Siku Walimu tutakapojitambua

pefla

Senior Member
Jan 31, 2012
105
74
Mwalimu ni mtu anayesaidia wengine/jamii kupata ujuzi, maarifa na tunu katika Nyanja mbalimbali zinazohusu jamii au ulimwengu/dunia. Na majukumu ya mwalimu yanaweza kutofautiana kadiri ya utamaduni husika katika nchi.

Kwa taifa la Tanzania mwalimu amechukuliwa kama shimo la katakata katika fikra fikirishi katika ujenzi wa maendeleo na ustawi wa jamii kwa taifa zima. Ndio maana hata matokeo ya mitihani mbalimbali hasa hasa ya kidato cha nne na sita ya kitangazwa mwanafunzi wa jamii husika anaulizwa umefeli hata alama ya kwenda kusoma ualimu huna? Lakini sio walimu wote wamekuwa walimu kwa sababu ya matokeo mabaya wa mitihani yao bali ni wito na kazi kama kazi nyingine.

Hii yote imetokana na taswira iliyojengwa na taifa letu kwa jamii kuhusu kazi/kada ya ualimu na imepelekea hata viongozi wa ngazi zote serikalini kujenga tamaduni ya kutowajali au kuthamini kada ya ualimu, ndio maana matamko ya kejeli na dharau yote ni ya walimu LAKINI na WAO NI CHIMBUKO LA MWALIMU DHARAULIWA.

Kuna kila sababu ya kuwa na walimu bora ili nao watoe elimu bora katika taifa letu.

Mwaka 1960 miaka mitatu baada ya kupatikana kwa Uhuru wa Ghana, aliyekuwa Rais wakati huo alipeleka bungeni mswada wa sheria ya kuwaongezea mshahara walimu, alisema “Naomba mniunge mkono ndugu wabunge katika hoja ya kupanga mshahara wa walimu wetu’’ anaendelea kusema “Mimi binafsi ni nimelazimika kuja bungeni kuhutubia kwa lengo moja la kuifanya Ghana iwatambue walimu na kuwapa mshahara unaoonyesha umuhimu wao kwa taifa hili. Mimi naamini kwa sababu sioni kama kuna namna unayoweza kutofautisha walimu wa Ghana na hatima au mustakabali wa Ghana’’ hii ni tofauti kidogo na taifa letu kila kukicha miswada iyopelekwa bungeni ni kwa ajili ya kupunja maslahi ya walimu na kuanzisha mifuko kandamizi kama CWT na umuhimu wa mwalimu unaonekana katika kazi zisizokuwa na maslahi kwao kwani tumejengwa katika uzalendo mfilisi kwa maslahi hayo tu.

Kwa mfano usimamizi wa uchaguzi katika ngazi zote (mitaa na uchaguzi mkuu) chaguo lao ni mwalimu na hii inapelekea walimu kuonekana siku zote za utumishi wetu kuwa shimo la TAKATAKA (garbage) katika jamii na kwa viongozi wetu kwani dharau inaoneshwa kupitia ahadi za uongo na ongezeko la shilingi elfu tisa(9,000/=) kwa mwaka. JITAMBUE

Lakini mwalimu anatumia zaidi ya nusu ya muda wake kujiandaa na kuandaa namna ya kumfinyanga mwanafunzi wake ili baadaye tuwe na kizazi bora na viongozi bora zaidi. Ili hili litokee, lazima mwalimu awekwe katika mazingira yanayofaa na yeye afae kwa majukumu anayokabidhiwa sio ahadi za uongo na kejeli juu yetu KUTOKA KWA UZAO WA MIKONO YETU NA JUHUDI ZETU.

Kutokana na kejeli hizo na ahadi za uongo leo kazi ya ualimu haivutii tena; kama leo watoto wa walimu hawatamani kazi ya wazazi wao, kama leo hii asilimia 70 ya walimu wanatamani kuacha kazi, tuna nini cha kujivunia katika taifa letu kama sehemu ya kuleta maendeleo katika taifa letu? Kazi ya kutengeneza taifa bora siyo kazi ndogo.

Na taifa bora litatengenezwa endapo wanaotengeneza watapunguziwa kejeli, dharau na ahadi za uongo na kama tutaendelea kuona elimu ni elimu kwa kushindwa kuthamini na kuwekeza kwa walimu siku chache zijazo tutanunua kila kitu na kutengeneza taifa la kejeli juu ya kada ya ualimu. Kumbuka Rais, Waziri Mkuu na wengine wengi ni kazi ya mikono yetu.

