Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,898
- Thread starter
- #21
Habari hii kuanzia kichwa cha habari imechukuliwa kutoka Gazeti la Nipashe, kichwa cha habari sijakitunga mimi.
Jambo moja la msingi ninavyofahamu RPC hulindwa wakati wote na jeshi la polisi. Nyumba anayoishi hulindwa pamoja na familia yake. Awepo asiwepo utakuta askari wanazamu ya kupokezana kulinda makazi ya RPC usiku na mchana.
Po pote aendako RPC anaendeshwa na dereva ambaye kwa namna nyingine ndiye mlinzi wake.
Mazingira ya kukutwa RPC akiwa peke yake akiendesha gari usiku akiwa na mwanamke ndani ya gari yake na hivyo kuuawa katika mazingira tatanishi bila uwepo wa dereva wake na bila ulinzi wa askari polisi kwa mujibu wa sheria kwa sasa ni jambo linalofunikwafunikwa, lakini ni kasoro kubwa ambayo sasa polisi wanategemea source moja tu ya yule mama aliyekuwa naye ambaye hakuguswa katika mauaji yale.
Kiongoze wa ngazi ya RPC hutakiwa muda wote alipo radio yake iwe on ili kubaini cho chote kinachoweza kumdhuru au mazunguzo yake yawe yanafuatiliwa na mfumo wa mawasiliano wa ofisi yake na ni njia ya usalama wa viongozi wa vyombo vya usalama.
Wenzetu polisi muda wote akiwa kazini hata wa kawaida radio na video viko on na kurekodi kila kitu na kuwa ofisini wanaona kila kitu kinavyoendelea polisi akiwapo kazini, hii husaidia utandawazi katika shughuli zao za kila siku bila kificho.
Nini kilichomwogopesha RPC kuwa na dereva wake wakati mauaji yakimkuta wakiwa wawili peke yao na mwanamke? Kwani hata mlinzi wake kama angekuwepo si Tanzania tumezoea wafanyayo wakubwa tunalinda heshima zao wakisha kunywa soda zao wakati tunajua wako wapi na tunawalinda kisha tutamfikisha salama kwake. Hata kama alitumia gari binafsi kwa nafasi yake na kwa taratibu za jeshi anapaswa kuwa na ulinzi.
Tusipokuwa waangalifu katika hili tutakuja kushangaa Rais wa nchi anaendesha collola ya Ridhiwan akiwa mazingira tatanishi yenye kuhatarisha usalama wake bila uwepo wa walinzi wake, bado tutajenga hoja za utetezi kumlinda.
Nemeshuhudia viongozi wengi wa ngazi yake hata wa chini ya ngazi yake wawapo katika vikao kama hivyo hufuatana walao na mtu au watu wenzake tena hao hawahitaji ulinzi wa pekee, sembuse RPC?
Jambo moja la msingi ninavyofahamu RPC hulindwa wakati wote na jeshi la polisi. Nyumba anayoishi hulindwa pamoja na familia yake. Awepo asiwepo utakuta askari wanazamu ya kupokezana kulinda makazi ya RPC usiku na mchana.
Po pote aendako RPC anaendeshwa na dereva ambaye kwa namna nyingine ndiye mlinzi wake.
Mazingira ya kukutwa RPC akiwa peke yake akiendesha gari usiku akiwa na mwanamke ndani ya gari yake na hivyo kuuawa katika mazingira tatanishi bila uwepo wa dereva wake na bila ulinzi wa askari polisi kwa mujibu wa sheria kwa sasa ni jambo linalofunikwafunikwa, lakini ni kasoro kubwa ambayo sasa polisi wanategemea source moja tu ya yule mama aliyekuwa naye ambaye hakuguswa katika mauaji yale.
Kiongoze wa ngazi ya RPC hutakiwa muda wote alipo radio yake iwe on ili kubaini cho chote kinachoweza kumdhuru au mazunguzo yake yawe yanafuatiliwa na mfumo wa mawasiliano wa ofisi yake na ni njia ya usalama wa viongozi wa vyombo vya usalama.
Wenzetu polisi muda wote akiwa kazini hata wa kawaida radio na video viko on na kurekodi kila kitu na kuwa ofisini wanaona kila kitu kinavyoendelea polisi akiwapo kazini, hii husaidia utandawazi katika shughuli zao za kila siku bila kificho.
Nini kilichomwogopesha RPC kuwa na dereva wake wakati mauaji yakimkuta wakiwa wawili peke yao na mwanamke? Kwani hata mlinzi wake kama angekuwepo si Tanzania tumezoea wafanyayo wakubwa tunalinda heshima zao wakisha kunywa soda zao wakati tunajua wako wapi na tunawalinda kisha tutamfikisha salama kwake. Hata kama alitumia gari binafsi kwa nafasi yake na kwa taratibu za jeshi anapaswa kuwa na ulinzi.
Tusipokuwa waangalifu katika hili tutakuja kushangaa Rais wa nchi anaendesha collola ya Ridhiwan akiwa mazingira tatanishi yenye kuhatarisha usalama wake bila uwepo wa walinzi wake, bado tutajenga hoja za utetezi kumlinda.
Nemeshuhudia viongozi wengi wa ngazi yake hata wa chini ya ngazi yake wawapo katika vikao kama hivyo hufuatana walao na mtu au watu wenzake tena hao hawahitaji ulinzi wa pekee, sembuse RPC?