Walimu wapewe posho ya kufundishia

Walimu wapewe posho ya kufundishia

haaaaaaa du mm ni mwalm but mnanichekesha hsa ukizngatia mie ni mtoro mpka najiogopa
 
Nakumbuka zamani watoto wa waalimu walijisikia faraja sana kwa kupata vitu vidogo ila nawaambia waalimu wa leo watoto wenu hawawezi kuwasamehe kwa kuona mtoto wa jirani anaenda shule na school bus pale Angel english medium na yeye anakatiza kwa miguu uku kabeba fagio na kidumu mkononi akiwahi chemchem primary,ipo siku atakuhukumu tu ni wakati wenu wa kupambana haswa na acheni hii imani ya kuja kukumbukwa na watawala maana kila mwaka mnadanganywa kama wanakuibia haki zako na wewe waibie muda maana mwisho wa siku ni wewe na familia yako ni aibu kuona watu wanashangaa wakiwaona walimu wanamiliki assets hii ni dharau tosha maana mwalimu akinunua hata baby walker lazima wawaseme kua ni mkopo.
 
Mabadiliko yanaanzia kwako mwenyewe,acha kuwa busy na watoto wa wenzako wakati huna posho,tumia muda mwingi kufanya kazi binafsi,acha kukomaa na wanafunzi utalaumiwa na watoto wako baadae,ushauri zaidi njoo PM,hata mwalimu mwingine unaweza kuomba ushauri

Uko Sahihi Mkuu Kwenye Nchi Yenye Watendaji Ngazi Zote Wasio Na Huruma Na Walimu Tubadilike.Nusu Kazini Nusu Mtaani.
 
Lakini jamani tunapofikilia kero wanazozipaya walimu tucwe na maamuzi ya jazba coz kila kitu kinautatatibu wake wa kifanikiwa so nashauri jaribuni kuyapeleka haya matatizo yenu kwenue ngazi stahili coz yawezekana mkafanikiwa kutatua tatizo hili, huu n uongozi mwengine, alaf kama ukisema uwaache hao wanafunzi mtakuwa mmewafanyia dhulma ebu fikiri kama wewe ungeliachwa ungelikuwa mwalimu.

Serikal Inaweza Ikawa Iko Safi Ila Wanaoharibu Na Kuleta Kero Kwa Walimu Ni Watendaji Wazembe Ambao Wanafanya Kazi Kwa Upendeleo Wanapandisha Madaraja Na Kulipa Malimbikizo Wanapojisikia Ila Dawa Ni Nusu Kazin Na Nusu Mtaani Watanyooka Tu.
 
Mwalimu anaelipwa mshahara laki saba,amesoma miaka mitatu degree,nurse anaelipwa laki tisa amesoma miaka minne na yuko exposed na maradhi kadha wa kadha mule hospitali lakini mwalimu yupo hapa analia lia sana kuwa anaonewa

Acha kufundisha,elimu is unayo nenda kafanye mambo mengine
 
lakini jamani Kauli mbiu yetu ni HAPA KAZI TU. Sasa tutatekelezaje haya kwa kuwa watoro KAZINI ? Bora hata aliyeshauri kukopa benki na kuanzisha biashara.

Utakufa maskini na madeni juu ng'ang'ania hapa kazi tu uone
 
Mwalimu anaelipwa mshahara laki saba,amesoma miaka mitatu degree,nurse anaelipwa laki tisa amesoma miaka minne na yuko exposed na maradhi kadha wa kadha mule hospitali lakini mwalimu yupo hapa analia lia sana kuwa anaonewa

Acha kufundisha,elimu is unayo nenda kafanye mambo mengine

kumbe mwalimu ana angalau kuliko nesi.
Mwalimu katumia muda mfupi kusoma, pia ana muda mwingi wa kufanya mambo binafsi; tofauti na nesi anayeshinda na wagonjwa kutwa, ikibidi analala kazini.
Mi ningekua mwalimu, nisingelalamika wakati nina muda wa kutosha kufanya mambo binafsi.
 
serikal inaweza ikawa iko safi ila wanaoharibu na kuleta kero kwa walimu ni watendaji wazembe ambao wanafanya kazi kwa upendeleo wanapandisha madaraja na kulipa malimbikizo wanapojisikia ila dawa ni nusu kazin na nusu mtaani watanyooka tu.
yaani mwalimu unakuwa unadai haki yako lakini jamaa wanakuchukulia kama tahira fulani hivi, nimestuka..............
 
kumbe mwalimu ana angalau kuliko nesi.
Mwalimu katumia muda mfupi kusoma, pia ana muda mwingi wa kufanya mambo binafsi; tofauti na nesi anayeshinda na wagonjwa kutwa, ikibidi analala kazini.
Mi ningekua mwalimu, nisingelalamika wakati nina muda wa kutosha kufanya mambo binafsi.
tatizo kubwa la baadhi ya waalimu ni kwamba walipata sifuri na baadae wakatumia vyeti vy ndugu zao kusomea ualimu, kwa hiyo hata uwezo wao ni mdogo sana.
 
Kwa hiyo mkuu unamshauri asiwe responsible kwenye kazi yake sio?

Nafikiri siyo sawa mwalimu kutokuwajibika kufundisha watoto aliokabidhiwa. Ni kweli walimu wanafanya kazi nyingi sana ndani na nje ya darasa. Serikali inawajibika kuboresha mshahara wa mwalimu na mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Kwa hali ilivyo sasa walimu hawapo responsible inavyotakiwa aidha kwa kuwa na wanafunzi wengi au vipindi vingi, au kwa uzembe.

