Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,011
- 9,878
ZAIDI ya walimu 50 wenye asili ya Kiafrika kwenye shule ya Sekondari ya The Agha Khan Mzizima wamegoma kuingia darasani kufundisha wanafunzi kwa kile walichodai kuwa uongozi wa shule hiyo umekuwa ukiwanyanyasa na kuwabagua kwa rangi.
MwanaHALISI kupitia chanzo cha kuaminika kilipata taarifa hizo na kufika shule hapo kushuhudia mgomo huo ulianza leo tarehe 24 Mei 2022 asubuhi.
Mwandishi wetu alipofika shule hapo aliwakuta wanafunzi wakirandaranda nje ya madarasa huku walimu wenye asili ya kitanzania wakiwa hawaonekani eneo hilo.
Mwandishi alifika mapokezi kwa ajili ya taratibu za kupata taarifa hizo na chanzo cha mgomo huo alimsikia mwanafunzi mmoja akimuomba mwalimu wa kike ruhusa “madam kama hatusomi mturuhusu turejee nyumbani mapema”
Hata hivyo uongozi wa shule hiyo haukuwa tayari kuzungumzia suala hilo lakini Mwana HALISI ilipata nafasi ya kuzungumza na walimu wa shule ambao walikuwa wamejikusanya pamoja kwenye jengo la nyuma wakisisitiza kuwa wamegoma kwa kile walichokidai kukithiri kwa ubaguzi na unyanyasaji.
Mwalimu Mohammed Haji mwalimu anayefundisha somo la Baiyolojia kwenye shule hiyo amesema kuwa shule hiyo ina waalimu wa kiafrika na walimu wanaotoka bara la Asia ambao wengi ni wahindi.
‘’Likifika suala la uamuzi, rangi inakuwa kigezo na wahanga wakubwa ni sisi watanzania, mpaka inafika kipindi tunakuwa hatuna imani na kesho yetu kwa sababu hapa unaweza kuzushiwa chochote kuchafuria CV zako mfano wale wenzentu waliosingiziwa kuvujisha mitihani.
“Mwaka jana kulitokea suala la kuvuja mitihani ambapo sisi tuna mashaka na kuvuja kwa mitihani hiyo lakini bila sababu yoyote walimu wa Kitanzania watatu waliangushiwa jumba bovu na kufukuzwa kazi, sisi ni watu wazima mambo yote yanayotokea hapa tunayaona,”amesema Haji.
Haji amesema kuwa ubaguzi huo umekwenda mbali mpaka kwenye masuala ya malipo kwa kuwa walimu wa kigeni wanalipwa kiwango cha juu mara nne zaidi ya kiasi cha Mtanzania ikiwa kiwango cha utendaji kazi ni sawa, “Tena walimu wa kitanzania wanafanya kazi zaidi”.
Anasema kuwa walimu wa Kitanzania hawaheshimiki, “ sisi walimu wa Kiafrika unaweza ukakemewa mbele ya wanafunzi na ukienda kulalamika unapewa onyo kali lakini hata kwenye ajira akiondolewa Mtanzania ataletwa raia wa kigeni na atapewa kiwango kikubwa cha mshahara.
“Tunanyanyaswa mpaka na walimu wenzetu wale wahindi wanatuona kama watu wa Second Class kwenye taasisi hii”
Issa Sumbi Mwalimu wa shule hiyo amesema kuwa ubaguzi huo unawaathiri na kwamba hivi karibu wameondolewa kazini walimu takribani watano bila kuwepo kwa sababu yoyote na waliojaza nafasi zao ni walimu wa kihindi.
Pamera Mboya Mwalimu wa TEHEMA katika shule hiyo amesema kuwa chanzo cha kuondolewa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ambaye alikuwa akisimama kutetea haki za walimu wa Kitanzania shuleni hapo kinaukakasi na kwamba wanahisi kuwa kuna shinikizo.
Samweli Kameme ni mmoja wa walimu wa The Agha Khan Mzizima amekiri kuwa uongozi wa shule huo unawabagua walimu hao wenye asili ya kiafrika.
“Unyanyasaji huu unafanyika kwa wazi kwetu sisi walimu kwa kubaguliwa na uongozi wa shule hususani Mkurugenzi wa shule anajua anachotenda hasa sisi walimu weusi , tunanyanyasika kwenye nchi yetu kwa kweli inauma”
“Mikataba inasitishwa bila sababu za msingi, wakiondolewa kazini walimu wa kiafrika wanaletwa walimu wenye asili ya kihindi tunaamini Rais Samia ataliona hili tunabaguliwa kwenye ardhi yetu,’ ameongeza.
John Kayoa Ofisa Rasilimali watu (HR) Msaidisi wa shule hiyo ambaye alimtaka mwandishi wa habari hizi aache maswali yake yote kwake ili siku inayofuata apate majibu.
Kayoa amesema kuwa kuhusu tuhuma za ubaguzi anaweza kuzisemea kidogo kuwa si za kweli.
“Unajua Mwandishi hapa kuna watu wanaotoka nchi tofauti tofauti na kila mtu anautamaduni wake hayo mambo hayana ukweli na kuhusu ajira kwa walimu wa kigeni sisi tunawaalimu zaidi ya 103 kwenye hao walimu raia wa kigeni ni walimu 13 tu,” amesema.
