Waliofeli Form Four kurudia mitihani bure mwaka huu?

Waliofeli Form Four kurudia mitihani bure mwaka huu?

hivi unawezaje kumchukua mwanafunzi aliyepata div.4...alafu akafundishe watoto...alafu upate watoto wenye ufaulu wa madaja ya juu (div.1&2)???....Labda mi sielewi....ebu nielewesheni jamani...to me it doesn't make any sense...and its not logical at all.....Kwamba mwalimu aliye tunda la failure....amfundishe mtoto afaulu!!!wapi na wapi hii!!.....Kwa nchi za wenzetu (mfano Scandinavia na hata Asia e.g China)waalimu ni matunda ya wanafunzi waliofanye vizuri....Hii dhana ya kuchukua waalimu kutoka kundi la wanafunzi waliofanya vibaya ni kitu cha kufanyia kazi pia hapa TZ....kama kweli tunataka mabadiliko ya dhati kwenye elimu.....hata kama tutapata wanafunzi wachache......lakini bora.....

Btw...mwaka huu watoto wamefeli.....kwanini tunataka warudie mitihani????...kwanini wasifuate utaratibu uliopo..kwamba wasubiri mpaka muda utakapowaruhusu kufanya mitihani kama private candidate???kwanini tunataka warudie sasa...na wakifeli tena je???...mtoto mjinga....ni mjinga tu...kama hukumwandaa tangu mwanzo atafeli tu....no miracles....
 
Wakuu mi sifikirii kama ni vema kwa hawa waliofeli kurudia mitihani tena kwa gharama za serikali,bali yatakiwa tujue tu ya kwamba huo ndio uhalisia wa shule zetu na watoto wetu.Katika shule zetu hizi za miaka hii watoto wapo vizuri sana katika habari za mapenzi kuliko habari za kitaaluma.Lakini pia serikali ndivyo ilvyo wekeza,kumuweka aliefeli akafundishe wenzie maanayake bado unazalisha mabomu.Tusishangae haya nahisi yanakuja makubwa zaidi ya haya.
 
Inabidi na naibu elimu naye akaufanye huo mtihani. Hii ni fursa nzuri kwake

Nimeipenda sana hii, pia na Nape akaufanye, maana matokeo yake ya form four ni aibu.

Ni muda mzuri pia kwa bwana Nape kurudia mtihani!
 
kawambwa na mulugo hizi hela ni nyingi sana

  • :yo:
    • :rockon:


 
Nadhani wakati umefika wa kuithamini taaluma ya ualimu....mtu mwenye busara huchagua punje za nafaka zilizobora kwa ajili ya mbegu kwa misimu ijayo....sisi tunafanya tofauti....kwanini tusipandishe maslahi ya waalimu kisha tukawachukua wale waliopata daraja la kwanza wawe mbegu kama wanavyofanya vyuo vikuu vingi....daraja la pili kuja chini ndiyo wakafanye kazi nyingine.....tupunguze maslahi ya wanasiasa tuyahamishie kwa waalimu....tukifanya hivi nadhani elimu yetu itapanda sana
 
selikari inazengua tu wameshindwa kuboresha shule watawezaje kuwalipia ada ya mtihani hao waliofeli,tatizo wanafanya mambo bila kufikiri.
 
halafu hao wanafunzi watafundishwa na mwalimu yupi? yaani ukiwa na akili kama ya Mulugo ni sawa na kuwa UKIMWI
 
Tatizo wizara inaangalia ilipojikwaa,hawa wengi wao ni wa shule za kata ambazo hazikuwa na walimu,akirudia hawezi kufanya vizuri,wanafunzi wa shule zisizokuwa na walimu wa baadhi ya masomo dawa sio kurudia!Tatizo ni mfumo na shule kutokuwa na walimu,mitalaa ya kisasa,maabara na mambo mengine.Tusitafute sababu ya ku justify kuwasomba waliofeli kwenda advance!
 
Huo ni upumbavu na umbumbu wa mawazo nafikra,kama mwanafunzi akiwa shuleni na walimu alishindwa ,mtihani,je akiwa peke yake kama mtahiniwa binafsi ndo ataweza?labda kama mnatka kuwapa mtihani kama wa form one,maana tumesh wazoea nyie kuharibu elimu ya watoto wetu kisa watoto wenu wasoma ulaya.Kwanini hizo pesa za kugharimia mtihani hamkuwapa walimu ili wawa fundishe watoto bila kinyongo? au ndiyo hako kamtindo kenu mliko gundua siku hizi kakuwachotea alama za bure watoto mmeona dili? darasa la saba mlishusha alama kutoka 100 hadi 70,kidato cha pili mliwaongezea watoto alama 12 kwa kila somo,hivi mnamdanganya nani? basi wapeni alama watoto wakiwa nyumbani kwao,mnasema waende shule kufanya nini kama baadae mnawapa alama za bure ili wafaulu?

