Feedback
JF-Expert Member
- Mar 14, 2011
- 7,988
- 4,507
CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) kimeipa serikali mwezi mmoja kuanzia jana, kuwalipa Sh13 bilioni wanazodai walimu vinginevyo itatangaza mgogoro utakaosababisha walimu kugoma nchi nzima.Hatua hiyo inatokana na kikao cha dharura cha baraza la taifa la CWT, kilichofanyika wiki hii mkoani Morogoro ambacho kilijadili matatizo ya walimu.