MWANAHALISI
MwanaHALISI kupitia chanzo cha kuaminika kilipata taarifa hizo na kufika shule hapo kushuhudia mgomo huo ulianza leo tarehe 24 Mei 2022 asubuhi.
Mwandishi wetu alipofika shule hapo aliwakuta wanafunzi wakirandaranda nje ya madarasa huku walimu wenye asili ya kitanzania wakiwa hawaonekani eneo hilo.
Mwandishi alifika mapokezi kwa ajili ya taratibu za kupata taarifa hizo na chanzo cha mgomo huo alimsikia mwanafunzi mmoja akimuomba mwalimu wa kike ruhusa “madam kama hatusomi mturuhusu turejee nyumbani mapema”
Hata hivyo uongozi wa shule hiyo haukuwa tayari kuzungumzia suala hilo lakini Mwana HALISI ilipata nafasi ya kuzungumza na walimu wa shule ambao walikuwa wamejikusanya pamoja kwenye jengo la nyuma wakisisitiza kuwa wamegoma kwa kile walichokidai kukithiri kwa ubaguzi na unyanyasaji.
Mwalimu Mohammed Haji mwalimu anayefundisha somo la Baiyolojia kwenye shule hiyo amesema kuwa shule hiyo ina waalimu wa kiafrika na walimu wanaotoka bara la Asia ambao wengi ni wahindi.
‘’Likifika suala la uamuzi, rangi inakuwa kigezo na wahanga wakubwa ni sisi watanzania, mpaka inafika kipindi tunakuwa hatuna imani na kesho yetu kwa sababu hapa unaweza kuzushiwa chochote kuchafuria CV zako mfano wale wenzentu waliosingiziwa kuvujisha mitihani.
“Mwaka jana kulitokea suala la kuvuja mitihani ambapo sisi tuna mashaka na kuvuja kwa mitihani hiyo lakini bila sababu yoyote walimu wa Kitanzania watatu waliangushiwa jumba bovu na kufukuzwa kazi, sisi ni watu wazima mambo yote yanayotokea hapa tunayaona,”amesema Haji.
Haji amesema kuwa ubaguzi huo umekwenda mbali mpaka kwenye masuala ya malipo kwa kuwa walimu wa kigeni wanalipwa kiwango cha juu mara nne zaidi ya kiasi cha Mtanzania ikiwa kiwango cha utendaji kazi ni sawa, “Tena walimu wa kitanzania wanafanya kazi zaidi”.
Anasema kuwa walimu wa Kitanzania hawaheshimiki, “ sisi walimu wa Kiafrika unaweza ukakemewa mbele ya wanafunzi na ukienda kulalamika unapewa onyo kali lakini hata kwenye ajira akiondolewa Mtanzania ataletwa raia wa kigeni na atapewa kiwango kikubwa cha mshahara.
“Tunanyanyaswa mpaka na walimu wenzetu wale wahindi wanatuona kama watu wa Second Class kwenye taasisi hii”
Issa Sumbi Mwalimu wa shule hiyo amesema kuwa ubaguzi huo unawaathiri na kwamba hivi karibu wameondolewa kazini walimu takribani watano bila kuwepo kwa sababu yoyote na waliojaza nafasi zao ni walimu wa kihindi.
Pamera Mboya Mwalimu wa TEHEMA katika shule hiyo amesema kuwa chanzo cha kuondolewa Mwalimu Mkuu wa shule hiyo ambaye alikuwa akisimama kutetea haki za walimu wa Kitanzania shuleni hapo kinaukakasi na kwamba wanahisi kuwa kuna shinikizo.
Samweli Kameme ni mmoja wa walimu wa The Agha Khan Mzizima amekiri kuwa uongozi wa shule huo unawabagua walimu hao wenye asili ya kiafrika.
“Unyanyasaji huu unafanyika kwa wazi kwetu sisi walimu kwa kubaguliwa na uongozi wa shule hususani Mkurugenzi wa shule anajua anachotenda hasa sisi walimu weusi , tunanyanyasika kwenye nchi yetu kwa kweli inauma”
“Mikataba inasitishwa bila sababu za msingi, wakiondolewa kazini walimu wa kiafrika wanaletwa walimu wenye asili ya kihindi tunaamini Rais Samia ataliona hili tunabaguliwa kwenye ardhi yetu,’ ameongeza.
John Kayoa Ofisa Rasilimali watu (HR) Msaidisi wa shule hiyo ambaye alimtaka mwandishi wa habari hizi aache maswali yake yote kwake ili siku inayofuata apate majibu.
Kayoa amesema kuwa kuhusu tuhuma za ubaguzi anaweza kuzisemea kidogo kuwa si za kweli.
“Unajua Mwandishi hapa kuna watu wanaotoka nchi tofauti tofauti na kila mtu anautamaduni wake hayo mambo hayana ukweli na kuhusu ajira kwa walimu wa kigeni sisi tunawaalimu zaidi ya 103 kwenye hao walimu raia wa kigeni ni walimu 13 tu,” amesema.
MWANAHALISI