Waliochaguliwa kuandaa mpango wa maendeleo 2050 wote wanaishi Mbezi Beach au Masaki, wanalishwa kwa kodi za umma miaka yote, wana umri zaidi ya 50 yrs

Leo kina shivji wanamsifu mwl wanamponda Jakaya, nani muasisi nani muishi
Nyerere ana kosa ametutendea. Ameulea na kuusimika mfumo kandamizi na chama jambazi kwa Watanzania.

Mimi namupna kama mtu aliyeidhibiti Tanzania na siyo kusimika taasisi zinazowajibika kwa nchi kwa maana ya ustawi, hadhi na utashi wa Taifa
 
Mipango ya Tanzania ni sawa na kujenga nyumba juu ya mchanga, itaanguka tu badae excuse na mafanikio ya kupika yanafata kujustify ulaji mwingine.Hii nchi ilipofikia sasa inahitaji default setting na hii itafanywa na wananchi wenyewe pale wataamuka kutoka katika usingizi na kuwaza yale yaliyo ya muhimu. Hayo mengine ni mabaraza ya kutafuna fedha za nchi na hayana majibu kwa matatizo ya nchi hii. Solution haiwezitoka kwa watu walewale waliotengeneza tatizo, hiyo ni tamthilia.
 
Hujaelewa hoja ya mtoa mada, ajakataa academicians, hoja wale wangebaki kwenye uchakataji wa mawazo ya wadau muhim na ambao wapo kwenye hualisia
Hao wa kwenye uhalisia watatoa maoni yao kwa hao wa "makaratasi" ndio wanyooshe maelezo. Hata bungeni la saba wataongea weee ila wanasheria ndio wanaenda kuuweka sawa muswada wa sheria ndio upitishwe. Huwezi weka laymen kuandaa andiko la kitaalamu. Hata ilani ya CCM iliandikwa na PhDs watupu same to CHADEMA tuliandikiwa na Bashiru Ally pamoja na PhDs wenzake.
 
Huyo Mduma ana uzoefu gani?Lecture wa chuo kikuu huyo Mduma

Mleta uzi analalamika uwepo wa hao lectures kama Neema Mduma

Wewe unamtetea huyo Neema Mduma,Una undugu nae huyo mwalimu ?

Badala ya kujibu hoja za kujaza akademician au walimu wa vyuo vikuu wewe unamtetea mwalimu mmoja wa chuo kikuu cha Nelson Mandela Arusha aitwae Neema

Profesa kabudi na Ossoro wa madini si ndio walimuingiza chaka JPM kwenye madini na sasa tunalipa?
Unamjua Dr Mduma? Umaarufu kaupata kwa tafiti anazofanya huko duniani tena ni practical. Nimekueleza kaandaa hadi mfumo wa kubashiri wajawazito mashuleni kutumia takwimu ili kupunguza school dropouts. From machine learning to Artificial Intelligence anatuwakilisha huko duniani na umri wake ni less than 40 unampuuzaje mtu wa hivyo!!
Profesa kabudi na Ossoro wa madini si ndio walimuingiza chaka JPM kwenye madini na sasa tunalipa
Kabudi na Osoro walifanya kazi bila uhuru mfano Rais ameshasema tunaibiwa madini wasingeweza kuonyesha hatujaibiwa!! Na hii ni shida ya taasisi kufanya kazi bila uhuru. Ila watu wakipewa uhuru kama alivyosema Leo Mama Samia obvious watajimwaga wanavyoweza. Nadhani it's clear Mama Samia ni pragmatic kuliko JPM ndio maana licha ya kupinga katiba mpya ila bado kikosi kazi kikashauri katiba mpya ni lazima. Hayo yasingewezekana chini ya JPM otherwise angehukumu wanyongwe kwenye Live TV.
 
Tulitegemea kuona wafanyabiashara, wataalam wa TEHAMa na watu wenye mafanikio kwenye jamii wakiwa Sehemu ya timu . Academia wangebaki kwenye technical team ya waandishi siyo wachakata hoja.

