Tangazo lilisema watalipwa sh.30,000/= (Makarani na Wasimamizi wasaidizi wa vituo) na sh.35,000/=(Wasimamizi Wakuu wa vituo) kwa siku 1,semina sh.30,000/= kila mtu kwa kila siku 1 ya kazi . Kusema kweli iliyoandikwa ilikuwa pesa ndogo sana na iliandikwa hivyo ili kuwakatisha tamaa watu wengi wasiombe kazi hiyo.
Ila kusema kweli jamaa walilipwa kati ya sh.290,000/= (Wasimamizi Wasaidizi) na sh.360,000/= (Wasimamizi Wakuu) kwa hizo siku 2 za kazi. Na 70% ya pesa hiyo walilipwa kabla ya kazi na ile 30% wakamaliziwa kesho yake. Wewe hiyo pesa ulikuwa huitaki?
Halafu suala la dola kufanya udanganyifu kwenye Uchaguzi hata wewe ungekuwa ndo unasimamia Uchaguzi kwenye kituo usingeweza kulizuia.Zuia uhatarishe maisha yako.Wewe ungeweza? Note:Kwa kusema hivi simaanishi kwamba naunga mkono 'ujambazi' uliofanyika.
Kama unadhani wewe ungeweza kuzuia wizi wa kura, kwanini hukushiriki kulinda kura hizo ili zisiibiwe na badala yake ukakaa mita 45,000 kutoka kituo cha kupigia kura (ilhali Upinzani ulikuwa unahamasisha wananchi wakalinde kura) ? Wewe pia unapaswa ulaumiwe kwa hili.
Pia,kwanini hukujitokeza kuandamana kupinga matokeo pale Viongozi wa Chadema walipohamasisha maandamano? Hapa napo huwezi kukwepa lawama.
Mwisho kabisa:Ishu hapa ni kwamba "the deep state" au the "bad boys" au "kitengo" walikuwa wamedhamiria kufanya ujambazi huo kiasi kwamba HAO WALIMU UNAWALAUMU BURE, NA HATA WEWE HUNGEWEZA KUWAZUIA "WASIOJULIKANA" KUFANYA YAO.