazo ya nani; tunaendelea kupeleka wanafunzi waliopata daraja la nne kwewnye ualimu tukitumaini kuwa wataenda kutoa watoto wa daraja la kwanza! Hii si haki kwa watoto wetu. Matokeo ya mwaka huu hata hivyo tukumbuke yameungamanika na mambo mengine mengi tu (mgomo wa walimu, harakati za kisiasa, burudani zisizokoma, miundombinu hafifu n.k).

Nakuhakikishia hawa watoto wana uwezo wa kupata daraja la kwanza na la pili wote kama tunataka wafanye hivyo. Mimi ninaamini akili ya mwanadamu ina uwezo wa kutosha kuweza kujifunza endapo itapatiwa structures nzuri za kufanya hivyo. Sasa hivi tumetokea kukubali tu ubovu kuwa ni kawaida kiasi kwamba hatufikirii kusahihisha.

Suala la kurudia mitihani siamini kama linapaswa kuwa "watarudia mitihani" halafu tusubiri mtihani. La hasha. Ninaamini pamoja na kuwapa nafasi ya kurudia mitihani ni muhimu kuwapa nafasi ya kujiandaa vyema na mithiani hiyo. Hii ni pamoja na kuhamasisha shule na walimu kuwapa mafunzo ya karibu mwaka mzima kuweza kuupgrade.. a vigorous preparation. Na hapa na wazazi washiriki. Sijui tutaweza kufanya vipi but we have to do it.

Ni hatari sana kwa taifa kuwa na watoto wasioelimika wanaongezeka mitaani. NI kosa letu sisi wazazi na viongozi - siwalaumu watoto hawa kabisa.
 
Kwanini inakuwa ni rahisi kuingia hasara kwa kulipia marudio ya mtihani lakini inakuwa ni ngumu wao kujiuzulu,au kwasababu hizo hela hazitoki mfukoni kwao? waache mchezo wa kuigiza.......hembu watuambie hao wanafunzi wakifeli tena baada ya kurudia mtihani nini kitafuata......Serikali imejaa wasanii kila kona na wananchi ni kama tumezoea kuongozwa kisanii, Mungu asaidie hili TAIFA.
watakao feli watarudia tena mpaka matokeo yawe mazuri. Hii itafanyika ili mheshimiwa asijiuzuru.
 
Ikiwa ni pamoja hao wazazi kuwalipia gharama zote za kurudia?

absolutely... wazazi walipie gharama za kurudia, tuition n.k. serikali itoe hata hivyo vitu viwili.

Mitaala ya mambo ya lazima mwanafunzi wa Form Four ayajue - kama hakuna mitaala watoto wanajifunza vipi nchi nzima? Lakini la pili ni kutoa nafasi kwa watu ambao wako kwenye ajira mbalimbali na ambao ni wataalamu katika masomo yao kurudi na kujitolea (volunteer) kuwaandaa watoto hawa kwamitihani.
 
Hii hatari,mtu mwenye div 4 anakwenda kusomea ualimu?sasa nimeelewa ziro zinapotokea!
 
absolutely... wazazi walipie gharama za kurudia, tuition n.k. serikali itoe hata hivyo vitu viwili.

Mitaala ya mambo ya lazima mwanafunzi wa Form Four ayajue - kama hakuna mitaala watoto wanajifunza vipi nchi nzima? Lakini la pili ni kutoa nafasi kwa watu ambao wako kwenye ajira mbalimbali na ambao ni wataalamu katika masomo yao kurudi na kujitolea (volunteer) kuwaandaa watoto hawa kwamitihani.

Lakini serikali inadai kuwa kama hilo suala la kurudia likipita basi itagharimia wale wote waliopata sifuri.

Kwa maana nyingine wazazi hawatalipa chochote kwa maana ya kulipa sh. 35,000 za kurudia.

Kwa muda uliobakia kweli unategemea hao watoto warudie mitihani na kufaulu kwa alama zinazotakiwa?

Pia kwa nini waliopata sifuri tuu ndiyo waruhusiwe kurudia bure? Vipi waliopata four? Kwani kiuhalisia hao wamefaulu?

Hata mtoto aliyepata division three si anaweza kudai kuwa hii siyo fair kwa sababu kama asingesoma kwenye hayo mazingira mabaya angepata division one?

Huoni kama serikali inataka kuwagawa hawa watoto na wazazi wao kwenye matabaka?
 