Baadhi ya mawaziri waliopita walishauri vibaya serikali wakidai watoto wana soma masomo mengi ni mzigo kwao ndiyo maana wanafeli,jambo ambalo siyo kweli kutokana na ukweli kuwa:

1.Mwanafunzi aliyekuwa anasoma PCM,PCB,PGM,CBG alikuwa hasomi FINE ART,MUSIC,UCHAPAJI WALA COMMERCE,na aliyekuwa anasoma ushonaji,upishi alikuwa hasomi HGL,HGK NK.

2.Wanafunzi funzi siku hizi wanasoma masomo yanayo fanana ndiyo maana wanafeli,kwani mtoto mwenye kipaji cha kuchora,analazimika kusoma sayansi au masomo ya lugha jambo ambalo linamfanya ashindwe kumudu,kisha anaamua kuchora picha wakati swali lilitaka aeleze athari za vita ya majimaji kwa mfano. Sasa ule mchoro lingekuwa somo siangepata A huyo? sasa sifuri zingetoka wapi? na wale wanao andika nnyimbo za bongo flava,kama somo la mziki lingekuwepo siangefaulu huyo?

3,Watoto wanaosoma masomo yanayo fanana nchi nzima baadae mtakuja muwaajiri wapi?
Halafu waziri wa elimu anatudanganya eti wanafunzi wamefeli shule nyingi zinakosa maabara,ni kweli,lakini miaka iliyopita mbona walifaulu shule hizohizo je,makta,maabara,vitabu na hao walimu walikuwapo/zilikwapo? mbona mlifika kuwapongeza wanafunzi waliofanya vizuri bungeni na mkawapa zawadi mkawasahau hata walimu japo hata kuwashika mkono tu.

Imekuwa ni tabia sasa kwa baadhi ya viongozi wa serikali kuwashauri/kuishauri serikali vibaya kwa maslahi yao binafsi,hata katika kipindi cha sensa waliamua kutumia kigezo cha mgomo wa walimu kuwanyima walimu sensa eti wataivuruga kumbe walitaka kuuza nafasi na kuwapa ndugu na jamaa zao.

4.Serikali yenyewe mwakajana ilifunga shule kwa muda mrefu kwa kisingizio cha sensa,ambapo walimu wachache tu walishiriki zoezi hilo,na wengine walikaa tu nyumbani,mlitegemea miujiza gani katika matokeo?

5.Ni waziri gani anaweza kufanya kazi kwa ufanisi huku akiwa anabubujikwa kwa na machozi kisa mshahara mdogo,na maslahi mengine anapunjwa?mlitegemea walimu wafanyaje kama wanachoomba hawapewi na kuambulia vitisho?

MAONI YANGU:

1.Kaeni meza moja na walimu mzungumze juu ya masilahi yao ili walimu warudishe moyo wa kazi
2.Rudisheni masomo ya biashara,uchoraji,kilimo,upishi,ushonaji na uchapaji ili watoto wawe na uwanja wa kuchagua masomo wanayoweza nayanayo weza kuwapa ajira.
3.Wizara ya elimu ni pana mno kiasi cha waziri mmoja hata akawa mahiri hawezi kuimudu,maoni yangu,kuanzia chekechea hadi darasa la saba iwe wizara moja,sekondari zimekuwa nyingi sasa,iwe wizara na vyuo vya ufundi,na ualimu iwe pia wizara yake na vyuo vikuu viwe na wizara yake na wizara ambazo hazina changamoto nyingi ka michezo,habari,nk zinaweza kuunganishwa pamoja.
4.Nchi nzima itumie kitabu cha aina moja kwa shule zote,kuliko ilivyo sasa kila mtunzi anapeleka kitabu kitumike shuleni.

5.Ikumbukwe kuna kipindi walimu wa shule za msingi walipata mafunzo ya ualimu kwa muda wa mwaka mmoja tu na huku ufaulu wao ukiwa chini,serikali imesahau kuwapa mafunzo kazini ili wajenge msingi mzuri kwa wanafunzi wa shule za msingi,hivyo wapate mafunzo kazini.

6.Waziri katika matatizo aliyoyataja,hakusema kama shule nyingi za kata wanafunzi hawapati,uji wala chakula cha mchana shuleni,serikali ifanye mpango watoto wale shuleni angalau hata uji tu.Haiwezekani mtoto aokea mbagala akasome bunju bila kula halafu mtoto huyo utegemee apate dision ONE.

