Matatizo ya waalimu yanaanzia kwenye ngazi ya chini kabisa mashuleni, walimu wakuu na wakuu wa shule wamegeuka miungu watu na kwa utawala huu nihatari zaidi kwa mwalimu kwani mkuu wa shule anaweza kumuandikia taarifa mbaya kwa Afisa Elimu ikawa kesi na matatizo makubwa.
Maafisa elimu wengi ni vilaza na wanawaogopa sana walimu wanaojielewa hivyo ukionekana unaleta ujuaji wa kila siku utatengenezewa kesi zisizoisha kila siku na faili litaharibika, wakati huo DED na DC hawatakutetea hata kidogo utabigwa ban la nguvu ukitoa mguu kituo cha kazi taarifa ilishafika hadi kwa waziri mkuu kuwa kuna mwalimu ameenda sokoni bila kuaga, na mshahara utafungwa muda huohuo.
Waalimu ndio wanaocheleweshewa hata kupanda madaraja ya mishahara na wengine wanakuwa nyuma hata kama ulianza mwaka mmoja na wengine utajikuta daraja lako liko nyuma na ukienda kwa afisa utumishi utaambulia matusi na kejeli zakijinga sana, utaonekana kama hukustahili hata kuitwa mwalimu kwani walimu wenzio wanamatatizo kama yako na wametulia ila wewe unaleta kimbelembele. Walimu wengi ni WANAFIKI wakubwa sana, kupikiana majungu kwa wakuu wa shule na maafisa elimu na wakurugenzi. utakuta mwalimu hampendi mwenzie kisa anapiga sana ngeli kuliko yeye. sasa huyu atakubali kuweka kunji la pamoja???
TAHOSSA ndio liumoja lingine lakijinga sanab katika kada ya ualimu. mm niliwahi kuwauliza hivi nyinyi tahossa mnashindwa kuwa na hata stationary yakuchapa na kutoa kopi mitihani yenu wenyewe kila siku mnapeleka tenda kwa watu binafsi, nikaja kustuka zile stationaries nizao wenyewe. TAHOSSA wakikutana wanaongelea walimu wakorofi katika mashule yao na jinsi yakuwadhibiti na wanapeleka mapendekezo kwa maafisa elimu kuwa umetuletea walimu wajorofi sana, mwalimu anakuwa yupo chini ya uangalizi wamajungu na fitna bila kujua. basi ni kero kila kukicha.
Mimi niliacha ualimu baada yakuvimbiana na kiafisa elimu kimoja hivi huko maporini nikamwambia kwaheri, hakuamini nikarudi nikafunga virago vyangu safari hadi kesho huu i mwaka wa 5 sasa. walimu msiwe wanyonge hao jamaa wanaowaendesha mkipata nafasi mnakunja ngumi, unamtoa meno 3 alafu unatafuta laki 5 za kesi.
Kuna kichama kingine chakipumbavu sana kinaitwa TSD, yaaaaaaani duuuuuuuuu walimu ni SHIIIIIIIIIIIIIIDA, ukiwaona hawa TSD ni vibabu flani vikoloni kishenzi yaani vimekaa pale kusubiri mwalimu ateleze apewe barua za nidhamu sijui ujinga gani, hawa wote ni wakoloni wanao waandama walimu na walimu hawana pakutokea masikini ya MUNGU. wamekuwa wanyonge sana, mara mkuu washule, akigeuka huku anakuta cwt, hajakaa sawa MEK, hajapinduka upande mwingine tsd, huku kuna madiwani nao wanawaandama walimu hatari. WALIMU SIO KAZI, UKITAKA UMASIKINI JIINGIZE HUKO