Kwahiyo sababu ya kufeli ni kwamba watoto wetu hawakujiandaa au hawakuandaliwa? Na sababu ya kurudia mtihani tena ni kutoa fursa kwa watoto wetu kujiandaa, kuandaliwa, au kujaribu tena bahati zao? Nina wasiwasi mkubwa kwamba vyombo husika vinaweza kuligeuza suala hili likae kisiasa zaidi na watoto wetu wakirudia mitihani, wengi watapasishwa hata kama hawana uwezo ili mradi tu takwimu husika ziwe mtaji wa kisiasa/political asset, na kuondokana na hali ya sasa ambapo matokeo husika ni a political liability;

Hivi Tutafika kweli?

Mchambazi wazo hilo la Wizara sio baya, ngoja vijana wajaribu bahati yao kwa mara ya pili, maana hali ni mbaya
 
Kama ni kusaidiwa kurudia hata waliopata div 4 wanahaki hiyo. lakini ni vema suala hili likawekwa pembeni wazazi ndio waamue wafanye nini. na je, kurudia kutaambatana na maandalzi gani na wapi? je, watarudi shule au watasoma mitaani? je, kama ni mitaani nani atawasaidia na kama ni shule walimu wataweza kubeba mzigo huo? Jambo hili haliwezekani.
 
Mtoto aliye shindwa kufaulu kwa miaka 4,ndani ya miezi hii 7 kweli miujiza gani itatokea?
Mbona tunakuwa na mipango ya kifala hivi kama taifa?
 
wanarudia mitihani ili iweje kama sababu za wao kufeli bado kuzisolve, pesa hizo zitumike katika kuboresha elimu na kutatua possible problem la watoto kufell wacheni mbwembwe
 
Itakuwa vipi kwa wanafunz waliopata divission 4 ya point 28 na kuendelea, je wanaweza kurudia mtihan huo? Au ndo wataendelea kubaki tu nyumbani?
 
hzo n propaganda zao za kutafuta KURA,mm nnachoona n bora hzo pesa wafanye mipango mikakat ya kuboresha baadhi za shule za kat hl matokeo ya mwakan yacje yakawa haibu zaid ya haya.Hv 2jiulze,leo hii 2nawalpia awa ,je 2nawaandaeje na awa wanaokuja?2nauwakka watafanya vzur?2jipange, kwan njia n 1,shule zilezile madarasa yaleyale na ictoje walmu walewale.Jaman 2nakwenda wap?
 
Mbaya zaidi N/waziri alizitaja sababu za kufeli ni wazazi kutowajibika na pili ni wanafunzi wenyewe.....Sasa kwa akili ndogo tu za primary hatukatai sababu alizozitaja Lakini kuendelea kukwepa kuwataja walimu ina maana wazazi na wanafunzi wao ni lazima wawajibike vilivyo maana Mwalimu hausiki apa kulingana na WIZARA YA ELIMU...Nani asiejua walimu ndo chanzo cha aya matatizo? Hivi tunawezaje kuwapeleka watoto wetu mashuleni uku walimu wakiwa bado wanamigomo baridi tunategemea nini? Au kwa vile wizara inatulaumu wazazi basi kwa tafsiri ndogo tu kila mzazi anawajibika kumfundisha mtoto wake maarifa ambayo hana...Ni aibu kuona wizara/serikali/Rais bado hawajakiri kua maslahi mabovu ya walimu ndo chanzo cha aya yote....AIBU IMEIRUDIA SERIKALI YENYEWE KWANI WALIMU NDO KWANZA WANAPONGEZANA KUA WAMEWEZA NA WANASONGA MBELE
 
Inabidi na naibu elimu naye akaufanye huo mtihani. Hii ni fursa nzuri kwake
 
daaah






naona mawazri
wanakurupuka,wanataka 4m 4
walofeli warudie mithani tena
wakifanya kama PC,



je inamaana
watafanya bla kukaa madarasani,
ikiwa kwa kukaa darasani
alifeli,xaiv afanye bila kukaa
darasani itakuje?




mnataka kuxafsha wizara kwa
kurudia mtihani?dis z nat
fair.mmekurupuka kwa kifup fanyeni
utafiti jins ya kukabiliana na co
kukurupuka ktk maamuzi.




ulale na mkeo,mshauriane ujinga
uje nao bila hata mipango,enough z
enough acheni kuhadaa watoto
pamoja na wazazi wao au ndo
mnatetea matumbo yenu?
au anaandaa kura za 2015???
kuweni na huruma
viongozi,kuwarudisha hao watoto
kufanya mtihani tena kama Pc
hamuwatendei haki.






mnyonge mnyongeni lakini na haki
yake apatiwe
 
Pia serikali iboreshe mazingira ya ufundishaji na ujifunzaji.
 
Back
Top Bottom