Taarifa ya vifo vya watu wawili waliobanwa na roli kwa zaidi ya masaa 16 iliyotangazwa leo na ITV inasikitisha sanasana.Jana ITV waliwaonyesha watanzania hao wakiwa wamebanwa na mizigo,huku wakiwa kwenye maumivu makali waliomba msaada kwa serikali yao sikivu ya CCM,cha kushangaza hakuna msaada wowote uliotolewa.Kamanda alijaribu bila mafanikio kuomba gari la kuinua mizigo winch .Hivi serikali ilishindwa kutoa msaada wa haraka kwa kupeleka winch kwa zaidi ya masaa 16 au walifanya makusudi maana walionaswa kwenye tukio walikuwa walalahoi? Hivi angekuwa kigogo amenaswa au fisadi papa kanaswa si wangepeleka winch kwa Helikopta? Watanzania umefika wakati wa kujiuliza,hivi serikali ya sasa ya CCM inajali usalama wa watanzania walalahoi? Nini kifanyike ili watanzania wote tuwe na uhakika wa kupata msaada tunaouhitaji toka serikali sikivu ya CCM pale tunapokumbana na majanga?
ITV jana ilifanya kazi yake km chombo cha habari kwa kutoa taarifa ya kina iliyojaa simanzi ya hali ya juu kwa wale waliotazama watakiri kwa hili yani mpaka mtangazaji studio alionyesha sura ya masikitiko makubwa wahanga kwa sauti zenye majonzi ziliomba msaada kwa serekali yao sikivu kuwasaidia kuwaokoa kwenye mauti lakini masikini ya Mungu hakuna msaada wowote toka serekalini inauma sana,wangekuwa wageni weupe toka ngambo serekali ingefunga ofisi kwenda kunusuru maisha yao
Nchi imeoza,JK unda DISASTER RECOVERY AGENCY haraka sana,hatuwezi shuhudia kufa hovyo
Mkuu Poleni!
Mngeomba gari ya washawasha ingesafirishwa hata kwa ndege.
Taarifa ya vifo vya watu wawili waliobanwa na roli kwa zaidi ya masaa 16 iliyotangazwa leo na ITV inasikitisha sanasana.Jana ITV waliwaonyesha watanzania hao wakiwa wamebanwa na mizigo,huku wakiwa kwenye maumivu makali waliomba msaada kwa serikali yao sikivu ya CCM,cha kushangaza hakuna msaada wowote uliotolewa.Kamanda alijaribu bila mafanikio kuomba gari la kuinua mizigo winch .Hivi serikali ilishindwa kutoa msaada wa haraka kwa kupeleka winch kwa zaidi ya masaa 16 au walifanya makusudi maana walionaswa kwenye tukio walikuwa walalahoi? Hivi angekuwa kigogo amenaswa au fisadi papa kanaswa si wangepeleka winch kwa Helikopta? Watanzania umefika wakati wa kujiuliza,hivi serikali ya sasa ya CCM inajali usalama wa watanzania walalahoi? Nini kifanyike ili watanzania wote tuwe na uhakika wa kupata msaada tunaouhitaji toka serikali sikivu ya CCM pale tunapokumbana na majanga?
Imeniuma sana aisee maana jana niliwaona wakiongea kwenye tv leo hatunao,lkn ingekuwa mtu ,wenye title tungeona hata meli za kijeshi maseyu zikitoa msaada. RIP comrades