7.Shule nyingi za kata hazina madarasa ya kutosha,msongamano madarasani ni mkubwa,wananchi siku hizi hawataki kuambiwa juu ya kujitolea ili kukamilisha madarasa katika shule zile.Sasa napendekeza mahabusu na wafungwa wakafanye kazi ya ktengeneza matofali,wajenge,wapaue na kufaya finishing ,huku serikali na wananchi wakichangia bati na saruji na mbao,kuliko kuwarundika tu magerezani bila kazi.

Maoni yangu kwa leo ni hayao,
FATHER OF HISTORY natoweka,byeeeeee!











H
Naibu Waziri wa Elimu Philipo Mulugo alipozungumza na gazeti la HabariLeo kuhusiana hatua zitakazochukuliwa na serikali kutokana na idadi kubwa ya watahiniwa wa kidato cha nne kupata sifuri, amedai kuwa serikali inafikiria warudie mtihani mwaka huu.

Amesema serikali inaangalia namna ya kuwalipia ada ya mtihani ambayo mwaka jana walilipa Sh 35,000 kila mwanafunzi. Likipita hilo la kurudia mtihani, serikali italipia ada hiyo na wataufanya kama watahiniwa binafsi.

Ingawa alisema wazo hilo halijapitishwa, lakini hivi sasa linajadiliwa kuona namna ya kuwasaidia watahiniwa zaidi ya 240,000 kurudia mtihani wa Taifa kwa gharama za serikali.

Kuhusu idadi ya watakaoingia kidato cha tano mwaka huu alisema, matokeo hayatarekebishwa kwa namna yoyote, ili kuongeza idadi ya watakaoingia kidato cha tano mwaka huu, bali watahiniwa 23,500 waliopata daraja la kwanza hadi la tatu ndio watakaoendelea. Alisema watakaochukuliwa Ualimu ni wa daraja la nne ya alama 26 na 27 huku wenye alama 28 wakiachwa bila kuchukuliwa mwaka huu.


Source: Habari Leo

N.B: Kwa mahesabu ya haraka haraka kama serikali itaamua kuwalipia wanafunzi zaidi ya 240,000 waliofeli kurudia mitihani itagarimu sio chini ya Sh. 8,400,000,000.
 
mkuu akenejo fanya kama bro. Nape unajiendeleza na madivision FOUR yako fresh maisha yanasonga mbele; ikiwezekana unamwomba akututie nawe ukatibu enezi wa kueneza elimu sasa na siasa tena.:ranger::ranger::ranger::ranger: ushanifahamu uzuri.
Ngoja na mimi niliyefeli enzi ya nyerere nikarudie nije niokoe taifa hili
 
tusimlaumu sana mkuu; hili tukio halijatokea mara moja tu paaa,, no. kuna sintofahamu nyuma ya pazia walioanza ilikuwa hadi kumfikia yeye. may be walikuwa ni majambazi wa mitihani wale waliopita:yo::yo::yo::yo: ushanifahamu uzuri
Gharama hizo ni kubwa sana ni lazima Waziri wa Elimu awajibike. Hatuwezi kuwalipia watoto hawa mara ya pili kwasababu ya usingizi wa mtu tuliyempa mamlaka awaelimishe vijana wetu.
 
kuna uwezekano wa kurudiwa kwa mitihani ya kidato cha nne 2012.ni kweli wakifanya hvyo itakuwa wameokoa taifa?
 
Kama wakirudia je wale wasiomaliza silabasi watarudi kumalizia? Nahisi ziro zitaongezeka kwa 20% zaidi
 
kuna uwezekano wa kurudiwa kwa mitihani ya kidato cha nne 2012.ni kweli wakifanya hvyo itakuwa wameokoa taifa?


Kama huo ndo mpango wa Serikali basi tumekwisha, ina maana ndo tuseme mtihani utakaorudiwa ni uleule uliokwisha fanyika ama ni kwamba utatungwa mtihani mwingine? Na kama ni kutunga mwingine utatungwa ulio rahisi ili WATAHINIWA wafauru ili kuficha aibu kwa Taifa? Ukiachana na suala la gharama, kama utatungwa ulio rahisi ili watahiniwa wafaulru si ndo tunaandaa VIHIYO huko mbeleni. Miye nadhani suala la kushughulikia ni kuangalia upya kwa nini wanafunzi wamefeli na hapa ni kwamba hata mtihani ukirudiwa wanafunzi hawaelewi kitu tu.
 
Back
Top Bottom