Tunaanza kufeli kupanga kama Ishara ya kufeli kufanikiwa...........nchi haiwezi ikapangiwa kila kitu na wakaazi wa mbezi beach inahitaji watu wa namtumbo, Kaperamsenga na Kipandaule washiriki pia.
Hali zao za kipato zipoje?
Asilogwe akaweka magabachori design ya Rostam Aziz watatuuza
 
Hahaha nimecheka sana

Haha entrprinuaaa😂

Oky
Haaahaaaa ndio profile yake inasema hivyo na kwakuwa yupo TanTrade so anajua jinsi biashara zinavyofanyika na changamoto zilizopo kisheria na kiuchumi.

Hao mama ntilie na boda boda wataombwa maoni ila hawa ndio waandishi tu
 
Mhe. Waziri Kitila Mkumbo ametoa majina ya watu alioteua kutengeneza mpango wa 2050. Wote walioteuliwa wana miaka 50 kwenda mbele, ni wake au watoto wa viongozi wa CCM, ni wanazuoni waliofundisha na kusoma naye chuo...........hizi siyo zama za giza ni zama za technology. Hakuna namna hawa wazee wanaweza kuweka projection za nchi kuendana na technology badala yake watakwenda kutuletea nadharia kwenye vitabu

Tulitegemea kuona wafanyabiashara, wataalam wa TEHAMa na watu wenye mafanikio kwenye jamii wakiwa Sehemu ya timu . Academia wangebaki kwenye technical team ya waandishi siyo wachakata hoja.

Tunaanza kufeli kupanga kama Ishara ya kufeli kufanikiwa...........nchi haiwezi ikapangiwa kila kitu na wakaazi wa mbezi beach inahitaji watu wa namtumbo, Kaperamsenga na Kipandaule washiriki pia.

Hawa watu wa masaki na Mbezi Beach wanawekwa kwenye mipango ya nchi ndio wanaotengeneza propaganda za utajiri kwenye umaskini. Mtu kazaliwa hadi anazeeka yupo analishwa na serikali kwa kodi za wananchi anawezaje kujua matatizo ya wananchi? Ndio hawa badala ya kuripoti uhalisia wao wanaripoti uongo na uzandiki walioandika kwenye vitabu vyao.
NCHI HII INA WAJINGA WENGI SANA

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Watafute watu kutoka nje pia hasa mataifa ya Singapore, Vietnam, Malaysia, Korea Kusini, Taiwan, Hong Kong.
 
hao ndio wanamshauri vibaya bibi shangwe, maana hawajui yanayoendelea mitaani...wao kutwa kucha wanalindwa na askari kuzunguka na magari hata masokoni hawaendi, hawapandi daladala..yaani hao ni kama vipofu wa mambo yanayoendelea nchini..alafu ndio hao wanateuliwa kuandaa mambo ya msingi. Ndio maana wananchi wanazidi kupokea maisha magumu tokea kwa viongozi wa nchi...yaani viongozi wa nchi wamekuwa vinara wa kupeleka kilio kwa wananchi wao....maumivu na uchungu tele, wanapeana ulaji tu mambo ya msingi hawazingatii
 
Nchi hii nafasi ziko kwa connections, huna connection hata uwe na uwezo kiasi gani utapata tabu sana kufikia nafasi za hivyo. Hiyo mipango wanayopanga mingi ni nadharia ndio maana wanachaguana wa huko huko ushefani.



Na lobbing kama zote.

Ukiwa hana na presidential appointment,

Yani hata ndani ya taasisi za umma wakuu wa idara na vitengo nasikia ni kwa lobbing .

Sasa wenye uwezo ambao hawaamini ktk kufanya lobbing hawapewi nafasi za uongozi.

Unakuwa watu uwezo ni Mdogo lakini sababu anajua ku-lobby anakuwa kiongozi na mambo yanaenda bora liende.

Na nasikia kuna mambo ya kujitoa mwili, fedha, na kuahidi regular marejesho?!

Na mpaka mtu anafanya lobbing kwa kutoa hela, mwili na ahadi ya kukuletea regularly hivi Kwanini usijiulize huyo mtu hiyo nafasi analenga kufaidika nayo kibinafsi mabala ya kuzingatia maslahi ya umma tu?!

Kama ni kweli unategemea utendaji utakuwa wa kuridhisha kimaendeleo kweli?

Kwanini kusiwe na mfumo wa kutangazwa na mchujo wa wazi?
 
1. Mbona hawa wamo au hujamuona Rais wa Tanzania Startup association. Pia yumo Dk Neema Mduma ndio ali design mifumo ya machine learning kubashiri mabinti kuacha shule kisa ujauzito!!. So watu wa technology ni wengi humo. Pia wapo wajasiriamali mfano hapo Mgetta she's an entrepreneur pia board member Tantrade.

2. Why academicians? Dunia nzima kazi za consultancy na strategic plans hakuna watu better kuziandaa kuliko Academicians. Hawa laymen/wafanyabiashara wataitwa tu watoe maoni ila wanaoandaa draft zile have to be academicians maana wamebobea kwenye hizo mambo kwa miaka mingi.

Ambacho labda hakijakaa sawa kama ulivyosema ni balance ya wasomi vs kada zingine. Sema mpango wa taifa ni framework tu mfano watasema Huduma za afya kupitia bima ya wote. Sasa mpango wa miaka mitano mitano ndio utaeleza KIVIPI hiyo vision inatekelezeka.

4. Ila miaka yote tatizo sio uandaaji mpango ila utekelezaji. Mfano mpango wa 2015-2020 ulisema Tanzania nchi ya viwanda alafu wa 2021-25 unasema tumeshavuka kuwa nchi ya viwanda eti sasa tunafanya value addition ili kuuza nje na sio kuuza raw material kama zamani. Ni maneno ya karatasi tu ila hakuna hata kiwanda kimoja cha kueleweka hapa nchini mfano say magari, ndege, kuchenjua dhahabu n.k
Issue watoto wa kishua hawajui shuruba za umasikini
 
Mhe. Waziri Kitila Mkumbo ametoa majina ya watu alioteua kutengeneza mpango wa 2050. Wote walioteuliwa wana miaka 50 kwenda mbele, ni wake au watoto wa viongozi wa CCM, ni wanazuoni waliofundisha na kusoma naye chuo...........hizi siyo zama za giza ni zama za technology. Hakuna namna hawa wazee wanaweza kuweka projection za nchi kuendana na technology badala yake watakwenda kutuletea nadharia kwenye vitabu

Tulitegemea kuona wafanyabiashara, wataalam wa TEHAMa na watu wenye mafanikio kwenye jamii wakiwa Sehemu ya timu . Academia wangebaki kwenye technical team ya waandishi siyo wachakata hoja.

Tunaanza kufeli kupanga kama Ishara ya kufeli kufanikiwa...........nchi haiwezi ikapangiwa kila kitu na wakaazi wa mbezi beach inahitaji watu wa namtumbo, Kaperamsenga na Kipandaule washiriki pia.

Hawa watu wa masaki na Mbezi Beach wanawekwa kwenye mipango ya nchi ndio wanaotengeneza propaganda za utajiri kwenye umaskini. Mtu kazaliwa hadi anazeeka yupo analishwa na serikali kwa kodi za wananchi anawezaje kujua matatizo ya wananchi? Ndio hawa badala ya kuripoti uhalisia wao wanaripoti uongo na uzandiki walioandika kwenye vitabu vyao.
Usomi wao, sio shida, shida ni siasa kuingilia Mambo ya kitaalamu,
Nimekutana na dokta mmoja, PHD, ni lecturer taasisi moja, jamaa, ana design electronic system, hatari, anakodishwa na makampuni makubwa duniani, kwa hapa bongo, wachina, kuwatengenezea na ku repair mifumo ya kielectenics, ya magari, mitambo, nk,
Wasomi ndio wanaoweza ku Jenga Sera kisayansi, x
 
Back
Top Bottom