TAMBUA THAMANI YA MIKONO YAKO NA JUHUDI ZAKO
 
Siku entrance qualifications kwenye ualimu itakapobadilishwa Na kuwa....Ni lazima ufaulu Kwa daraja la kwanza ndio upate udahili ndio heshima ya hii kada itarudi. Wewe mtu ana D nne unampaje majukumu ya kuelimisha taifa? Wako inferior Kwa sababu wengi hudhani na (ndio ukweli) kwamba wamepata hizo Ajira kama fadhira!
 
Waalimu ni kama wanafunzi tu. Nilishakiwa kwenye kamati ya chakula kwenye tukio la kiserikali ambapo watumishi wa serikali walialikwa. Sitosahau walimu walikuwa wanagombana kwa sababu ya msosi, yaani ni vurugu mechi.
Sasa watu wa namna hii ni wa kuwadhibiti kipato, vinginevyo watafanya maajabu, serikali iliona hilo
 
Mimi ni mwalimu kwa miaka mingi,japo natamani nikajiendeleze kielimu ili nitoke huku kwenye kuhangaika na vitoto,natamani kuwa tutor/ lecturer baada ya ku- up grade elimu yangu,moja ya vitu vinavyonisukuma ni kuwa mwalimu ana mabos wengi sana kitu ambacho usipokuwa makini kila mtu anakukolomea,na mimi siko hivyo ni mbishi wa asili,kitu kingine sisi walimu ni wanafiki sana,elewa neno wanafiki,tunajipendekeza sana ili kwavurugia wenzetu,mimi siko hivyo,

Kingine nachukia sana CWT,sipendi kabisa kuona wanakata mshahara wangu,nimrjatibu kupambana ili nitolewe nimekwama😭😭😭
 
SIKU WALIMU TUTAKAPO JITAMBUA!

Mwalimu ni mtu anayesaidia wengine/jamii kupata ujuzi, maarifa na tunu katika Nyanja mbalimbali zinazohusu jamii au ulimwengu/dunia.
Na majukumu ya mwalimu yanaweza kutofautiana kadiri ya utamaduni husika katika nchi.

Kwa taifa la Tanzania mwalimu amechukuliwa kama shimo la katakata katika fikra fikirishi katika ujenzi wa maendeleo na ustawi wa jamii kwa taifa zima. Ndio maana hata matokeo ya mitihani mbalimbali hasa hasa ya kidato cha nne na sita ya kitangazwa mwanafunzi wa jamii husika anaulizwa umefeli hata alama ya kwenda kusoma ualimu huna? Lakini sio walimu wote wamekuwa walimu kwa sababu ya matokeo mabaya wa mitihani yao bali ni wito na kazi kama kazi nyingine.

Hii yote imetokana na taswira iliyojengwa na taifa letu kwa jamii kuhusu kazi/kada ya ualimu na imepelekea hata viongozi wa ngazi zote serikalini kujenga tamaduni ya kutowajali au kuthamini kada ya ualimu, ndio maana matamko ya kejeli na dharau yote ni ya walimu LAKINI na WAO NI CHIMBUKO LA MWALIMU DHARAULIWA.

Kuna kila sababu ya kuwa na walimu bora ili nao watoe elimu bora katika taifa letu.

Mwaka 1960 miaka mitatu baada ya kupatikana kwa Uhuru wa Ghana, aliyekuwa Rais wakati huo alipeleka bungeni mswada wa sheria ya kuwaongezea mshahara walimu, alisema “Naomba mniunge mkono ndugu wabunge katika hoja ya kupanga mshahara wa walimu wetu’’ anaendelea kusema “Mimi binafsi ni nimelazimika kuja bungeni kuhutubia kwa lengo moja la kuifanya Ghana iwatambue walimu na kuwapa mshahara unaoonyesha umuhimu wao kwa taifa hili. Mimi naamini kwa sababu sioni kama kuna namna unayoweza kutofautisha walimu wa Ghana na hatima au mustakabali wa Ghana’’ hii ni tofauti kidogo na taifa letu kila kukicha miswada iyopelekwa bungeni ni kwa ajili ya kupunja maslahi ya walimu na kuanzisha mifuko kandamizi kama CWT na umuhimu wa mwalimu unaonekana katika kazi zisizokuwa na maslahi kwao kwani tumejengwa katika uzalendo mfilisi kwa maslahi hayo tu.

