Waliobanwa katika ajali wafariki

Waliobanwa katika ajali wafariki

Sina la kusema,pumzikeni kwa amani ndugu zetu
 
Yaaani nimewaona jana usk na leo asb Itv, nimeumia mpk basi. Vijana shababi si mchezo taifa limepoteza nguvu kazi. Je hakuna wa kujiuzuru hapo kweli?
 
Taarifa ya vifo vya watu wawili waliobanwa na roli kwa zaidi ya masaa 16 iliyotangazwa leo na ITV inasikitisha sanasana.Jana ITV waliwaonyesha watanzania hao wakiwa wamebanwa na mizigo,huku wakiwa kwenye maumivu makali waliomba msaada kwa serikali yao sikivu ya CCM,cha kushangaza hakuna msaada wowote uliotolewa.Kamanda alijaribu bila mafanikio kuomba gari la kuinua mizigo winch .Hivi serikali ilishindwa kutoa msaada wa haraka kwa kupeleka winch kwa zaidi ya masaa 16 au walifanya makusudi maana walionaswa kwenye tukio walikuwa walalahoi? Hivi angekuwa kigogo amenaswa au fisadi papa kanaswa si wangepeleka winch kwa Helikopta? Watanzania umefika wakati wa kujiuliza,hivi serikali ya sasa ya CCM inajali usalama wa watanzania walalahoi? Nini kifanyike ili watanzania wote tuwe na uhakika wa kupata msaada tunaouhitaji toka serikali sikivu ya CCM pale tunapokumbana na majanga?

Mkuu Poleni!

Mngeomba gari ya washawasha ingesafirishwa hata kwa ndege.
 
ITV jana ilifanya kazi yake km chombo cha habari kwa kutoa taarifa ya kina iliyojaa simanzi ya hali ya juu kwa wale waliotazama watakiri kwa hili yani mpaka mtangazaji studio alionyesha sura ya masikitiko makubwa wahanga kwa sauti zenye majonzi ziliomba msaada kwa serekali yao sikivu kuwasaidia kuwaokoa kwenye mauti lakini masikini ya Mungu hakuna msaada wowote toka serekalini inauma sana,wangekuwa wageni weupe toka ngambo serekali ingefunga ofisi kwenda kunusuru maisha yao

Na bado kamanda wa kikosi cha zimamoto na uokoaji wa mkoa na wa kitaifa wapo kazini! Magari yote yanalipa ada ya zima moto na uokoaji. Mimi kagari kangu ka cc 1998 ninalipa TShs 30,000/= kwa mwaka. Hizi hela zinaenda wapi?
 
Inauma sana, kwani mpaka ITV wanarusha ni zaidi ya masaa8, nauliza mkuu wa wilaya/mkoa ktk eneo husika walikuwa wapi? R.I.P
 
pole kwa watanzania wenzangu makabwela km mm!!kiukwel hii ni hataree,ITICAFU hpa lzm ifanye kazi tu!
 
yan kwa hayo masaa hata vifaa vingetoka dar vingewakuta wako hai..poleni wafiwa ila naimani watakuwa wamelala wakitegemea ufalme wa mbinguni siku moja kwa mateso waliyopata sidhani kama wameshindwa kumlilia Mungu naimani wametamka Mungu ndani ya masaa yote hayo kumi.
 
Mabadiliko NI MiMi na wewe mambo magumu sana nchi hii inamaana hata wasafiri wenye magari walishindwa kufanya mchakato hata wa kuvuta hyo gar kwa minyororo? Hatuna uzalendo hata kidogo na hatuna utu kabisaaaaa tunajali tuu Pesa, serikali bom feki na zembe inatilia mkazo mambo yasio YA maana kama kutumia nguvu nyingi ktk kuzuia maandamano YA chadema lakn kuwanusuru watanzania wasio na hatia tena masikini hakina
 
Hii ni mbaya sina maelezo ya kuisimulia nchii ni hatari kuishi kuliko somalia na syria Mungu atusaidie ila hii serikali ya CCM
 
Pamoja na vyombo vya habari kuonyesha tukio lile, hakuna hata kiongozi mmoja aliyeshtuka. Hakuna aliyeona thamani ya uhai wao.
Kesho tutawasikia na salaam zao za rambirambi, ujinga mtupu.
Siamini kwamba hakukuwa namna yoyote ya kuwaokoa, siamini na siwezi kuamini asilani. Damn this country

RIP wapiganaji.
 
Mkuu Poleni!

Mngeomba gari ya washawasha ingesafirishwa hata kwa ndege.

C' est le 'laissez a' affaire gvt'! who cares! kuna maeneo ninapoishi, karibu na mkuu wa wilaya/halmashauri lakini miundombinu ovyo ovyo. wanachukua chao mapema.
 
Jamaa wa CCM thread Kama hizi hauwaoni. Yaani serious my first enarmy in this world ni CCM. Nawachukia sana watu hawa wanafiki
 
nimepata uchungu hasa.na ninayo kila sababu ya kuamini serikali ya ccm imeachwa na Mungu na hakuna hata aliyebaki mwenye busara na hekima
 
Taarifa ya vifo vya watu wawili waliobanwa na roli kwa zaidi ya masaa 16 iliyotangazwa leo na ITV inasikitisha sanasana.Jana ITV waliwaonyesha watanzania hao wakiwa wamebanwa na mizigo,huku wakiwa kwenye maumivu makali waliomba msaada kwa serikali yao sikivu ya CCM,cha kushangaza hakuna msaada wowote uliotolewa.Kamanda alijaribu bila mafanikio kuomba gari la kuinua mizigo winch .Hivi serikali ilishindwa kutoa msaada wa haraka kwa kupeleka winch kwa zaidi ya masaa 16 au walifanya makusudi maana walionaswa kwenye tukio walikuwa walalahoi? Hivi angekuwa kigogo amenaswa au fisadi papa kanaswa si wangepeleka winch kwa Helikopta? Watanzania umefika wakati wa kujiuliza,hivi serikali ya sasa ya CCM inajali usalama wa watanzania walalahoi? Nini kifanyike ili watanzania wote tuwe na uhakika wa kupata msaada tunaouhitaji toka serikali sikivu ya CCM pale tunapokumbana na majanga?

Fikiri kama ingekuwa bw nepi au chemba, dk 5 tu wangechomolewa. Ccm hoyeee.
 
Imeniuma sana aisee maana jana niliwaona wakiongea kwenye tv leo hatunao,lkn ingekuwa mtu ,wenye title tungeona hata meli za kijeshi maseyu zikitoa msaada. RIP comrades

Mkuu hii inaweza kutokea kwa nchi ya mabwege tu.
Hao fire and rescue pamoja na jeshi la polisi wanatakiwa kuwajibika kwa vifo hivyo.

Wangeweza kuomba crane hata Mbeya kama iringa hakuna hata ya private. Na wangeweza ku organize first aid kwa watu hao lakini hawakufanya....hayo ni mauaji tena kwa kukusudia.
 
........ Wamekufa vifo vya kusikitisha saana huku wanajiona.....Wakulaumiwa ni viongozi wote kuanzia wilaya na mkoa husika.... hii ndiyo Tanzania....wanangoja mpaka Rais aende ndo wanapapatka......... Unadhani hata uokoaji kwenye gorofa lililoanguka bila Rais kwenda pale yale magari ya Strabag na zile winji ........... ungeambiwa hayana mafuta .. nk nk R.I.P.marehemu wote
 
Aandae chakula kwa waliopoteza Maisha!!R.I.P watz wenzangu
 
Back
Top Bottom