Wasimamizi wa walimu nao hawawajibiki ipasavyo; maafisa elimu na wakuu wa shule hawawajibiki kuwasimamia walimu. Hakuna anayejali elimu kwa sababu ya ubinafsi au hofu ya kuchukiwa na jamii au walimu. Magufuli teua waziri makini wa elimu na Tamisemi ili wahakikishe walimu na maafisa elimu wanawajibika.

Wakati tunawataka walimu wawajibike tusisahau kuikumbusha serikali kuboresha mshahara wa mwalimu. Kuliko mwalimu aache kufundisha vizuri ni afadhali aache kufanya kazi zingine kama vile kusimamia michezo.
 
lakini jamani Kauli mbiu yetu ni HAPA KAZI TU. Sasa tutatekelezaje haya kwa kuwa watoro KAZINI ? Bora hata aliyeshauri kukopa benki na kuanzisha biashara.

Atawezaje kusimamia biashara yake wakati huohuo ajiandae na kufundisha vipindi 48 kwa wiki? atawezaje kusimamia biashara wakati huo huo atoe na kusahihisha homework? Ili mwalimu aweze kufanya biashara au mishemishe zake ni lazima awe awe mtoro au asitekeleze majukumu yake kikamilifu. Kwa hali hii Taifa linaangamia.
 
Mabadiliko yanaanzia kwako mwenyewe,acha kuwa busy na watoto wa wenzako wakati huna posho,tumia muda mwingi kufanya kazi binafsi,acha kukomaa na wanafunzi utalaumiwa na watoto wako baadae,ushauri zaidi njoo PM,hata mwalimu mwingine unaweza kuomba ushauri

Umempa jibu zuri sana.
 
kumbe mwalimu ana angalau kuliko nesi.
Mwalimu katumia muda mfupi kusoma, pia ana muda mwingi wa kufanya mambo binafsi; tofauti na nesi anayeshinda na wagonjwa kutwa, ikibidi analala kazini.
Mi ningekua mwalimu, nisingelalamika wakati nina muda wa kutosha kufanya mambo binafsi.

Utakuwa hujui kazi za mwalimu; mwalimu anafanya kazi darasani(kufundisha) na nje ya darasa mfano kusimamia usafi, michezo na kazi zingine kama hizo. Pia mwalimu anatakiwa atoe kazi za kutosha kwa wanafunzi mara baada ya kufundisha na kuzisahihisha; kisha kuwasaidia wanafunzi ambao hawakuelewa mada ili waelewe. Sasa kama ana wanafunzi 300 atamudu kusahihisha kazi hizo ndani ya muda wa kazi (saa 1 - 9:30 mchana)? Jibu ni kuwa haiwezekani; ili akamilishe wajibu huo inabidi aende nyumbani na madaftari ili asahihishe nje ya muda wa kazi; asipofanya hivyo hatawasaidia wanafunzi kuelewa. Baada ya muda wa kazi mwalimu licha ya kusahihisha homework, inabidi ajiandae kufundisha masomo ya siku inayofuata. Sasa muda huo unaosema mwalimu anao kwa ajili ya kufanya kazi za uzalishaji mali upo wapi?

Ni kweli walimu siku hizi wapo busy na mambo yao binafsi hasa ya uzalishaji mali kwa sababu na wao wanahitaji maisha bora ambayo hayawezi kupatikana kwa kutegemea mshahara. Ili wafanye kazi hizo za uzalishaji mali, inabidi wasifanye kazi ya mwalimu kadiri ya taaluma ya ualimu. Siku hizi walimu wengi hawajiandai kufundisha masomo yao; wanaingia darasani ili mradi tu aonekane amefundisha.
 
Kwanza napenda kuzungumza kuna watumishi wengine bado ni woga sana yaani mtumishi ananyanyaswa na mwenyekiti wa kijiji na bado hapo hapo wanakijiji wanakuwa wanasauti kuliko maafisa au mkurugez yaan wanakijiji wanajickia kusema mwalimu huyu hatumtaki na viongoz wa juu wanafuata hayo na kumuonfoa HV mwalimu ni nani?mbona tunanyanyasika kiasi hicho....kwa upande wangu nasema walimu tuwe jasir na wakakamavu tusikubali kuyumbishwa kam gari bovu.....kama nambaaa wataisomaaa tu hakuna kubabaishwa MTU kwani wajibu wetu tunatekeleza kwann MTU baki tu aje kuzuia haki zetu ,nasema mwalim kama unashughuli zako binafsi zifanye tens kwa ufasaha bila kuogopa lolote lile
 
Walimu wapewe posho za kufundishia ni sawa

Walimu wapewe mishahara sawa na madaktari na mafamasia ni sawa

Ila sio kwa walimu wa hii generation.Sisi kama taifa tuamue kuwa kuanzia mwaka kesho tunabadili required qualification za mtu kuwa admitted into programms za ualimu ziwe kubwa kama au zaidi ya udaktari(kwa mfano).Yani wanafunzi waliofaulu sana ndio wakawe walimu na product yao ndio ianze kuneemeka na maposho na masalary manono

Hatuna tatizo na walimu wetu,
 
Back
Top Bottom