Kwa mfano usimamizi wa uchaguzi katika ngazi zote (mitaa na uchaguzi mkuu) chaguo lao ni mwalimu na hii inapelekea walimu kuonekana siku zote za utumishi wetu kuwa shimo la TAKATAKA (garbage) katika jamii na kwa viongozi wetu kwani dharau inaoneshwa kupitia ahadi za uongo na ongezeko la shilingi elfu tisa(9,000/=) kwa mwaka. JITAMBUE

Lakini mwalimu anatumia zaidi ya nusu ya muda wake kujiandaa na kuandaa namna ya kumfinyanga mwanafunzi wake ili baadaye tuwe na kizazi bora na viongozi bora zaidi. Ili hili litokee, lazima mwalimu awekwe katika mazingira yanayofaa na yeye afae kwa majukumu anayokabidhiwa sio ahadi za uongo na kejeli juu yetu KUTOKA KWA UZAO WA MIKONO YETU NA JUHUDI ZETU.

Kutokana na kejeli hizo na ahadi za uongo leo kazi ya ualimu haivutii tena; kama leo watoto wa walimu hawatamani kazi ya wazazi wao, kama leo hii asilimia 70 ya walimu wanatamani kuacha kazi, tuna nini cha kujivunia katika taifa letu kama sehemu ya kuleta maendeleo katika taifa letu? Kazi ya kutengeneza taifa bora siyo kazi ndogo.

Na taifa bora litatengenezwa endapo wanaotengeneza watapunguziwa kejeli, dharau na ahadi za uongo na kama tutaendelea kuona elimu ni elimu kwa kushindwa kuthamini na kuwekeza kwa walimu siku chache zijazo tutanunua kila kitu na kutengeneza taifa la kejeli juu ya kada ya ualimu. Kumbuka Rais, Waziri Mkuu na wengine wengi ni kazi ya mikono yetu.
TAMBUA THAMANI YA MIKONO YAKO NA JUHUDI ZAKO
ualimu ni tunu , ualimu ni wito..

walimu ni watu muhimu sana katika jamii na taifa kwa ujumla. Wanastahili heshima, wanastahili pongezi.
walimu ni watu waaminifu sana, watiifu mno na wasio na tamaa. walimu ni wastaarabu, wastahimilivu na mara zote wana subra..
walimu hawana papara, si wachoyo wa maarifa na ujuzi kwa wanafunzi na taifa kwa ujumla...

Asie na wito wa ualimu hawezi kudumu kwenye jamii au kundi hili muhimu sana kwa Taifa.

Wale walio tayari, basi wachape kazi kwa bidii na kwa weledi mkubwa bila kujali mabezo, kejeli na daima wasikate tamaa kabisa..
Serikali iko pamoja nao wakati wote kuwasikiliza na kuwatimizia yale muhimu yanayowezekana kwa wakati muafaka kulingana na uwezo ulioko.

Mungu Ibariki tanzania..
 
Niliwahi kutana na mwalimu mmoja wa kiume huko Mtwara,akaniambia jinsi mwaka 2015 alivyoshiriki kwenye mchakato wa "uchafuzi mkuu" kwa kuwa msimamizi mkuu wa kituo fulani.
Kwa aliyoniambia ya kupewa vitisho na yeye kusifia kuwa walipewa posho kubwa tu na CCM,nilisikitika sana na kuamini kuwa hii kada haijitambui kabisa.

Yaani mustakabali wako unaweka rehani kisa posho ya elfu 50!!???

Hii kada haijitambui na wala haifai kuonewa huruma mpaka wao wajitambue kwanza na watoke kwenye minyororo ya utumwa.
 
Sijawahi juta kuwa mwalimu

Ila nafurahi sana sijakuwa na kazi nyingine tofauti na ualimu

Ualimu wala sio uzuzu na kama ni uzuzu basi watoto wenu watakuwaje sasa??

Kuna watu wanapenda kuropoka sana.

Sasa mwanao anafundishwa na huyo zuzu. Sasa wewe mzazi ndio zuzu zaidi unamkabidhije mwanao kwa zuzu??
 
Acha kutudhalilisha ,sisi ndo tumefanya ujue kuandika huu upuuzi uliouandika,mbona hamsemi waandishi wa habari ambao hata akiwa na D 2 anaenda kusoma chuo na akishika kalamu ndo anakuwa kama wewe, waliopanga grade za kusoma ualimu ni wasomi wenye viwango vikubwa vya elimu kuzidi wewe,kuwa mstaarabu na kazi za wengine, maslai hatupangi walimu, usitusemange kisa una kipato kuliko mwl.
 
Nimesema Mwl ni sawa na Mchungaji au Pastor Ila Pastor sio Shekhe ingawa Mapastor wengi ni matajiri wanakusanya sana maokoto kuliku mashekhe ni mashekhe wachache sana ambao ni matajiri kwa hio Mwl ni Shekhe aliechangamka
Wabaki hivyo hiyvo
 
Back
Top Bottom