Chama cha Walimu (CWT) kitapata wapi ujasiri wa kutetea msalahi ya Walimu?

Kiranja wa jamii

JF-Expert Member
Jan 2, 2023
222
529
Hili ni swali ambalo kila Mwalimu na mdau wa maendeleo anatakiwa kujiuliza kabla hajafikiria kuwa ipo siku chama hicho cha wafanyakazi kitakuja kutetea maslahi ya Walimu nchini

Binafsi kwa wiki hizi mbili nimekuwa nikifuatilia mwenendo wa chama hiki cha Walimu Tanzania (CWT) na nimebaini kuwa Walimu wengi hawakipendi chama chao. Baadhi ya sababu ni hizi zifuatazo:-

1. Viongozi wa chama hiki ni sehemu ya "chawa" wa serikali kwa maana ya kuogopa rungu la serikali wakienda kinyume na matakwa yake

2. Walimu wengi wameshapata uelewa kuwa makato ya 2% wanayokatwa kwenye mshahara wao ni makubwa na hayana msaada wa moja kwa moja kwao (Zaidi ya Bilioni nne kwa kila mwezi)

3. Chama kina mali nyingi ambazo haziwafaidishi wanachama moja kwa moja. Mfano; Jengo la Mwalimu House, Majengo kila wilaya ambayo yamepangishwa kwa shughuli mbalimbali ikiwemo ofisi na biashara nk

4. Mishahara ya wafanyakazi wa chama hata wale wa chini na posho ni kubwa kuliko ya walimu

5. Viongozi wanapata nafasi kwa "kuhonga" na "kujipendekeza" kwa viongozi (hili halina ushahidi wa moja kwa moja lakini lipo)

6. Mapato ya chama ni makubwa sana (Zaidi ya Bilioni nne kila mwezi) kuliko huduma wanazopata

7. Matumizi ya fedha za chama ni makubwa na matumizi hayo si kwa lengo la kuwanufaisha wanachama. Mfano; Tamasha linalotarajia kugharimu Bilioni saba kuadhimisha miaka 33 ya chama hicho

Ikiwa chama chenyewe peke yake kinanyooshewa vidole na wanachama wake, kitawezaje kuinyooshea kidole serikali pale inapokiuka haki za walimu??

Ni wakati sasa TUCTA kama mlezi wa vyama vyote vya wafanyakazi waingilie kati kunusuru hali hii vinginevyo Walimu watakosa mtetezi katika mambo yao au laa Walimu nchi nzima "waliamshe" kwa hash tag ya "FUTA CWT, HAINA MSAADA KWA MWALIMU" halafu waanze upya!

Au mnasemaje wajameni!
 
Mapendekezo yako hayana tofauti na ule msemo wa kesi ya nyani unampelekea ngedere aamue.
Kama ulikuwa hujui, hiyo CWT na TUCTA ni matawi ya CCM. Hivyo usitegemee maajabu. Hivyo makato ya 2% yako pale pale mpaka CCM itakapo ondolewa madarakani.
 
Hayo maadhimisho ya miaka 33 Yana maana Kwa hao Viongozi wa CWT.Walimu wetu wameendelea kudhalilika,kudharauliwa,kupuuzwa,kuonewa na kuchezewa TU.Sijuwi mafanikio au faida ya Cwt Kwa walimu wetu wanazungumzia kwenye nyanja ipi.Walimu hawana posho ila viongozi wa Cwt wanalipana wao kupitia 2% ya wanachama,walimu wetu hawana hata overtime kama tunavyoona watumishi wengine wakipatiwa.Adui wa mwalimu ni mwalimu hususa aliyepata nafasi nje ya uwalimu.
 
Msingi wa cwt kuwa Kama ilivyo leo no matokeo ya utekaji uliofanywa na unaofaywa na serikali kufifisha vyama huru vya wafanyakazi!!!!!Tanu iliifuta TFL Kwa kumtumia kawawa Rashid na kumpoteza kabisa Michael Kamaliza!!!!
Nani hajui Margret Sita,kachero Rwehumbiza Anatoli walivyomwangamiza raise wa Kwanza Peter Lebabu Mashanga?
Au walimu wamesahau Katibu was uv ccm yahaya musulwa alivyokuwa akimkaba mkoba?
Nani amesahau ya oluoch na mradi wa ccm kuhakikisha Leah ulaya na mfungwa wa nje seif walivyoingia madarakani CWT?
Changa la macho la wateule wa rais ulaya,maganga na mwenzao kukataa uteuzi wa ukuu wa wilaya litakavyo tumika kuondoa kabisa malengo ya asili ya chama Cha wafanyakazi!!!!!
 
Hatimaye yametimia na bado yataendelea mengi

CWT wameahirisha sherehe zao zilizokuwa zimepangwa kutumia zaidi ya Billioni saba

Sababu zilizotolewa hazina mashiko na ni aibu kuja mbele ya kamera na kuzisema. Haiingii akilini eti Rais amepata dharula kuwa mgeni rasmi hivyo wanaahirisha. Ikiwa kweli alikubali kuhudhuria sherehe hizo, U Rais ni Taasisi hawezi kukosa mwakilishi wa kumtuma kwa niaba yake. Huu ni uongo!

Sababu nyingine wanasema uwanja utakuwa na shughuli ya kiserikali! Hii ni aibu kulisema. Booking ya uwanja ilifanywa, wakapangiwa tarehe ambayo uwanja utakuwa free, wakaja kwenye media wakapromoti! Hiyo shughuli imeshuka toka mbinguni?

rais wa CWT afahamu kwamba si rahisi Rais Samia kukaa meza moja na mtu aliyegomea uteuzi wake!! Tutayaona mengi sana
View attachment 2841035
 
CWT Yaumbuka
Screenshot_20231213_055255_Instagram.jpg
 
Walimu tunawashukuru kwa kutuondolea ujinga na kutufundisha lakini naona hii elimu inashindwa kuwasaidia nyie wenyewe

Mmekua kama mafundi , unakuta fundi ujenz anaishi kwenye nyumba mbovu, fundi randa (carpenter) kwake hata meza au kitanda hana au mlango wa nyumba yake ni wa ovyo nk nk

Walimu poleni sana
 
Walimu nchi hii ni kundi kubwa ila wapo mithili ya nyumbu wengi wao ni kama hawajitambui
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom